Kwa vile tatizo ni CCM, Rais Vunja Bunge chini ya Article 90 ya Katiba

Wazo zuri kama kujenga daraja la kutoka Dar mpaka Zanzibar, inawezekana lakini ngumu kama ngamia kupita kwenye tundu la sindano
 
Japo sina takwimu sahihi ya wizi na ufisadi unaofanyika kwa mwaka< ama kwa hakika fedha wanazofuja huko serikalini kwa miezi sita tu zinatosha kuitisha uchaguzi mkuu mpya na tukapita salama. tukijidanganya kua ni gharama kufanya hivyo tutakua sawa na mtu anayedhani kula kipande cha mkate asubuhi na kujikalia nyumbani ni bora kuliko kuliko kwenda shambani kwake mwenyewe kuvuna gunia la mahindi kwa lishe yake ya siku zijazo. ajue akiyaacha huko yataliwa na nyani na yatakayoanguka chini kuliwa na mchwa
 
gharama za uchaguzi tutachangia sisi wapiga kura wenyewe kama ilivyo kwa M4C, tumechoka.
 
HAIWEZEKANI
Kwa hulka na silka ya wabunge wa CCM, (walio wengi) suala hili litakuwa gumu kufanyika kwani wengi wao ni wabinafsi na wametanguliza maslahi yao nay a vyama vyao mbele. Kwa mantiki hiyo hawana uhakika na mustakabali wao mbele ya wapiga kura wao kama hili likitokea.

Nionanavyo mimi, hili unalopendkeza linategemea sana busara na maono ya Rais, hivyo ninakubaliana nawe kama Rais atafanya hivi ili kuondoa mzizi wa tatizo. Wait a minute, did I say kuondoa mzizi wa tatizo? Kwan uchaguzi ukirudiwa baada ya miaka mitatu, hizi kansa zinazotukabili zitakuwa zimeshatuisha? Hebu fikiria suala la uhuru wa tume, ya uchaguzi, daftari la wapiga kura, sheria mbovu za uchaguzi, rushwa kwenye uchaguzi, kuteuwana, uwajibikaji duni &#8230;. (list inaendelea)

Nionavyo mimi hata uchaguzi ukifanyika sasa hivi, sehemu kubwa ya matokeo yake itakuwa kama sasa, hivyo ni wito wangu, kwa watanzania wenzangu kuchukua hatua sasa. Tatizo letu sisi, tunatawaliwa na HOFU, ULALAMIKAJI, na KUTOKUWA NA ARI YA KUCHUKUA HATUA.

Haiwezekani polisi wauwe watu halafu sisi, tunakalia matamko (tunapaswa kuchukua hatua)
Haiwezekani serikali ifuje mali za UMMA halafu sisi tuzidi kulalamika, (tunapaswa kuchukua hatua)
Haiwezekani bei ya bidhaa ipande bei kwa kasi hii, halafu sisi tukae na kulalamika (tunapaswa kuchukua hatua)
Haiwezekani wahuni wagawe bandari bure halafu tuzidi kulalamika, (tunapaswa kuchukua hatua).
Haiwezekani watoa rushwa wakubwa walindwe, na PCCB hafu sissi tuzidi kulalamika
Haiwezekani wabunge washindwe kuiwajibisha serikali wakati wana meno, (ni lazima tuchukue hatua),
Haiwezekani Tume ya Uchaguzi ishindwe kuhuisha daftari la kudumu la wapiga kura, wakati teknolojia iliyopo inaruhusu tena kwa gharama nafuu (ni lazima tuchukue hatua)

HAIWEZEKANI, SASA TUSEME IMETOSHA. TUTOKE KWENYE ULALAMIKAJI TWENDE KWENYE UTENDAJI (Zitto ameonyesha njia ya hili huko Bungeni, na sisi tuonyeshe hili huku Mtaani)
 
Mkuu MMM impeachment unayoirejea iko ibara ya 46A ile ya 46 inapiga marufuku kumshtaki Rais akiwa madarakani. Mkuu nadhani Wabunge kwa maana ya Zitto ameangalia vizuri vifungu hivyo na kugundua kwamba ni vigumu sana kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais. Ukirejea Ibara ya 46A (2) vifungu vidogo vya (a), (b) na (c) utagundua ilivyo ngumu kumshtaki Rais. Ila ukirejea ibara ya 53A na Ibara ya 52 hasa ibara ndogo ya 1 basi utaona mambo yale yaliyoongelewa Bungeni jana yanamhusu PM moja kwa moja na kwa mujibu wa ibara hizo ni rahisi kupiga kura ya kutokuwa na imani naye kwa mujibu wa Katiba. Hii itaonyesha hasira za wabunge kwa serikali na Rais itabidi awe makini kuanzia hapo.
Umeenda nje ya topic....nani amependekeza anamshitaki rais hapa?Impeachment is lawful procedure .Hujiulizi hata kwa nini wanahitaji idadi saini n.k kabla ya zoezi,,,,,,
Kwani impechment kwa rais iko nje ya katiba?
 
Kuvunja bunge na kufanya uchaguzi mpya ni hatua kali na yakishupavu lakini haitasaidia kwa sasa kwasababu system iliyowaweka madarakani waliopo leo bado inanguvu ileile yakuwarudisha. Wengi tunaamini serikali iliyopo madarakani imeingia kwa mgongo wa vyombo vya usalama.

Tukiitisha uchaguzi mwingine kwakutumia utaratibu wa 2010 (katiba na vyombo vya usalama) tusitegemee matokeo tofauti sana. Wananch wameamka wanaona maovu lakin kwa namna moja au nyingine vyombo vya usalama vinanufaika na waliopo madarakani ndio maana ni rahisi kurubuniwa au kuamrishwa kusimamia matakwa ya wezi/mafisadi/manyang'au au wahujumu uchumi.

Kubadilisha baraza la mawaziri peke yake hakutaleta matokeo mazuri sana na kubadilisha maisha ya mtanzania. Baraza la mawaziri libadilike na hatua kali zichukuliwe.

Hakika wazo la rais kuvunja bunge ndilo hasa litakalo leta mabadiliko, maana hata hiyo katika ya JK itakuwa imebadilika cover tu, contents zitabaki kuwa zile zile!! Vyombo vya usalama vitabaki kuwa vile vile vyenye kuwajibika kwa JK. Sababu ya kushindwa kusimamia vyema kodi yaweza kuiondoa CCM madarakani hata sasa!!

Kwa kuwa wananchi wameanza kupata mwanga wa haki zao, hakika rais akivunja bunge sasa hivi na uchaguzi ukarudiwa; CDM wakajenga hoja vizuri kwa wananchi CCM itakuwa hoi na chali. Munkari wa hali ya wananchi utachochea vizuri kuiangusha!!!
 
Umeenda nje ya topic....nani amependekeza anamshitaki rais hapa?Impeachment is lawful procedure .Hujiulizi hata kwa nini wanahitaji idadi saini n.k kabla ya zoezi,,,,,,
Kwani impechment kwa rais iko nje ya katiba?

Mkuu soma post ya MMM na post yangu pia rejea ibara za katiba ambazo nimeweka hapo. Impeachment ni mashtaka siyo ya mahakamani bali kwa utaratibu wa kibunge. Niko ndani ya topic. Nilichokifanya ni kumkumbusha MMM kwamba ibara ya 46 ni mashtaka mahakamani na Ibara ya 46A ni mashtaka ya Bungeni. Lakini nikaenda mbele zaidi na kusema kwa ibara hizo ni vigumu sana kufanya impeachment kwa Rais kuliko waziri Mkuu. Soma Katiba mkuu ili wakati wa kutoa maoni ya katiba mpya uwe na cha kuchangia katika mchakato wa kumshtaki rais bungeni ili iwe rahisi kuliko sasa.
 
MMK, ni lazima ujue kuwa through kuitikisa serikali ya CCM kwa kutumia bunge tunaweza kujikuta upinzani tukipata mashiko(kuongeza wanachama)good willing, pia siamini sana kama Tanzania hii impeachiment inawezekana, Ibara ya 46A imeweka wazi kuwa kikatiba Rais anaweza kupigiwa kura na bunge na kuondolewa madarakani, ila kwa wabunge wa CCM ambao ndiyo wengi .....sijui,
 
kwangu mimi hizi zote ni sarakasi tu, tatizo ni rais mwenyewe, hii ripoti kabla haijaenda bungeni yeye ndiye aliyekuwa wa mwanzo kukabidhiwa, hakuyaona hayo madudu, hivi kweli wewe kama mtawala bora unasubiri wabunge wakwambie nini ufanye, tatizo ni rais, jingine silioni
 
Gharama ya kuitisha uchaguzi sasa hivi ni ndogo sana kulinganisha na gharama ya wao kuendelea kutawala kwa miaka mitatu iliyobakia!

Nadhani unasahau utekelezekaji na uhalisia wa unayoyasema. Kama alivyosema Mh Zitto, tusche kuwa walalamikaji, tuwe watendaji, naongezea tuwe watendaji wahalisia. Atakaevunja bunge ni Rais gani? Huyu huyu Kikwete aliyeshindwa kumuwajibisha Jairo, Ngeleja, waziri Mwinyi, mama katibu (wizara ya afya) na wengineo, do you think hilo litatokea???
Besides hata naamini hata wewe ungekuwa Rais naamini isingekurupukia kuvunja bunge, unless you've run out of more sensible option.
Nashukuru kwa mchango wako, but I think umekua just too ambitious and unrealistic.
 
Mawazo ya watu kama hawa ndiyo yanawapa upenyo hawa wezi. Mtu anaona kuitisha uchaguzi ni gharama, lakini ndege mbovu inayokodishwa kwa dola milioni 200 haoni kama inamgharimu zaidi. VIP Lounge inayojengwa pale uwanja wa ndege kwa dola milioni 8 haoni kama ni tatizo. Na kibaya zaidi, haya ni awazo ya mtu anayejiita revolutionary na msomi.

Sioni tatizo lounge kujengwa kwa hicho kiwango as long as thamani ya pesa imezingatiwa.
Kwa mawazo yangu silengi kuwapa wezi upenyo ila ningependa tuwe wajalisia zaidi katika kutafuta suluhu ya mambo. I just dont think Rais kuvunja bunge is more sensible kuliko option ya mh Zitto. Besides it wont happen, lets not hallucinate and bring our arguments as practical individuals.
 
Sidhani kama wabunge wa CCM wako tayari kumsulubisha mwenyekiti wa chama chao kwa kura ya kutokuwa na imani...ukiitishwa uchaguzi sasa hivi zaidi ya nusu ya wabunge wa ccm wanaweza wasirudi!!
 
Ni kweli gharama za kurudia uchaguzi ni kubwa kulinganisha na gharama za kuendelea kutawaliwa na ccm!
 
Kikwete ni mnaf*ki na kiburi, hawezi kufanya kitu kama hiyo. Fisadi analinda Mafisadi wenzake
 
Back
Top Bottom