Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,038
- 2,199
Kwanza kabisa natoa pongezi nyingi kwenu kwa kuchaguliwa au kuteuliwa ili muweze kutetea maslahi ya wananchi wote wenye itikadi mbalimbali.
Baada ya wananchi kuridhishwa na kazi iliyofanywa na wabunge wachache wa chadema miaka mitano iliyopita waliamua kuongeza idadi yenu wakitarajia mambo makubwa zaidi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Hakuna ubishi kwamba CDM ni chama cha siasa kilichojijengea heshima na uaminifu mbele ya watanzania kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.kutokana na ukweli huu CDM imeongeza idadi ya maadui wakiongozwa na CCM ambaye ni adui hatari aliyejeruhiwa.kuna mambo matatu ambayo CCM kama majeruhi anaweza kufanya:
1.FEAR-hili ni jambo la kwanza lilotokea/linaendelea kutokea.
2.FIGHT-hili ni jambo la pili linaloweza kutokea iwapo CCM inaamini kuwa uwezo wa kupambana na CDM upo.
3.FLIGHT-hili litatokea pale CCM itakapoona kuwa CDM is like a giant na hivyo kuamua kujiweka pembeni/kukimbia kama kunguru.
Nionavyo CCM watatumia reaction ya pili,wataamua/wameamua kupambana.ni haki yao kupambana tena kwa kutumia mbinu zote(pamoja na coalition zisozokuwa rasmi) kabla ya kuamua kukimbia.
Hivyo waheshimiwa wabunge wa CDM mko kwenye vita kali sana huku mkiwa na vifaa duni lakini mnayo SILAHA moja nayo si nyingine ni 'spirit' ya wapenda mabadiliko ambao ni wengi na wanaendelea kuongezeka.
Mpigane kufa na kupona bila kutumia panga au ngumi bali hoja thabiti zinazogusa maslahi ya umma wa watanzania.waacheni wengine waendelee na 'mipasho' wakati nyinyi mkitoa lyrics za ukombozi.
Asanteni kwa kunielewa.
MUNGU IBARIKI TANZANIA!!
Baada ya wananchi kuridhishwa na kazi iliyofanywa na wabunge wachache wa chadema miaka mitano iliyopita waliamua kuongeza idadi yenu wakitarajia mambo makubwa zaidi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Hakuna ubishi kwamba CDM ni chama cha siasa kilichojijengea heshima na uaminifu mbele ya watanzania kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.kutokana na ukweli huu CDM imeongeza idadi ya maadui wakiongozwa na CCM ambaye ni adui hatari aliyejeruhiwa.kuna mambo matatu ambayo CCM kama majeruhi anaweza kufanya:
1.FEAR-hili ni jambo la kwanza lilotokea/linaendelea kutokea.
2.FIGHT-hili ni jambo la pili linaloweza kutokea iwapo CCM inaamini kuwa uwezo wa kupambana na CDM upo.
3.FLIGHT-hili litatokea pale CCM itakapoona kuwa CDM is like a giant na hivyo kuamua kujiweka pembeni/kukimbia kama kunguru.
Nionavyo CCM watatumia reaction ya pili,wataamua/wameamua kupambana.ni haki yao kupambana tena kwa kutumia mbinu zote(pamoja na coalition zisozokuwa rasmi) kabla ya kuamua kukimbia.
Hivyo waheshimiwa wabunge wa CDM mko kwenye vita kali sana huku mkiwa na vifaa duni lakini mnayo SILAHA moja nayo si nyingine ni 'spirit' ya wapenda mabadiliko ambao ni wengi na wanaendelea kuongezeka.
Mpigane kufa na kupona bila kutumia panga au ngumi bali hoja thabiti zinazogusa maslahi ya umma wa watanzania.waacheni wengine waendelee na 'mipasho' wakati nyinyi mkitoa lyrics za ukombozi.
Asanteni kwa kunielewa.
MUNGU IBARIKI TANZANIA!!