JAYJAY
JF-Expert Member
- Oct 31, 2008
- 7,502
- 7,530
ndugu wadau wa JF, nimejiuliza swali hili kutokana na taarifa nilizowahi kuzisikia zamani na taarifa ambazo ni za hivi karibuni. mwaka 2007 nadhani, kuna yule mzee wa Austria ambaye alihukumiwa jela maisha kwa kumbaka binti yake na kumzalisha watoto kadhaa, baadhi ya watoto walikuwa na aina fulani ya ulemavu na mmoja alifariki. jumapili ya desemba 4, 2011, kulikuwa na habari kwenye moja ya gazeti la kiswahili kuhusu mzee wa ujerumani ambaye naye anashitakiwa kwa makosa ya aina hiyo pia, baadhi ya watoto aliomzalisha binti yake wana matatizo ya ulemavu. naomba kuuliza wadau ni kwa nini hii hali inatokea sana kwa wazazi ndugu (baba na binti, kaka na dada,...) kuzaa watoto wenye ulemavu wa viungo au akili?