MAJANI YA KUNDE
JF-Expert Member
- Aug 25, 2008
- 213
- 37
Jana usiku kulikuwa na kipindi TBC1 KIPINDI MAALUM.KUIJADILI HOTUBA YA KIKWETE Nilipokisikiliza sikuona mjadala juu ya Hotuba badala yake WAZIRI WASIRA alikitumia kipindi chote kuisema vibaya CHADEMA dhidi ya Maandamano kanda ya Ziwa,Kama baraza zima halina cha kuongea juu ya kuwasaidia Watanzania badala yake Rais,Waziri Mkuu na Mawaziri wote wameaua kupambana na Dr Slaa na Chadema basi wajue Maandamano yatakuwa zaidi ya hayo kwani Watanzania wanaotaabika watakuwa na mengi yanayowasumbua.Akipatikana mtu atakaetuzungumzia shida na Matatizo yetu tutamsikiliza tu hata kama ni chizi. Kikwete na Mawaziri wako fanyeni kazi muone kama tutawasumbua.