Nijuavyo mimi nchi hii inaendeshwa kwa mujibu wa sheria. Je ni sababu zipi zinazoifanya serikali isiwafikishe watuhumiwa wa ufisadi mahakamani? kwani kwenye sheria kuna madaraja?
Mara kadhaa tumeshuhudia watuhumiwa wengi wakiachiwa huru na Polisi kwa kukosa ushahidi wa kuwapeleka mahakamani je hawa watuhumiwa ambao miaka inapita bila kuwafikisha mahakamani? je huku sio kwenda kinyume na haki za binadamu? kwanini wasitendewe haki?
Hizi taasisi zinazojigamba kuwa ni watetezi wa haki za binadamu hili hawalioni? mara kadhaa nimekuwa kinyume na wale wote wanaotuhumu wenzao bila kuwa na ushaidi wa kutosha, sina tatizo kabisa na mtu yeyote kama ushahidi utakuwepo, wasiwasi wangu ni kuwa kama utaratibu huu wa kuamini tetesi utakuwa unaaminiwa kuna baadhi ya watu ambao hawana hatia wakajikuta wanaadhibiwa kwa majungu, hisia au njama zinazosukwa na mahasimu wao.
Ningefurahi sana kama nitaelezwa sababu za watu ambao ni watuhumiwa wa ufisadi kutokufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake ikibidi kama kunafedha walizokwapua za watanzania waagizwe zirejeshwe kama wakina Maranda.
Mara kadhaa tumeshuhudia watuhumiwa wengi wakiachiwa huru na Polisi kwa kukosa ushahidi wa kuwapeleka mahakamani je hawa watuhumiwa ambao miaka inapita bila kuwafikisha mahakamani? je huku sio kwenda kinyume na haki za binadamu? kwanini wasitendewe haki?
Hizi taasisi zinazojigamba kuwa ni watetezi wa haki za binadamu hili hawalioni? mara kadhaa nimekuwa kinyume na wale wote wanaotuhumu wenzao bila kuwa na ushaidi wa kutosha, sina tatizo kabisa na mtu yeyote kama ushahidi utakuwepo, wasiwasi wangu ni kuwa kama utaratibu huu wa kuamini tetesi utakuwa unaaminiwa kuna baadhi ya watu ambao hawana hatia wakajikuta wanaadhibiwa kwa majungu, hisia au njama zinazosukwa na mahasimu wao.
Ningefurahi sana kama nitaelezwa sababu za watu ambao ni watuhumiwa wa ufisadi kutokufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake ikibidi kama kunafedha walizokwapua za watanzania waagizwe zirejeshwe kama wakina Maranda.