Kwa salamu hizi maendeleo hakuna.

mayenga

JF-Expert Member
Sep 6, 2009
4,118
1,966
Musa:Mambo
Juma:poa
Musa:hamjambo
Juma:Sie wazima,za uko?
Musa:Huko kwema,ndugu na jamaa?
Juma:Ni wazima,sijui huko.
Musa:Huko Shwari kabisa,vipi shemeji na watoto?
Juma;Wazima kabisa.Kazi inakwendaje?
Musa:Kazi inakwenda vema.Shwari lakini?
Juma:Kwema Mungu anasaidia.Huko shwari?
Musa:shwari kabisa.Familia?
Juma:Familia haijambo.Vp maendeleo?

Aaaaagh!!
 
kiafrica zaidi...yule mbuzi wangu amekufa bwana Juma...alikula maganda ya mihogo...
Musa nae ataelezea yake...
heri mzungu mimi...nikikwambia Hi...shukuru na ujue nakufahamu sana...
 
Musa:Mambo
Juma:poa
Musa:hamjambo
Juma:Sie wazima,za uko?
Musa:Huko kwema,ndugu na jamaa?
Juma:Ni wazima,sijui huko.
Musa:Huko Shwari kabisa,vipi shemeji na watoto?
Juma;Wazima kabisa.Kazi inakwendaje?
Musa:Kazi inakwenda vema.Shwari lakini?
Juma:Kwema Mungu anasaidia.Huko shwari?
Musa:shwari kabisa.Familia?
Juma:Familia haijambo.Vp maendeleo?

Aaaaagh!!

Musa; eeh mambo mengine vp
Juma:swari, inakuwaje?
Musa:poa tu, niambie
Juma: poa, issue zinaendaje
Musa tunamshukuru mungu




yaan salamu ile ile mpaka daah inaboa
 
Hahahah hahahha hahah,
Nyie watu mmenichekesha aiseee!
Sijawahi kutana na salamu ya ivo lol!
 
swaga zinaendajeee:.........wajionaje...fresh...au vp...haina noma..
 
Back
Top Bottom