Kwa nini tunaimba ubeti mmoja wa wimbo wetu wa Taifa ?

Sinkala

JF-Expert Member
Dec 22, 2008
1,773
683
Nimekuwa nikipata mkanganyiko kuhusu matukio ambayo yanastahili kuimbiwa ubeti mmoja na yale yanayostahili beti zote mbili za wimbo wa Taifa wa Tanzania. Utakuta wakati wa tukio fulani linaimbwa beti moja (Mungu ibariki Tanzania) na wakati mwingine zinaimbwa zote (Mungu ibariki Afrika kwanza halafu Mungu ibariki Tanzania mwisho).
Afadhali hata ukiimbwa kwa instrumental, si rahisi kujua unaoimbwa ni upi. Hali inakuwa mbaya iwapo wimbo utaimbwa kwa vocal, kwani hapa kila mtu ataanza kivyake, mwingine Afrika na mwingine Tanzania, huyu atasema Wabariki viongozi wake, na yule atasema Dumisha Uhuru na Umoja.
Sasa waungwana, naombeni mnifafanulie matukio yapi yanastahili beti ngapi, maana ni aibu kuimba mbele ya wageni kutoka nje, huku wakishuhudia jinsi ambavyo hatujui wimbo wetu !!
 
Wimbo wetu wa Taifa.
Huu wimbo ulitungwa tulipopata Uhuru 1961, na kwa vile wakati huo nchi nyingi Afrika zilikuwa bado chini ya wakoloni, viongozi walisisitiza uhuru na upendo wa Afrika nzima kwanza. Itakumbukwa hata Hayati Julius Nyerere aliweza kutamka kwamba 'Uhuru kwa Tanganyika bila kuwa na Uhuru kwa Afrika nzima haukuwa na maana' (au maneno karibu na hayo). Kwa hiyo ubeti wa kwanza wa wimbo wa taifa ulihusu Afrika; na wa pili ulihusu Tanganyika.
Maoni yangu ni kwamba Wimbo wa Taifa ni mrefu sana, hasa pale inapokuwa ni lazima wimbo wa taifa lingine ufuate au utangulie; kwa mfano wakati wa kumkaribisha Mkuu wa nchi nyingine anayezuru Tanzania. Kwa hiyo ingefaa Ubeti wa Pili unaohusu Tanzania tu uimbwe. Ikiwa ni instrumental, basi haitatambulika kama tunaombea Tanzania na tumeacha kuombea Afrika.

Kilasara (Junior Member)
 
Nimekuwa nikipata mkanganyiko kuhusu matukio ambayo yanastahili kuimbiwa ubeti mmoja na yale yanayostahili beti zote mbili za wimbo wa Taifa wa Tanzania. Utakuta wakati wa tukio fulani linaimbwa beti moja (Mungu ibariki Tanzania) na wakati mwingine zinaimbwa zote (Mungu ibariki Afrika kwanza halafu Mungu ibariki Tanzania mwisho).
Afadhali hata ukiimbwa kwa instrumental, si rahisi kujua unaoimbwa ni upi. Hali inakuwa mbaya iwapo wimbo utaimbwa kwa vocal, kwani hapa kila mtu ataanza kivyake, mwingine Afrika na mwingine Tanzania, huyu atasema Wabariki viongozi wake, na yule atasema Dumisha Uhuru na Umoja.
Sasa waungwana, naombeni mnifafanulie matukio yapi yanastahili beti ngapi, maana ni aibu kuimba mbele ya wageni kutoka nje, huku wakishuhudia jinsi ambavyo hatujui wimbo wetu !!

Mimi sijui kama kuna matukio ya kuimbiwa beti moja na mengine beti zote mbili.Ndiyo kwanza nasikia leo.Najua tu kwamba wimbo wa taifa unapoimbwa lazima ukamilishwe kwa beti zote mbili huku waimbaji wakisimama kikakamavu bila kutikisika hata nzi akikunusa nusa na mtu anayepita njia karibu ya hapo lazima nae 'afe ganzi'.Ndiyo tulivyofundishwa kwenye primary yetu!
 
Mimi sijui kama kuna matukio ya kuimbiwa beti moja na mengine beti zote mbili.Ndiyo kwanza nasikia leo.Najua tu kwamba wimbo wa taifa unapoimbwa lazima ukamilishwe kwa beti zote mbili huku waimbaji wakisimama kikakamavu bila kutikisika hata nzi akikunusa nusa na mtu anayepita njia karibu ya hapo lazima nae 'afe ganzi'.Ndiyo tulivyofundishwa kwenye primary yetu!

Ukihudhuria mechi siku ambayo timu ya taifa inacheza, utagundua kwamba ni kweli huwa unaimbwa ubeti mmoja tu. Hata mimi sielewi huwa ni kwa nini inakuwa hivyo!
 
Mbona mimi sioni tatizo hapo mkuu?Huo siyo wimbo wa taifa ni wimbo mwingine tu wa kuwajengea vijana uzalendo,au?

Mkuu imenikumbusha sana enzi hizooo, nchi ni nchi kweli...viongozi walikuwa patriotic kweli, sio hivi sasa wakipata nafasi ya kunyofoa wanatengeneza na makazi kabisa.
 
Wimbo wetu wa Taifa.
Huu wimbo ulitungwa tulipopata Uhuru 1961, na kwa vile wakati huo nchi nyingi Afrika zilikuwa bado chini ya wakoloni, viongozi walisisitiza uhuru na upendo wa Afrika nzima kwanza. Itakumbukwa hata Hayati Julius Nyerere aliweza kutamka kwamba 'Uhuru kwa Tanganyika bila kuwa na Uhuru kwa Afrika nzima haukuwa na maana' (au maneno karibu na hayo). Kwa hiyo ubeti wa kwanza wa wimbo wa taifa ulihusu Afrika; na wa pili ulihusu Tanganyika.
Maoni yangu ni kwamba Wimbo wa Taifa ni mrefu sana, hasa pale inapokuwa ni lazima wimbo wa taifa lingine ufuate au utangulie; kwa mfano wakati wa kumkaribisha Mkuu wa nchi nyingine anayezuru Tanzania. Kwa hiyo ingefaa Ubeti wa Pili unaohusu Tanzania tu uimbwe. Ikiwa ni instrumental, basi haitatambulika kama tunaombea Tanzania na tumeacha kuombea Afrika.

Kilasara (Junior Member)
Wimbo wa Taifa ni mrefu ukilinganisha na wimbo upi?
Si kweli. Natioanal Anthem inatakiwa kuimbwa yote.Kwa faida ya wengine HII NI SALA YA TAIFA.
Nchi hii ya ajabu sana.SIJUI...MH
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom