Wanajf mambo vp,nafikiri hakuna asiefaham kuwa watoto wa kambo huwa wananyanyasika sn au kunyanyaswa na mama wa kambo japo si wote lkn % kubwa ndio iko hivyo,tujadili hili!
Yatupasa tuelewe kuwa kuna aina 3 za umama na utoto wa kambo. 1. Ni ukambo wa kufikia. Mara nyingi mama wa kambo wa aina hii huwa si katili kwani hujiamini na hulea watoto aliowakuta kama wakwake.Ila tatizo huwa kwa watoto km watagundua kuwa huyo si mama mzazi. 2.Ukambo wa kuletewa (Watoto wa nje ya ndoa kuletwa ndan ya ndoa) Hapa kuna kazi kwelikweli,maana mama wa kambo hukosa kujiamini na huwa katili hata kama hakuwa na tabia hiyo kabla mtoto/watoto hawajaletwa, atajifunza mkuu! Kwa upande wa watoto huwa wasikivu hujiamini zaidi hufurahia busara ya baba kuwaleta ndani ya Familia. 3. Ukambo wa aina hii ni ule wa uyatima. (mama kafariki,Baba kaoa mke mwingine.) Mhh! hapa mama mara nyingi hupungukiwa busara na kukosa huruma na utu! huwa shurutisha watoto kwa kujua yeye ndo malkia! Na watoto hujibu mapigo kwa kuto mheshimu hata afanyaje.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.