kwa nini unakosa ajira kwa watu kujiuliza tutakulipa nini?

jakisek

New Member
Dec 29, 2011
3
0
Napenda kuwasalimu wote mliopo kwenye jamiiforum kwani ni mara yangu ya kwanza kupost topic. Kuna jambo nisilolielewa labda mnaweza kunisaidia. Nimekuwa nikitafuta kazi kwa muda sasa japo nimejishikiza sehemu lakini bado sijatulia. Kinachonishangaza ni kwamba nimeenda kwenye interview kadhaa nafanya vizuri lakini mwisho wa siku unaambiwa "tukikuajiri tutakulipa nini?" Hapo hujaambiwa mshahara ni shilingi ngapi , hujaulizwa kama unakubaliana nao au la. Ninachojua unapaswa kuulizwa unataka shilingi ngapi halafu wao wanakwambia ngapi wanaweza kukulipa. Swala hili linanikwaza sana kwani sina elimu ya kutisha. Je ni njia tu ya kuninyima kazi? hebu nisaidieni wana jamii labda mimi ndio sielewi. Mwisho nawatakieni wote mwaka mpya mwema.
 
Napenda kuwasalimu wote mliopo kwenye jamiiforum kwani ni mara yangu ya kwanza kupost topic. Kuna jambo nisilolielewa labda mnaweza kunisaidia. Nimekuwa nikitafuta kazi kwa muda sasa japo nimejishikiza sehemu lakini bado sijatulia. Kinachonishangaza ni kwamba nimeenda kwenye interview kadhaa nafanya vizuri lakini mwisho wa siku unaambiwa "tukikuajiri tutakulipa nini?" Hapo hujaambiwa mshahara ni shilingi ngapi , hujaulizwa kama unakubaliana nao au la. Ninachojua unapaswa kuulizwa unataka shilingi ngapi halafu wao wanakwambia ngapi wanaweza kukulipa. Swala hili linanikwaza sana kwani sina elimu ya kutisha. Je ni njia tu ya kuninyima kazi? hebu nisaidieni wana jamii labda mimi ndio sielewi. Mwisho nawatakieni wote mwaka mpya mwema.
Kama hawana cha kukulipa kwa nini wakuite kwenye interview?
 
Napenda kuwasalimu wote mliopo kwenye jamiiforum kwani ni mara yangu ya kwanza kupost topic. Kuna jambo nisilolielewa labda mnaweza kunisaidia. Nimekuwa nikitafuta kazi kwa muda sasa japo nimejishikiza sehemu lakini bado sijatulia. Kinachonishangaza ni kwamba nimeenda kwenye interview kadhaa nafanya vizuri lakini mwisho wa siku unaambiwa "tukikuajiri tutakulipa nini?" Hapo hujaambiwa mshahara ni shilingi ngapi , hujaulizwa kama unakubaliana nao au la. Ninachojua unapaswa kuulizwa unataka shilingi ngapi halafu wao wanakwambia ngapi wanaweza kukulipa. Swala hili linanikwaza sana kwani sina elimu ya kutisha. Je ni njia tu ya kuninyima kazi? hebu nisaidieni wana jamii labda mimi ndio sielewi. Mwisho nawatakieni wote mwaka mpya mwema.

Hilo swali linaashiria ulitakiwa kuzunguka mbuyu..................aka kutoa mlungula!
 
Siku nyingine ukiulizwa swali hilo waambie nataka niwe nalipwa fedha halali kwa malipo na kazi halali nitakayopewa na kutimiza wajibu wangu.
 
Achana nao,tena wala isikuumize kichwa.Hao ni waajiri uchwara tu.Kwani ilikuwaje mpk wakakuita kwa interview?Just stay focused kuwa unatafuta kazi,ipo siku tu utakutana na mwajiri wa maana na sio hao wababaishaji wasiojielewa!Eeti tutakulipa nini?Kwani wao wanalipwa nini?wao pia si ni waajiriwa wa kampuni hiyo?
 
Back
Top Bottom