Ndugu Zangu,
MAGAZETI, Redio na Runinga zimeripoti, jana na leo; Freeman Mbowe amemtosa John Shibuda kwenye Baraza Kivuli la Mawaziri.
Tafsiri yangu, Mzee John Shibuda, Mbunge wa Maswa Magharibi kwa tiketi ya CHADEMA ( CCM?) hana wakati mzuri ndani ya CHADEMA. Kule ' kwao' kwa asili CCM alifanyiwa fitna. Jina lake likaenguliwa kwenye kura za maoni.
Na Mzee wa watu alikuwa juu kwenye kura za maoni. Lakin,i CCM tunawajua, wakafanya ' Vitu vyao!' Wakamnyima kivuli cha kisiasa. Shibuda, Msukuma anayewazidi Wasukuma wote kwa Kiswahili fasaha akaachwa na chama chake aungue juani!
Masikini Mzee Shibuda, kada mahiri asiyekana wala kuidharau asili yake kiitikadi, alichanganyikiwa. Akakata shauri kuvuka bahari. Akaenda Unguja kuomba ushauri kwa watani zake, Waswahili wa Unguja. Msukuma wa watu akarudi bara.
Breki ya kwanza ikawa Kinondoni, Makao Makuu ya CHADEMA- Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo. Na jana akaambiwa laivu- Hata CHADEMA hakuna kivuli!
Mwenyekiti Mbowe amem-freeze Shibuda. Inasemwa magazetini, kuwa Shibuda ameonekana kuwa na mitazamo tofauti dhidi ya chama chake cha sasa. ( Mwananchi, Februari 15, 2011)
Na ugomvi si ulianzia tangu Bagamoyo, au? Iliandikwa wakati ule, kuwa kulikuwa na kushikana mashati kati ya Kijana Ezekiel Wenje na Mzee John Shibuda. Kijana Wenje alimshutumu Mzee wake kwa uroho wa minofu! Ndio maana, wakati wenzake wamesusa, yeye akavaa shati lake jeupe na kwenda Ikulu ya Chamwino; kula nyama, kunywa na kucheza mduara kwenye sherehe ya Jakaya, Rais wa nchi.
Waandishi wakamfuata Shibuda kumwuliza kulikoni kushikana mashati na Wenje. Tukamsikia Mzee Shibuda akitamka; Nitakwenda kumshtaki Wenje kwa Wazee wa Mwanza!
Hata pale kuna tulioingiwa mashaka; hivi CHADEMA hakuna Wazee?
Na leo imeripotiwa, kuwa vijana wa CHADEMA vyuo vikuu mkoani Dodoma wamepanga leo waende ofisi za Bunge kumzuia Mzee Shibuda asiingie Bungeni, kisa? Msaliti!
Si Shibuda alitamka juma la jana pale Bungeni, kuwa vijana wa sasa wanahitaji mwongozo mzuri zaidi wa malezi na kwamba yeye atabaki na maadili aliyojifunza ndani ya CCM. Na hakuwa mchoyo, Mzee Shibuda akasema atayapeleka CHADEMA!
Hapo ndipo alipokosea mtani wangu, Msukuma wa watu Shibuda, Ya CCM kuyapeleka CHADEMA! Vijana wa CHADEMA wamemjia juu kama moshi wa kifuu. Wanasema; " Yeye anataka kuleta malezi aliyoyapata CCM alete CHADEMA, malezi ya CCM ayalete CHADEMA! Hapa hatutaki na sisi tutaandama Jumanne ( leo) kwenda kumzuia Shibuda asiingie Bungeni". Alitamka kijana Toju, Mwenyekiti wa tawi la Miyuji, Dodoma.
Wabunge Lema na Mdee walikuwapo . Lema akatamka, kuwa suala hilo liko ndani ya uwezo wa viongozi wa chama chao. Mdee akasema hakuna haja ya kumfutilia mbunge huyo ( Shibuda). Kama hukumu atahukumiwa na jamii husika. ( Mwananchi, Februari, 15, 2011).
Yote haya yanaacha maswali. Moja nalojiuliza, hivi kwanini vyama vyetu vya siasa vinapata tabu sana kumvumilia mwanachama mwenye fikra au mtazamo tofauti na wezake. Kwa nini muono tofauti uwe sawa na usaliti? Tumeyaona ndani ya CCM, na sasa CHADEMA.
Nini kifanyike kuimarisha Intra- Party Democracy ndani ya vyama vyetu hivi? Nimechokoza mjadala.
Maggid
Iringa,
Februari 15, 2011http://mjengwa.blogspot.com
MAGAZETI, Redio na Runinga zimeripoti, jana na leo; Freeman Mbowe amemtosa John Shibuda kwenye Baraza Kivuli la Mawaziri.
Tafsiri yangu, Mzee John Shibuda, Mbunge wa Maswa Magharibi kwa tiketi ya CHADEMA ( CCM?) hana wakati mzuri ndani ya CHADEMA. Kule ' kwao' kwa asili CCM alifanyiwa fitna. Jina lake likaenguliwa kwenye kura za maoni.
Na Mzee wa watu alikuwa juu kwenye kura za maoni. Lakin,i CCM tunawajua, wakafanya ' Vitu vyao!' Wakamnyima kivuli cha kisiasa. Shibuda, Msukuma anayewazidi Wasukuma wote kwa Kiswahili fasaha akaachwa na chama chake aungue juani!
Masikini Mzee Shibuda, kada mahiri asiyekana wala kuidharau asili yake kiitikadi, alichanganyikiwa. Akakata shauri kuvuka bahari. Akaenda Unguja kuomba ushauri kwa watani zake, Waswahili wa Unguja. Msukuma wa watu akarudi bara.
Breki ya kwanza ikawa Kinondoni, Makao Makuu ya CHADEMA- Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo. Na jana akaambiwa laivu- Hata CHADEMA hakuna kivuli!
Mwenyekiti Mbowe amem-freeze Shibuda. Inasemwa magazetini, kuwa Shibuda ameonekana kuwa na mitazamo tofauti dhidi ya chama chake cha sasa. ( Mwananchi, Februari 15, 2011)
Na ugomvi si ulianzia tangu Bagamoyo, au? Iliandikwa wakati ule, kuwa kulikuwa na kushikana mashati kati ya Kijana Ezekiel Wenje na Mzee John Shibuda. Kijana Wenje alimshutumu Mzee wake kwa uroho wa minofu! Ndio maana, wakati wenzake wamesusa, yeye akavaa shati lake jeupe na kwenda Ikulu ya Chamwino; kula nyama, kunywa na kucheza mduara kwenye sherehe ya Jakaya, Rais wa nchi.
Waandishi wakamfuata Shibuda kumwuliza kulikoni kushikana mashati na Wenje. Tukamsikia Mzee Shibuda akitamka; Nitakwenda kumshtaki Wenje kwa Wazee wa Mwanza!
Hata pale kuna tulioingiwa mashaka; hivi CHADEMA hakuna Wazee?
Na leo imeripotiwa, kuwa vijana wa CHADEMA vyuo vikuu mkoani Dodoma wamepanga leo waende ofisi za Bunge kumzuia Mzee Shibuda asiingie Bungeni, kisa? Msaliti!
Si Shibuda alitamka juma la jana pale Bungeni, kuwa vijana wa sasa wanahitaji mwongozo mzuri zaidi wa malezi na kwamba yeye atabaki na maadili aliyojifunza ndani ya CCM. Na hakuwa mchoyo, Mzee Shibuda akasema atayapeleka CHADEMA!
Hapo ndipo alipokosea mtani wangu, Msukuma wa watu Shibuda, Ya CCM kuyapeleka CHADEMA! Vijana wa CHADEMA wamemjia juu kama moshi wa kifuu. Wanasema; " Yeye anataka kuleta malezi aliyoyapata CCM alete CHADEMA, malezi ya CCM ayalete CHADEMA! Hapa hatutaki na sisi tutaandama Jumanne ( leo) kwenda kumzuia Shibuda asiingie Bungeni". Alitamka kijana Toju, Mwenyekiti wa tawi la Miyuji, Dodoma.
Wabunge Lema na Mdee walikuwapo . Lema akatamka, kuwa suala hilo liko ndani ya uwezo wa viongozi wa chama chao. Mdee akasema hakuna haja ya kumfutilia mbunge huyo ( Shibuda). Kama hukumu atahukumiwa na jamii husika. ( Mwananchi, Februari, 15, 2011).
Yote haya yanaacha maswali. Moja nalojiuliza, hivi kwanini vyama vyetu vya siasa vinapata tabu sana kumvumilia mwanachama mwenye fikra au mtazamo tofauti na wezake. Kwa nini muono tofauti uwe sawa na usaliti? Tumeyaona ndani ya CCM, na sasa CHADEMA.
Nini kifanyike kuimarisha Intra- Party Democracy ndani ya vyama vyetu hivi? Nimechokoza mjadala.
Maggid
Iringa,
Februari 15, 2011http://mjengwa.blogspot.com