Smile
JF-Expert Member
- Jul 18, 2011
- 15,347
- 11,610
UNAPOKUWA NI MCHUMBA WA MTU, HASWAKWA YULE AMBAYE UNAFIKIRI AU UNATEGEMEA ATAKUWA MUMEO,, NI VIZURI KUZINGATIABAADHI YA VIPENGELE HUSIKA VYA KULETEA HESHIMA YAKO KWENYE KIPINDI CHA MAHUSIANO
1 Usivaenguo za kuacha maungo yako wazi, usipende kutoka bila kumjulisha, unapotoka kwaruhusa yake au kwa kumpatia taarifa, hakikisha unaporudi unampa taarifa,usipende kufanya simu yako private sana, unapoongea na simu hakikisha baadhi yamaongezi yako ambayo sio delicate anayasikia, usipende kuwa mficha simu na kuwana vitu vya siri siri mpaka akakushtukia
2 Anapokutambulisha kwa marafiki zake, usionekane kuwafurahia sana walemarafiki zake , na wala usihitaji simu zao, akitaka kukupatia simu, mwambienitachukua kwa my (mchumba wako) Usipende kuwa na marafiki wa kike ambao niwale walioshindikana, au viruka njia, au wasiofaa hata kutambulisha.. Muonyesheunajali wazazi wako tangu mwanzo kabisa, kila kitu ukiongea usiache kuzungumziamzazi wako kwa njia moja au nyinginge
3 Unywaji wa pombe si jambo bora kwa msichana ambaye anategemea kuwa mamaBora, unashauriwa usipende sana kukaa bar au kunywa pombe , ni vizuri ukitolewaout na mpenzi wako akupeleke maeneo ambayo yana hadhi yako, na si mahali ambaokuna wingi watu, au mahali ambapo kila mwanamke anaingia,, ziko sehemu nzuriambazo zina ustarabu na si ghali sana, usipende mabaaa ya uchochoroni, hukondiko mnaopoibiwa waume zenu, kwani wanawake machangu wamejaa tele nahuwakodolea mimacho
4 Unapokuwa na mpenzio mahali popote, usipende kumsifia mwanaume mwingineyeyote kuwa ana gari zuri, kazi nzuri, au anavaa vizuri, hata kunukia vizuri,hii inamfanya mpenzio ajishushe hadhi, wakati wowote uwe tayari kumsifia yeyekama yeye, hii inamsaidia kumtia moyo na kuongeza juhudi kwenye kilaanachokifanya, Ni vizuri kumuonyesha kuwa kila kitu chake unakipenda, na kilaanachofanya amejitahidi, kama kuna kumkosoa au kumrekebisha basi kuna mahaliambapo au siku ambayo ni rasimi kumwambia kila unachofikiri kitamsaidia
5 Usiwe mstari wa mbele kumsapoti pale anapokuambia kuhusu udhaifu wa nduguzake, wazazi wako au boss wake, Tumia akili ya ziada kutoa mchango wako kwenyekila kitu atakachokushirikisha, ,, kumbuka yeye ni mume tu na kwenye mapenziyake yamejigawanya kwenye maeneo mengi, .. kazi, wazazi, ngudu, marafiki nk..hivyo usifikiri wewe peke yako ndiye unayehitaji upenzi wake..
6 husninyo swiitlady,afrodenzi lizzy ,firslady ,kongosho endeleeni