Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Nimekuwa nikijiuliza ni kwa nini wanawake husalitiwa zaidi na mashoga zao kwenye uhusiano kuliko ilivyo kwa wanaume? Naamini kila mmoja ni shahidi kwa kutendwa, kusikia au kuona wanawake walionyanganywa waume au wapenzi na mashoga zao. Je tatizo ni nini? Je ni tamaa za wanaume au wanawake hao walikuwa na kasoro ambazo zilikuwa hazirekebishiki na wanaume hao walikuwa wanasubiri tu atokee mwenye sifa wazitakazo waoe?