Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,217
- 6,348
Ndugu zangu, naandika mada hii kwa huzuni na haibu kibao kutokana na kile nilichokiona Dar Es Salaam mwezi uliopita wakati nikiwa likizo. Huzuni na haibu niliyopata Dar ni juu ya madada zetu na urahisi wao. Dar kwa kweli inabidi mtu uwe mwangalifu sana la sivyo utakufa huku unajiona. Mademu wa Dar ni vicheche haijalishi yuko na mtu ama la...Mwanzoni hii tabia nilifikiri ipo kwa madada zetu walio nje kumbe hii tabia ni ya kurithi? Dar, unaweza kutoka kimahaba na mke wa mtu kwa muhogo tu wa kuchoma ama hata pakti mbili za karanga yaani ili mradi tu mtaani aonekane yuko na buzi. Najiuliza kwa nini mademu wa kibongo wako hivi? Nilikutana na demu fulani (mke wa mtu Dar) pale posta mpya, huyu dada nilimshangaa kweli maana alikuwa kila mara ananipigia simu na kunialika sehemu mpaka akanitongoza (yaliyojiri ni siri yangu). Dada ni mzuri na ana uwezo wake maana ana miliki gari la bei mbaya (bongo style) na nyumba yake ni safi sana, yaani full dozi utafikiri upo majuu humo ndani. Nilipomuuliza kama ana mtu kwanza akasita then akaniambia kuwa anaye lakini si hata yeye (mumewe) anapiga nje kwani shida iko wapi? Kweli nilishangaa. Nilipomwambia ndugu yangu akaniambia ndiyo mademu wa kibongo walivyo. Unaambiwa mademu wa kibongo si rahisi kukuta demu ana mtu mmoja, yaani wenyewe wanazidiana kete kwa kuwa na mabuzi wengi ili waweze kukidhi mahitajia yao na cha kushangaza ni kwamba wanatambiana nani ana vitu vya bei mbaya shinda mwenziwe, na ndiyo maana unakuta umalaya umezidi. Wiki yangu ya mwisho tukaenda Kunduchi Beach na shosti wake (anatarajia kuolewa mwezi wa 12, mwaka huu) kupunga upepo. Jamani yaliyojiri hapa ni balaa. Yule rafiki yangu akawa ameenda haja then nikabaki na yule shosti wake tunapiga stori tu za hapa na pale. Yule shosti akaniuliza kwa nini nilimpenda shosti wake wakati mimi naishi nje ya TZ, kwa kweli ikabidi nimdanganye maana sikumpenda shosti wake ila yeye ndiye aliyejigonga kwangu. Baada ya kuridhika na jibu langu akaniuliza, je akinipa nitakula bila kumuambia rafikiye? Yaliyojiri sisemi, ila najiuliza wanawake wa kibongo wamefikia hatua hii kweli? Kwa Nini?