Kwa nini sikugombea uongozi 2010...

Ramos

JF-Expert Member
May 13, 2010
498
130
Ndugu wanaJF, lengo la thread hii ni kuonyesha kuwa pamoja na kuwa wengi wetu tunaunga mkono mabadiliko, tena wengi ni watu wenye uzalendo 'kiasi' na kuipenda nchi yetu, bado kuna mambo yanayofanya uwanja wa kudai haki zetu usiwe flat.

Nimejiuliza pamoja na kuwa ukiongea na wasomi wengi wanakuwa wana-support vyama vya upinzani, lakini ukiangalia mwaka huu ari ya kujitokeza kupitia vyama hivyo kugombea ni ndogo ukilingasha na wanaojitokeza kwenye CCM...

Nimejaribu kuwaza sababu mbalimbali zinazotufanya 'tuogope' kugombea na vyama vya upinzani, lakini kabla sijamwambia mtu yeyote, nikagundua hata hapa JF waliojitangaza kugombea uongozi ni wachache, wakati naamini hapa kuna vichwa vizuri tu vya kuongoza.

Hivi kama unadhani kuwa unaweza kuwa kiongozi wa kisiasa, lakini hujagombea, unafikiri nini kimekuzuia kufanya hivyo, na nini iwe suluhisho lake?
 
Ndugu wanaJF, lengo la thread hii ni kuonyesha kuwa pamoja na kuwa wengi wetu tunaunga mkono mabadiliko, tena wengi ni watu wenye uzalendo 'kiasi' na kuipenda nchi yetu, bado kuna mambo yanayofanya uwanja wa kudai haki zetu usiwe flat.

Nimejiuliza pamoja na kuwa ukiongea na wasomi wengi wanakuwa wana-support vyama vya upinzani, lakini ukiangalia mwaka huu ari ya kujitokeza kupitia vyama hivyo kugombea ni ndogo ukilingasha na wanaojitokeza kwenye CCM...

Nimejaribu kuwaza sababu mbalimbali zinazotufanya 'tuogope' kugombea na vyama vya upinzani, lakini kabla sijamwambia mtu yeyote, nikagundua hata hapa JF waliojitangaza kugombea uongozi ni wachache, wakati naamini hapa kuna vichwa vizuri tu vya kuongoza.

Hivi kama unadhani kuwa unaweza kuwa kiongozi wa kisiasa, lakini hujagombea, unafikiri nini kimekuzuia kufanya hivyo, na nini iwe suluhisho lake?
niko ughaibuni kwa hiyo siwezi kutelekeza majukumu ya Ubunge au udiwani nikiwa sipo huko ndo maana nawaunga mkono wagombeaji huko
 
Sikugombea kwa sababu ninafundisha watoto wadogo shuleni. Iwapo sote tutakuwa wanasiasa, ni nani atafundisha watoto wetu maadili ili waje kuwa viongozi wazuri baadaye? Najua kuna waalimu wenzangu wengi wamekimbilia siasa kwa kufuata masilahi, lakini naamini kuwa maslahi ya wanasiasa yatokanayo na kuwadhulumu wananchi ni laana mbaya sana, heri nibaki na faraja yangu itokanayo na kujua kuwa ninatenda mema
 
Back
Top Bottom