Kwa tuhuma hizi za rushwa tatizo ni CCM au watanzania wenyewe?

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,274
Zimekua ni fikra za upinzani hasa CDM kwamba ili uwe mla rushwa au fisadi lazma uwe CCM wanasahau kwamba sisi sote ni wa tanzania.Halafu wapinzani wanajisahaulisha kwamba zaidi ya 80% ya wanachama wa vyama vyao wametoka CCM kutokana na ukweli kwamba huko nyuma vyama hivi hivikuepo.Sasa kubadili vyama hakuwezi kubadili tabia zao kwani watabaki kua walewale tu.
Kama watz hatuto badili tabia kwa m2 mmoja mmoja tutalipeleka taifa pabaya.
Sasa mtu kama ZZK anakua mtuhumiwa wa ulaji rushwa inaleta sura gani kwa watz?
Je CCM,CDM,TLP,NCCR ndio suluhisho la matatizo yetu au ni wa tz wenyewe?
 
Tatizo ni watanzania wenyewe. Hata CCM ikiondoka leo, rushwa itabiakia pale pale kwa kuwa tumekuwa wavivu wa kufikiri na kutaka maisha ya haraka bila jasho. Bila kubadilika sisi wenyewe, hata tukibadili utawala kila siku rushwa inabaki kwenye damu na fikra zetu.
 
Mtazamo wa wengi wanapoingia madarakani ni kuleta maendeleo ya kweli na ya haki lakini wanapokuta mfumo unanuka kwa kupendeleana na umeoza kwa rushwa nao hujikuta wameingia.Tatizo hapa ni watu na mfumo
 
Back
Top Bottom