zema21
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 619
- 251
Ikiwa ni miezi sita imepita toka yalipofanyika mahafali ya katika chuo kikuu cha Dodom(Udom) inashangaza sana kuona ni jinsi gani chuo hicho kinaongozwa na genge la mafisadi.
Wahitimu wa mwaka 2011 walitakiwa kulipia ukodishaji wa josho shilingi 45,000/= za kitanzania kwa kila mhitimu, ahadi ilikuwa fedha shilingi 20,000/= zingerudishwa mara baada ya mhusika kurejesha joho (kwa wahitimu zaidi ya 5000). Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha siku ya urejeshaji wa majoho wahitimu walitakiwa kuandika akaunti namba kwa ahadi kuwa fedha hizo zitalipwa kupitia akaunti namba za wahusika baada ya wiki mbili. Cha ajabu mpaka leo fedha hizo hazijarejeshwa wala haifahamiki ni lini zitarejeshwa. Mwezi wa tatu mwishoni ilitolewa ahadi kuwa fedha hizo zingerejeshwa mwezi wa nne mwanzoni. Lakini hiyo ilikuwa ahadi ya kisiasa kama ilivyo kawaida ya chuo hicho kikuu cha kisiasa cha chama cha magamba.
Pia hata fedha za taadhari za wahitimu hao walizolipa wakati wakianza mwaka wa kwanza chuoni hapo zilitakiwa kurejeshwa pindi wanapohitimu lakini hilo halikufanyika.
Pia itakumbukwa jinsi gani fedha za mikopo zinavyocheleweshwa kulipwa kwa wanafunzi ambapo kuna wakati wanafunzi hukaa hata mwezi mmoja wakiwa bado hawajalipwa fedha zao za chakula na malazi. Hata sasa wasomi hawa wa udom wanalia njaa mno.
Lakini pia sote tunakumbuka jinsi wanataaluma chuoni hapo walivyogoma mwaka 2011 mwanzoni kutokana na mishahara yao kuwa inachakachuliwa na chuo kilikuwa kikianda salary slip zilizochakachuliwa tofauti na zile zilizokuwa zinatoka hazina.
Hivi mwisho wa haya yote ni nini?
Lakini kila lenye mwanzo lina mwisho wake pia
Wahitimu wa mwaka 2011 walitakiwa kulipia ukodishaji wa josho shilingi 45,000/= za kitanzania kwa kila mhitimu, ahadi ilikuwa fedha shilingi 20,000/= zingerudishwa mara baada ya mhusika kurejesha joho (kwa wahitimu zaidi ya 5000). Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha siku ya urejeshaji wa majoho wahitimu walitakiwa kuandika akaunti namba kwa ahadi kuwa fedha hizo zitalipwa kupitia akaunti namba za wahusika baada ya wiki mbili. Cha ajabu mpaka leo fedha hizo hazijarejeshwa wala haifahamiki ni lini zitarejeshwa. Mwezi wa tatu mwishoni ilitolewa ahadi kuwa fedha hizo zingerejeshwa mwezi wa nne mwanzoni. Lakini hiyo ilikuwa ahadi ya kisiasa kama ilivyo kawaida ya chuo hicho kikuu cha kisiasa cha chama cha magamba.
Pia hata fedha za taadhari za wahitimu hao walizolipa wakati wakianza mwaka wa kwanza chuoni hapo zilitakiwa kurejeshwa pindi wanapohitimu lakini hilo halikufanyika.
Pia itakumbukwa jinsi gani fedha za mikopo zinavyocheleweshwa kulipwa kwa wanafunzi ambapo kuna wakati wanafunzi hukaa hata mwezi mmoja wakiwa bado hawajalipwa fedha zao za chakula na malazi. Hata sasa wasomi hawa wa udom wanalia njaa mno.
Lakini pia sote tunakumbuka jinsi wanataaluma chuoni hapo walivyogoma mwaka 2011 mwanzoni kutokana na mishahara yao kuwa inachakachuliwa na chuo kilikuwa kikianda salary slip zilizochakachuliwa tofauti na zile zilizokuwa zinatoka hazina.
Hivi mwisho wa haya yote ni nini?
Lakini kila lenye mwanzo lina mwisho wake pia