Kwa nini Rais analazimisha kitu ambacho hana madaraka nacho ya Kikatiba? (Video)

Nisemeje.

Kikwete hataki kubadilisha katiba ila anataka kuonekana kuwa anataka kuibadilisha baada ya kujulikana kuwa katiba iliyopo ni mbovu na ubovu huo ndio unaomfanya abaki madarakani hadi leo ingawa watu wenye akili wanajua kuwa alirudi madarakani kwa njia dubious zikichangiwa na ubovu wa katiba ya sasa.

Iwapo anakiri kuwa katiba ya sasa ina mapungufu yanayotakiwa kurekebishwa, asingeweza kuitumia hiyo kama kinga yake ya kumpa madaraka ya kutunga katiba nyingine; alitakiwa atoe milango wazi ya kuwa na utaratibu wa kutunga katiba huru. Huwezi kujenga nyumba imara kwa kutumia msingi mbovu. Vitisho vya kufunga watu wanaohoji katiba hiyo ni vya kijinga sana na vinatokana na akili mbovu ya Werema kwa vile ana upungufu mkubwa sana wa kuona mambo kwa kina, ndiyo maana nimegundua kuwa hukumu nyingi alizotoa akiwa jaji zimekuwa na utata. Vitisho hivi vinaweza vikaaiharibu kabisa nchi hii iwapo watu wa busara hawataingilia kati kulikokoa taifa hili lenye raslimali nyingi za asili na kukosa raslimali za binadamu wa kuiongoza
 
Huwezi kutaja ACT itokanayo na sheria inayotafuta KULITUMIKISHA KATIBA YETU YA SASA iendane nayo badala ya bunge kukidhi msingi mama wa kufanya sheria zote za nchi KUITUMIKIA sheria mama ambayo ni katiba ya nchi.

Indeed, yours is a miserably confused shot here!!
Hii ndiyo problem right here!.... Bunge likipitisha mswaada, unakuwa sheria.... labda uniambie bunge limevunja kifungu kipi cha katiba kwa kutunga shreia hii ya kuunda tume.
An act becomes law when signed by the president.
 
Act No.15 0f 1984. Section 12
Labda uanze na Article 62 (1) and (3).
Oanisha na article 64(1).
Halafu jaribu kuoanisha na article 63(1) na (3)(d).

Vipengele vyote hivyo havihusiani na uandikaji wa Katiba Mpya. Vinahusiana na utaratibu wa kutunga sheria - utaratibu ambao unaweza kutumika kufanyia mabadiliko katiba iliyopo sasa.
 
Bunge la CCM bila aibu tena kwa ushabiki mkubwa kichama sheria batili ya Makinda inayojitia bingwa kupingana na katiba yetu:

1. Kwa kujiandaa kufunga Wa-Tanzania jela miaka mitatu eti kwa kupinga KATIBA YA KIKWETE na kwamba wala tusiwaze kutumia mamlaka yetu wenyewe kujadili, kupinga na kuunda katiba ya wananchi wenyewe? (The Doctrine of Ultraires)

2. Sheria inayotafuta kutugawa kimatabaka kwa maana kwamba KATIBA YA KIKWETE itapata kuundwa na hata kukosolewa tu na matajiri peke yao nchini ambao ndio wenye uwezo wa kukwepa kwenda jela Ukonga kwa kulipa faini ya milioni moja. (Malice)

3. Sheria iliotungwa sirini kwa maswahiba wachache kualikana wenyewe kwenye mijengo ya kifahari sehemu za mijini tu (Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar) KWA MWALIKO MAALUM ilhali wenye nchi kwa asilimia zetu zaidi ya 80 vijijini tukifungiwa milango nje. (Selective)

...
 
Kuna dalili hapa hawa CCM wanataka kufanya mchezo mchafu kwenye hiyo katiba ndio maana mkuu wa kaya kaamua kuingilia kati, so guys tusilale mlango wazi tule nao sambamba madam tunajuwa sheria zinasemaje, hawa watu wasitufanye sisi mambumbumbu ambao bado tunapelekeshwa kama watu tusiojuwa nini tunafanya, wanataka kujitungia katiba then ionekane kama wamefanya changes, so lazima tujue na kama kuna mahali hapaeleweki then tuende next step tujue nini cha kufanya na sio kuwachekea tu hawa watu wasiokuwa na maana kwa nchi yetu,
 
Any piece of legislation, whether expressly and or under disguise, that seeks to insubodinate the mother-law hereby referred to as the national CONSTITUTION of the United Republi of Tanzania, does NOT and shall never come a full-moon as an effective instrument of administration of 'JUSTICE' to anyone in our land even it were to be SIGNED into a Commandment by God leave alone President Kikwete if never spring from the masses, identify with it and borrow from it a sense of ownership.

Hii ndiyo problem right here!.... Bunge likipitisha mswaada, unakuwa sheria.... labda uniambie bunge limevunja kifungu kipi cha katiba kwa kutunga shreia hii ya kuunda tume.
An act becomes law when signed by the president.
 
Mh. Mwanakijiji,
Una hoja yenye mashiko na ushawishi hapa. Two wrongs makes one right, NO? Kikwete na ccm wanasema ndiyo!
Usanii kila mahali, ni kweli marekebisho yalipaswa kufanyika ktk katiba ya sasa ili kuandaa hayo mazingira pamoja na uhalali (legal legitimacy) ya mazingira/mchakato.


Kikwete ni mnafiki sana. Hana nia (hata kidogo) wala uwezo (kiakili au kisheria) wa kuandaa mazingira ya Katiba Mpya Tz licha ya Katiba yenyewe. Kwa bahati mbaya (kwake) pia sio msikivu na mweledi. Kwa vile amejitabanaisha tena kuwa yeye ni rais legelege, mnafiki na bunge la ccm kumpa shavu; sisi wananchi tutawaonesha upande wa pili wa sarafu ambao hawataki kuuona wala kuusikia.
 
Vipengele vyote hivyo havihusiani na uandikaji wa Katiba Mpya. Vinahusiana na utaratibu wa kutunga sheria - utaratibu ambao unaweza kutumika kufanyia mabadiliko katiba iliyopo sasa.
Huwezi kuandika katiba mpya, bila kutunga sheria ya kuandika katiba mpya.
 
Kikwete ana tabia ya kutoa vitisho anapotaka kufanikisha jambo,kumbukeni hotuba ya kusapress tucta na mgaya,....
 
Any piece of legislation, whether expressly and or under disguise, that seeks to insubodinate the mother-law hereby referred to as the national CONSTITUTION of the United Republi of Tanzania, does NOT and shall never come a full-moon as an effective instrument of administration of 'JUSTICE' to anyone in our land even it were to be SIGNED into a Commandment by God leave alone President Kikwete if never spring from the masses, identify with it and borrow from it a sense of ownership.
You are entintled to your own opinion, but YOU ARE NOT! entitled to your own facts.
Halafu mbona una hasira?..... calm down, grab a cold one and lets talk politics.
 
nimemnukuu tu yeye kuwa anadai kuwa anayo mamlaka hayo na katiba na pia ametoa mfano wa tume mbalimbali huko nyuma za kushugulikia maswala ya katiba mwaka 1963 na mwaka 1983 ambazo ni Rais ndio aliziunda utaratibu ambao binafasi sikubaliani nao kwani kwa kuwa ulitumika mwaka 1983 na 1963 basi unafaa kwa watu wa 2011 that is wrong. kwahiyo kama hakuna kipengele chochote basi ndio itatupa hoja nzuri ya kuingia barabarani hiyo jumapili.

wewe unaakili fupi sana acha ubishi kama hujui nyamaza. Sasa hapa alikuwa ananukuu vipengele vya katiba au alikuwa anadesa kutoka kwa wezake waliopita. Hapo anaiga wezake na sis tunataka mawazo mapya coz ni watu wa zama tofauti. Tunataka mabadiliko. Ndugu mwanakijiji yuko sahihi, katiba ya sasa inaruhusu kuifanyia marekebisho na si kuandika mpya. Jk ni kilaza hafikirii na wala hata haijui katiba anoisimamia.
 
wewe unaakili fupi sana acha ubishi kama hujui nyamaza. Sasa hapa alikuwa ananukuu vipengele vya katiba au alikuwa anadesa kutoka kwa wezake waliopita. Hapo anaiga wezake na sis tunataka mawazo mapya coz ni watu wa zama tofauti. Tunataka mabadiliko. Ndugu mwanakijiji yuko sahihi, katiba ya sasa inaruhusu kuifanyia marekebisho na si kuandika mpya. Jk ni kilaza hafikirii na wala hata haijui katiba anoisimamia.
Katiba iliyopo inamruhusu rais kutunga sheria. Na huwezi kupata katiba mpya bila kutunga sheria ya kuandika katiba mpya.... kwa hiyo ni rais na bunge ndio wanaohusika na kutunga sheria ya kutafuta katiba mpya, na si mtu mwingine yeyote yule. Ila kuna njia mbadala, nayo ni kufanya mapinduzi au kusubiri 2015 na kuing'oa serikali na bunge lililopo.
Au kumuomba mkuu Sarkozy na Obama wawape tafu ya mabomu ili tupate serikali mpya, katiba mpya na uchaguzi mpya.
Zaidi ya hapo, ni kutumia bunge,wahisani au wananchi mitaani wamshinikize rais au bunge liandike sheria tofauti.
 
WAKATI CCM WAJIKIMBIZA KICHOYO NA AJENDA YAO KUREKEBISHA SHERIA, WANANCHI TWENDE MBELE ZAIDI KUANZISHA MCHAKATO WA KWELI KUPATIKANA KATIBA YA WANANCHI TANGU SASA BILA VURUGU

Kamwe huwezi kutumia a MERE ACT OF PARLIAMENT kuanzisha mchakato wa kuundwa upwa kwa katiba ya nchi isipokua ni kwa njia pekee ya kuibadilisha kifungu, kuongezea na au kuboresha kifungu kimojawapo ndani ya katiba ya sasa ndipo upate kuunda upya katiba mpya.

Hadi hivi sasa kile kilichopitishwa na CCM Dodoma aka 'Muswada wa Makinda' nis an infutility right from its inception; HAKUNA KITU PALE, BURE KABISA!!! Hivyo basi tukumbuke kwamba mpaka hapo ni dhahiri kwamba wao CCM huenda wamekusudia kubadilisha vijisheria fulani fulani hivi ndio maana wameamua kutumia hicho chombo kiitwacho 'AN ACT OF PARLIAMENT'.

Kwa msingi huo, basi ni dhahiri kwamba agenda ya CCM kuhusu mabadiliko yanapishana njia panda na yale ya umma ambao baadhi yao wanaonekana kutubeza. Wakati lao ni kubadilisha vijisheria, letu ni kubadilisha KATIBA YETU YA TAIFA.

Ndio, nasema wakati letu moyoni kutfuta njiaa bora zaidi kutetea maslahi ya HAKI NA UTU WA MTANZANIA, wao lao ni kutafuta kutetea haki na maslahi ya chama cha kisiasa.

Na ndio maana si rahisi watu tukaelewana lugha hapa; wananchi wenzangu tutumie madaraka yetu ya kikatiba, bila kukasimu kwa mtu au kundi lolote, kwa kujisainisha sahihi zaidi ya milioni 1 ili tupate legitimacy wa kujianzishia wenyewe mchakato wa KATIBA MPYA na tuondokane kabisa na hawa wenzetu chini ya idadi ya Watanzania 200 waliojikusanya Dodoma kutekeleza wajibu wao wa utunzi wa sheria tu na wala si kuunda upya katiba.

Mh. Mwanakijiji,
Una hoja yenye mashiko na ushawishi hapa.

Two wrongs makes one right, NO? Kikwete na ccm wanasema ndiyo!
Usanii kila mahali, ni kweli marekebisho yalipaswa kufanyika ktk katiba ya sasa ili kuandaa hayo mazingira pamoja na uhalali (legal legitimacy) ya mazingira/mchakato.


Kikwete ni mnafiki sana. Hana nia (hata kidogo) wala uwezo (kiakili au kisheria) wa kuandaa mazingira ya Katiba Mpya Tz licha ya Katiba yenyewe. Kwa bahati mbaya (kwake) pia sio msikivu na mweledi. Kwa vile amejitabanaisha tena kuwa yeye ni rais legelege, mnafiki na bunge la ccm kumpa shavu; sisi wananchi tutawaonesha upande wa pili wa sarafu ambao hawataki kuuona wala kuusikia.
 







Kwa haraka inawezekana kudhaniwa kuwa Rais Kikwete ameweza kutetea kwanini yeye ndiye aanzishe na kusimamia mchakato wa Katiba Mpya. Kwamba alitumia madaraka yale yale ambayo yalitumiwa na viongozi wengine wa nyuma- japo mara zote hizo haikuwa kuhusu Katiba Mpya bali kubadilisha katiba iliyokuwepo na kuiboresha na pale ambapo kulikuwa na kwenda kwenye Katiba ya kudumu kulifanyika katika mazingira ya chama kimoja na hivyo kuondoa hoja ya ushiriki wa vyama vingine na hata kuhoji. Rais ndiye alikuwa mkuu wa chama hicho kimoja na ndiye mkuu wa serikali na hivyo inaeleweka kwanini ilikuwa hivyo. Hili halihalalishi hali iyo kurudiwa sasa katika uelewa wetu wa demokrasia ya vyama vingi na ukuu wa wananchi (siyo chama kama ilivyokuwa zamani).

Hatujawahi kuwepo hapa tulipo sasa. Njia hizo za zamani zilizotumika ndizo zilipotufikisha hapa na tunahitaji ubunifu wa hali ya juu. Kurudia mambo yale yale kwa namna ile ile kuna jina lake lakini kwa vile tunaishi katika zama mpya tungetarajia ubunifu zaidi.

Katiba ya sasa haimpi Rais kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya ana uwezo akitaka wa kusimamia kwa kupitia chama chake mchakato wa kufanya mabadiliko ya katiba ya sasa. Lakini kwa vile anachotaka ni katiba Mpya napendekeza kuwa Katiba ya sasa haina madaraka hayo kwa Rais au kwa mtu mwingine yeyote na kiukali kabisa tunaweza kugeuza na kudai zoezi zima haliwezi kufanya na wale walioapa kulinda Katiba ya sasa! Hakuna kipengele chochote kinachohusiana na kuandika katiba mpya katika Katiba yetu ya sasa. Sasa kama hakuna imekuwaje Rais aamini kuwa ana madaraka ya kuanzisha hata kuitisha Bunge la Katiba?

Kujibu swali lake la mwisho ni kuwa:

a. Kabla ya kuundwa kwa tume hiyo ya kukusanya maoni ilitakiwa kwanza yafanyike mabadiliko katika Katiba ya sasa ambayo yangeweza utaratibu wa kuandika Upya Katiba ya nchi. Katiba ya sasa inaruhusu kufanyiwa mabadiliko tu (ammendments) lakini hairuhusu kuwepo kwa mchakato wa kuandika Katiba Mpya.

b. Mabadiliko hayo ya Katiba ya kuweka mchakato ndio yangejadili nani na kwa vipi teuzi za tume ya kuandika Katiba unatakiwa kufanyika. Haiwezekani Rais aliyeko madarakani anajiamulia tu kuandika Katiba Upya yeye mwenyewe halafu wengine wafuate; Tukumbuke tamko la kuandika Katiba Mpya lilitolewa kwenye salamu za mwaka mpya! Halikutolewa Bungeni na wala hakukuwa na utaratibu wa kuonesha kuwa umejali wananchi. Ulikuwa ni uamuzi binafsi wa Kikwete. Tukumbuke kuwa kwenye hotuba ile hakusema "amedhamiria" la hasha alisema "ameamua".

c. Ni kutoka hapo sasa ndio sheria ya kusimamia mchakato wa kuelekea Katiba Mpya ungeweka. Ina maana ya kwamba suala la Kuandika Katiba Mpya lingewekwa ndani ya Katiba ya sasa na kuangaliwa kama tunavyoangalia yale mambo 8 ambayo yanahitaji ridhaa ya pande mbili za Muungano (theluthi mbili ya wajumbe). Lakini kwa hivi ilivyo Kikwete na Shein wataamua wao wenyewe. Sasa hiyo sheria ndio ingezingatia maoni ya watu wengine.

Utaona basi kuwa kosa la kwanza limefanyika kwa kutozingatia Katiba ya sasa kwanza - haina mchakato wa kuandika Katiba Mpya - na hivyo kufanya hoja ya Katiba Mpya haiwezi kutolewa na wale walioapa kuilinda ya sasa na kama inatolewa walitakiwa kwanza kufanyia mabadiliko hii Katiba ili wajipe uwezo wa kuzungumzia "katiba mpya".

Kwa vile suala la Katiba Mpya basi ni la nje ya watawala wetu wa sasa ni wazi kuwa toka mwanzo ushiriki wao ulitakiwa uwepo na siyo mtindo huu wa kuburuzana na kuwapa wananchi taarifa zisizo za kweli kwa ajili ya faida za kisiasa (political expediency). Badala ya kusahihisha makosa wameamua kuendelea katika kukosea. Wananchi wafanye nini?

a. Watahamasishana wasishiriki kwenye hiyo tume na kuwaachia wana CCM wakaambizane wanayotaka kuyasikia. Yaani A total boycott of the exercise. Hakuna namna ya kuwalazimisha wananchi washiriki. Na kama tulivyoona leo hata wana CCM wenyewe hawako katika hali ya kuruka ruka sana na kufurahia mchakato wenyewe.

b. Watasubiri ije siku ya kupiga kura ya maoni watahamasishana kwenda kuungusha kwenye sanduku la kura kuwaonesha watawala kuwa wananchi ndio wako supreme zaidi ya Rais na Bunge. Kwa vile wamekubali kuweka kiwango cha chini ya asilimia 50 kupitisha ni kiwango kidogo sana kukifikia! kwani upinzani unahitaji kuhamasisha asilimia 51 tu!

Sioni dalili yoyote ya watawala kukaa pamoja na kama tuliyoyashuhudia wiki hii ni mfano basi Kikwete hayuko tayari hata kukubali hoja za upande wa pili - ila upande wake ndio anataka ukubaliwe bila kuhojiwa au kupingwa. Na uamuzi wa kuweka adhabu kwa watu watakopinga mchakato huu umethibitisha pasipo shaka kuwa kwa njia ya kawaida haiwezekni kushinda isipokuwa kwa shurti, vitisho na vifungo.


Utabiri wangu: Mswada huu utarudishwa mapema tena Bungeni ili ufanyiwe marekebisho kama walivyofanya kwenye msaada ya gharama za uchaguzi ambao wengine tuliupinga na kuonesha makosa mapema wakang'ang'ania na kusaini kwa mbwembwe lakini miezi mitatu tu baadaye wakaurudisha na bado wanahitaji kuufanyia marekebisho. Mswada huu ukiwa sheria hautekelezeki, haukubaliki, na watawalazimisha watu kuupuza. Tunaposema katiba ni 'mama' hatusemi tu hivi hivi. Sasa mama habambikiziwi! Vingenevyo wapo Watanzania ambao wataiona katiba ijayo kuwa ni 'katiba ya kambo'! Hawataipenda, hawataizingatia na watajaribu kweli kweli kuibadilisha. Kama Rais wa sasa ameweza kufanya hivi bila kuulizwa na mtu guess what akija Rais mwingine?

Hadi wakubali kusikiliza upande wa pili na kufuata ile kanuni ya kwanza - KATIBA LAZIMA ITOKE KWA WANANCHI WENYEWE. Kuanzia mfumo wa kuwashirikisha wananchi, nani anasimamia na inafikiwa vipi ni lazima iwe inasimama kwenye madaraka ya wananchi kutawala.


Mwana kijiji wewe wajulikana ni cdm kufa , haya mawazo yako sinto shangaa kuyasikia. Kelele za chura...............

 
Last edited by a moderator:
WAKATI CCM WAJIKIMBIZA KICHOYO NA AJENDA YAO KUREKEBISHA SHERIA, WANANCHI TWENDE MBELE ZAIDI KUANZISHA MCHAKATO WA KWELI KUPATIKANA KATIBA YA WANANCHI TANGU SASA BILA VURUGU

Kamwe huwezi kutumia a MERE ACT OF PARLIAMENT kuanzisha mchakato wa kuundwa upwa kwa katiba ya nchi isipokua ni kwa njia pekee ya kuibadilisha kifungu, kuongezea na au kuboresha kifungu kimojawapo ndani ya katiba ya sasa ndipo upate kuunda upya katiba mpya.

Hadi hivi sasa kile kilichopitishwa na CCM Dodoma aka 'Muswada wa Makinda' nis an infutility right from its inception; HAKUNA KITU PALE, BURE KABISA!!! Hivyo basi tukumbuke kwamba mpaka hapo ni dhahiri kwamba wao CCM huenda wamekusudia kubadilisha vijisheria fulani fulani hivi ndio maana wameamua kutumia hicho chombo kiitwacho 'AN ACT OF PARLIAMENT'.

Kwa msingi huo, basi ni dhahiri kwamba agenda ya CCM kuhusu mabadiliko yanapishana njia panda na yale ya umma ambao baadhi yao wanaonekana kutubeza. Wakati lao ni kubadilisha vijisheria, letu ni kubadilisha KATIBA YETU YA TAIFA.

Ndio, nasema wakati letu moyoni kutfuta njiaa bora zaidi kutetea maslahi ya HAKI NA UTU WA MTANZANIA, wao lao ni kutafuta kutetea haki na maslahi ya chama cha kisiasa.

Na ndio maana si rahisi watu tukaelewana lugha hapa; wananchi wenzangu tutumie madaraka yetu ya kikatiba, bila kukasimu kwa mtu au kundi lolote, kwa kujisainisha sahihi zaidi ya milioni 1 ili tupate legitimacy wa kujianzishia wenyewe mchakato wa KATIBA MPYA na tuondokane kabisa na hawa wenzetu chini ya idadi ya Watanzania 200 waliojikusanya Dodoma kutekeleza wajibu wao wa utunzi wa sheria tu na wala si kuunda upya katiba.


Utaanzishaje na ww huna madaraka ! labda ndani ya familia yako poa, ila kwa watanzania BIG NO

 
sababu ya kuzuia wananchi tusijadili muungano ni ipi?
Amesema kwa sababu ni "tunu ya Taifa."

Sababu za Muungano za kijinga jingaaa! Tunu ya Taifa ni madini yanayochimbwa na Barrick bure na twiga wanaotoroshwa na ndege.

Ndio maana hii naiita ni TUME YA RAIS YA KUCHAGUA MAONI YA WANANCHI NA KUANDIKA RASIMU YA KATIBA MPYA
 
Back
Top Bottom