Kwa nini tusifanye maandamano ya amani jamani.

GAGL

JF-Expert Member
Aug 5, 2010
390
395
Napenda kutoa wito kwa watanzania wote hasa vijana na wanafunzi wa vyuo vikuu pamoja na wote wenye mapenzi mema na tz, tufanye maandamano ya amani kuhimiza juhudi za ziada zifanyike kumaliza tatizo la umeme. Jamani tumeambiwa Stiegler's Gorge inaweza kumaliza tatizo la umeme, mbona hatuoni juhudi za kuwezesha mradi huu uanze kazi. Ila kabla ya hapo ningeomba forum ya wanafunzi wa vyuo vikuu TAHLISO imwite waziri husika imuulize kuna mkakati upi wa kudumu kumaliza tatizo hili ila aseme kuhusu stiegler gorge, asipotoa maelezo ya kueleweka tufanye maandamano kuishinikiza serikali kuanza mradi huu. Ukosefu wa umeme wa uhakika ni janga la kitaifa.
 
Back
Top Bottom