KING COBRA
JF-Expert Member
- Nov 10, 2011
- 2,782
- 864
Mhe Pinda alimujibu Mhe Godfrey Zambi Bungeni kuwa Suala la Kahawa Mbichi , Wakulima Waachiwe wapange wao wenyewe bei ya kahawa Mbichi na wachague wenyewe ni nani wa kumuuzia !!
Zambi na Wana CCM wengine Mkoani Mbeya Mbozi walipiga marufuku ununuzi wa Kahawa Mbichi kwa Wakulima.
Source: Gzt Mwananchi leo pg 20
Soma Barua hii ya Wakulima upate Ukweli !!!!!!!!!!!!
04/02/2012 MHESHIMIWA KATIBU MKUU (CHIEF SECRETARY) IKULU – DAR ES SALAAM S.L.P 9120 DAR ES SALAAM. Somo tajwa hapo juu la husika sana. Mh. Rais. Sisi ni wakulima maelfu kutika Wilaya ya Mbozi, Mbeya vijijini, Rungwe na Ileje Mkoni Mbeya, tumekuandikia barua hii ili kukuonyesha kero zinazotengenezwa na watendaji serikalini ili kugandamiza wakulima, kuua zao la kahawa na kwa kutumia madaraka yao vibaya hali inayochochea migogoro vijijini. Mhe Rais mwaka 2011 ilifanyika agenda na mbinu chafu mno kati ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya wakati huo kwa kushirikishiana na Wakuu wa Wilaya za Mbeya, Mbozi, Rungwe na Ileje wakiwemo wakurugenzi watendaji wa Mbozi, Mbeya na Rungwe zilizolenga kumuondoa mwekezaji LIMA kwenye ununuzi wa kahawa mbivu (red cherry). Kutokana na LIMA kufanya vizuri sana katika kuboresha zao la kahawa na maisha ya mkulima kuliko vikundi na kampuni yote. Mhe Rais kampuni ya uwekezaji LIMA ambayo hapa Tanzania inaendeshwa na watanzania wenyewe wenye taaluma ya kahawa tangu 2004 imeleta mabadiliko makubwa kwetu wakulima kwa kujenga viwanda vya kumenya kahawa mbivu mabwawa ya maji na ugavi na madawati mashuleni na uchangiaji wa huduma za afya kwenye hospitali. Kampuni LIMA ndiyo inayoongoza kwa kutoa ajira kwa wananchi na vijana wengi Mkoani Mbeya pamoja na huduma ya ugani kwa mkulima wa kahawa na mashamba darasa. LIMA ndiyo kampuni pekee ambayo imefanikiwa kuboresha kahawa yetu kimataifa na kwa sasa tumepata masoko Marekani na Japan siyo hivyo tu LIMA imehamasisha vijana kupenda kilimo hususani kahawa kwa asilimia 80 na kuondoa uhalifu hasa hasa Wilayani Mbozi ambako jeshi la polisi Mkoani Mbeya lina kata ya mfano wa usalama, kata ya Isansa ambayo ilikuwa inaongoza kwa uhalifu Mkoani Mbeya, lakini leo vijana wapo kwenye kilimo cha kahawa kwa msaada wa LIMA. Sisi wakulima tumeona faida kubwa kwenye mauzo ya kahawa mbivu au cherry kwani inatuondolea usumbufu kwenye maandalizi kutokana na uhaba wa maji na vitendea kazi vingine ili kufikia ubora, ukiuzwa kahawa mbivu kwa LIMA unalipwa na mabaki kila mara bei zinapopanda kwenye soko. Kama uliza kilo moja kwa Tshs 2000 na bei zikapanda mara mbili kwenye soko mkulima analipwa Tshs 5000 kwa kilo ya kahawa mbivu. (kupita hata bei elekeziza serikali). Mhe, mbinu hiyo chafu ilitokana na mwekezaji LIMA kufanya kazi vizuri ya kumfufua mkulima wa zao la kahawa ambaye nyuma yake tulikuwa wafu. Kutokana na kudolola kwa bei za kahawa, ujio wa mwekezaji LIMA ambaye alipoingia Mkoani Mbeya mwaka 2004 amekuwa mkombozi kwetu wakulima wadogowadogo na wakati ni asilimia 100 ya wakulima wote Mkoani Mbeya, kwa kuongeza ubora wa kahawa, bei na kutupatia mbolea bila riba. Hivyo kitendo cha kumpiga vita LIMA ni kuwapiga vita maelfu wakulima wadogo na wakati ambao tunakombolewa na mwekezaji LIMA kwani tumegundua kuwa umaskini tuliokuwa nao wa kukosa mbolea na bei duni za kahawa, ulikuwa mtaji kwa mafisadi wakiwemo wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi watendaji tuliowataja kwenye Wilaya hizi kwani wao wanauza pembe jeo kwa bei ya juu mno ambapo mbolea aina ya DAP wanatuuzia kwa Tshs 240,000/= walanguzi hao pamoja walioko na watendaji wako wanauza pia mbolea aina ya UREA kwa Tshs 180,000/= CAN 120,000/= wakati mwekezaji LIMA mbolea hizo hizo atuuzia kwa Tshs 75, 000/= , UREA 65,000/= na CAN 50,000/= unaweza kuona tofauti hii. Mhe Rais hii ni orodha chache tu ya viongozi wanaojishughulisha na ununuzi wa kahawa kwa kutengeneza vikundi hewa, vya kitapeli na vikundi vya kifamilia ili kutengeneza migogoro kwa lengo la kuendelea kufaidi jasho letu huku wakisimama majukwaani na hawakubali bei za kionyonyaji kwa mkulima wa kahawa kumbe wao ndiyo wanyonyaji na mafisadi na wanafiki wabaya. Na ndio maana mpango wa vocha za mbole umeshindwa kumsaidia mkulima, kutokana na vocha hizo kuishia mikononi mwa majambazi hawa, yaani Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Madiwani na Wafanyabiashara majambazi. Tumekutumia barua za siri za utekelezaji wa maagizo ya kumjumu LIMA kutoka kwa Wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya kulingana na agizo la siri lilllosambazwa na mafisadi hao kwa kupitia Mkuu wa Mkoa wakati huo na jambo ambalo ni kinyume kabisa na sheri Na. 23/1001 ya kahawa. Mkuuu wa Wilaya Mhe. Gabriel Kimalo anajihusisha na kufanya biashara chini ya mwamvuli wa kikundi cha Peoples Coffee Group na Mpito Coffee Group. Vikundi hivi hujihusisha na ununuzi wa kahawa mbivu ambayo Mhe. Gabriel anaikataza kampuni ya LIMA isinunue licha ya kampuni hiyo kuwekeza kwenye ujenzi wa mitambo ya kumenyea kahawa mbivu 23 ya thamani ya mabilioni ya fedha kwenye Wilaya zote za kahawa. Aidha Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya Mbozi Ndigu Aloyce Mdalavuma ni mnunuzi wa kahawa mbivu na anamiliki kikundi cha Guzyo Farmers Group. Yeye ni Mwenyekiti wa kikundi hicho na hadi leo hajawalipa wakulima. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya anaitwa Eric Ambakisye Minga. Yeye ni mwanahisa kwenye kikundi kinachoitwa Peoples Coffee Group. Kikundi hiki kinanunua na kusindika kahawa mbivu. Afisa Ntumishi wa Wilaya Ndugu Ngaikwela ana mahasiano ya kibiashara na Ndug Adam Kalonge mmiliki wa Mpito Coffee Group ambaye ni mnunuzi wa kahawa mbivu. Ndugu Burton Sinienga Diwani ya kata ya Ipunga ni mmiliki wa kikundi kinachoitwa Ifungo Coffee Group,. Kikundi chake bado kinadaiwa na wakulima. Ndugu Sende Shula Diwani ya kata ya Myovizi ni mmikliki wa kikundi cha Ichesa Coffee Group., na katibu wa kikundi hicho. Mpaka hivi tunavyozungumza anadaiwa na wakulima. Mbunge Godfrey Zambi anafanya biashara kwa ushilikiano wa siri na Musa Zambi na Burton Sinienga Diwani wa kata ya Ipunga kupitia kikundi kiitwacho Ifungo Coffee Group. Mhe. Rais zichukuliwe hatua za haraka kuzuia agenda hiyo chafu ambayo imepangwa na mafisadi kupitia watendaji wa Halmashauri ili kuhujumu wanunuzi wanaojali maslai ya wakulima kama LIMA kwa lengo la kupata nafasi kuhodhi soko na wakulima tusiwe na uchaguzi wa mahali bora pa kuuza kahawa yetu. Iundwe tume kuchunguza mwenendo wa viongozi wa Mkoa na hasa Wakuu wa Wilaya wa Mbeya, Mbozi na Rungwe ambapo kwa mfano Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe amepora kilo 483 za kahawa mbivu na kilo 1090 za kahawa kavu kutoka kwa wanunuzi wa kampuni ya LIMA vijijini na kwenda kuiuza kusikojulikana je? Haya ni maadili ya utumishi wa um,ma? Mhe. Rais tunaomba usifumbie macho siri iliyojificha kwenye mkanganyiko uliojitokeza wakati wa ziara ya Waziri wa kilimo na chakula Mhe. Jumanne Magembe ambapo watendaji hao bila aibu waliamua kumtukana na kumdhalilisha Waziri na kumnyima kabisa fursa ya kuongea na wakulima ambao ndio tulikuwa tunamsubili kwa hamu sana. Mhe. Rais mfumo wa bodi ya kahawa TCB ubadilishwe ili bodi iwe na jukumu la kutafuta masoko, kusimamia, ubora na bei badala ya sasa ambapo bodi inafanya biashara kwani viongozi wakuu wa bodi (TCB) wako nyuma ya mbinu hii chafu. Mwenyekiti mhe. Pius Genze na Mkurugenzi (Adolph Kumbulu) wa bodi ya kahawa walifanya vikao katika kila Wilaya wakishauri Makampuni wanyimwe vibali vya kufanya biashara ya kahawa mbivu (cherry). Tunaamini japo ili lina siri nzito nyuma yake kwani Mkurugenzi (Adolph Kumbulu) pamoja na Mwenyekiti (Mhe. Ngeze ) wa bodi ya kahawa kwa pamoja wana maslahi kwa biashara iendeshwayo na Kilcafe chini ya ushauri wa kitaalamu unaotolewa na Technoserve. Ili kulinda maslahi ya Kilcafe Mkurugenzi ameamua kwa makusudi kushawishi Halmashauri zipige marufuku biashara ya kahawa mbivu. Msukumo huu ulitokana na Kilcafe kushindwa kabisa kuhimili ushindani wa ununuzi wa kahawa mbivu, hivyo namna pekee ya kuinusuru ambayo ilibuniwa na Mkurugenzi wa bodi ya kahawa ni kusitisha utoaji wa leseni ya ununuzi wa kahawa mbivu. Usitishaji huu ulianza mara tu Adolph Kumbulu alipoteuliwa kuwa Mkurugenzi wa bodi ya kahawa 2008/2009. Mhe. Rais migogoro hii ni chanzo chake kikubwa ni Mkurugenzi wa bodi ya kahawa (TCB) ambaye ameigeuza bodi hiyo kama zizi lake la mbuzi anachinja apendavyo, ndiye anayetumika na mafisadi maneno yake ni tofauti na matendo yake chonde chonde sisi wakulima tunaiona TBC mzogo mkubwa kwetu. Mhe. Rais tunaungana na Waziri wa kilimo Ushirika na chakula kusisitiza ushindani wenye lengo la kuboresha kahawa na bei, ndio uwe msisitizo na si vinginevyo vita hii ya kimaslai tunaiona kwamba itatudhuru wakulima kwani uuzaji wa kahawa mbivu umetuondoa kwenye umaskini kwa sasa tunalipa karo za watoto wetu kwa wakati, kununua pembe jeo kwa wakati na pia imetoa ajira kwa vijana wetu na kupunguza matukio ya kihalifu. Mhe. Rais MUHIMU LESENI na vibali vya ununuzi wa zao la kahawa vitoke wizarani na sio kwenye Halmashauri wala bodi ya kahawa. Bodi na Halmashauri wabaki na jukumu la kusimamia sheria zao la kahawa Na. 23 ya 2001 tu ili kuondoa ukiritiba na mianya ya rushwa kwa Wakurugenzi na Watendaji wa Halmashauri. Mbinu za kuzuia ununuzi wa kahawa mbivu (red cherry) zina lengo la kuua ubora wa kahawa na kurudisha umaskini kwa wakulima kwani ni asilimia 20 tu ya kahawa mbivu zonazopita kwenye viwanda vya kumenyea kahawa hiyo katika Mikoa ya nyanda za juu wakati wenzetu wa Kigoma zaidi ya asilimia 70 ya kahawa mbivu zinapita kwenye viwanda (CPU). Mhe. Rais sisi wakulima wa zao la kahawa hususani Wilaya ya Mbozi, Mbeya, Ireje na Rungwe tunayo imani na wewe na serikali yako kwamba kilio chetu kitafanyiwa kazi, ikiwa ni pamoja na kuwawajibisha mara moja Wakuu wa Wilaya za Mbozi, Rungwe na Mbeye na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi ambaye dhahili hana maadili ya uongozi kwani kitendo cha kumtukana Waziri wa kilimo na Rais aliye mteua hadharani kimewaacha wananchi na taswira tofauti tangu tarehe 16/01/2012. Mhe. Rais baada ya kukupatia picha sahihi, ya kero, hujuma na matumizi mabaya madaraka ya baadhi ya watendaji Mkoani hapa tunavyotendewa, CHONDE CHONDE Mhe. Rais na Mhe. Waziri wa Wizara ya kilimo na Ushirika na chakula tunaomba serikali itoe haraka Leseni na Kibali kwa mwekezaji LIMA ili ianze kutugawia mbolea kwani mpaka sasa anasubili Leseni na vibali na sisi wakulima tungali tumepanga foleni kwake kusubili mbolea. Ili tuanze kumwaga mashambani kwani mwaka huu kahawa zimeanza vizuri na kama hatutapata mbolea mapema punje zitaharibika. Na mwisho wakulima tumeapa kamwe hatupo tayari kuruhusu kampuni nyingine za mafisadi kuchukua kahawa zetu zaidi ya LIMA mkombozi wa mkulima wa kahawa nyanda za juu kusini ambaye tumeamua kuingia mikataba ya kumuuzia kahawa mbivu (red cherry). Kikao cha muungano kw Wakulima wa kahawa 1240 kilichofanyika tarehe 04/02/2012 mji mdogo wa Mlowo. Chini ya Mwenyekiti Japhet Kibona…………………………………………………………… Dickison Nzowa ……………………………………… Joel Mwakangale ………………………………….. na Abeli Mwashamba……………………………………………………….. Tunawakilisha kwako Mheshimiwa Rais. Kutika kata za:- 1. Bugoba – Tukuyu 2. Luswiswi – Ileje 3. Iluya – Mbozi 4. Kagwina – Tukuyu 5. Ikuti – Tukuyu 6. Kijiji cha bara – Mbozi 7. Kijiji cha Mlangali – Mbozi 8. Igamba – Mbozi 9. Kijiji acha Msia – Ireje 10. Kijiji cha Luwati – Mbozi 11. Kijiji cha Magamba – Mbozi 12. Kijiji cha Ruanda – Mbozi 13. Kijiji cha Uhowa – Mbozi 14. Kata ya Isansa 15. Kata ya Ihanda 16. Kata ya Igamba 17. Kata ya Ipunga 18. Kata ya Nyimbili 19. Kata ya Iyula 20. Kata ya Halungu 21. Kata ya Itaka 22. Kata ya Msiya 23. Kata ya Itengule – Mbeya vijijini 24. Kata ya Mlangali 25. Kata ya Myovizi 26. Kata ya Ruanda 27. Kata ya Nambinzo
NAKALA:- MHE: WAZIRI MKUU,
MIZENGI PINDA – (MB), S.L.P 1923 DAR ES SALAAM/DODOMA.
WAZIRI KILIMO NA USHIRIKA MHE. PROF J. MAGHEMBE, S.L.P 9192, DAR ES SALAAM
Zambi na Wana CCM wengine Mkoani Mbeya Mbozi walipiga marufuku ununuzi wa Kahawa Mbichi kwa Wakulima.
Source: Gzt Mwananchi leo pg 20
Soma Barua hii ya Wakulima upate Ukweli !!!!!!!!!!!!
04/02/2012 MHESHIMIWA KATIBU MKUU (CHIEF SECRETARY) IKULU – DAR ES SALAAM S.L.P 9120 DAR ES SALAAM.
YAH: AGENDA YA SIRI YA KUUA ZAO LA KAHAWA NA MAENDELEO YA WAKULIMA MKOA WA MBEYA NA UCHUMI WA TAIFA.
NAKALA:- MHE: WAZIRI MKUU,
MIZENGI PINDA – (MB), S.L.P 1923 DAR ES SALAAM/DODOMA.
WAZIRI KILIMO NA USHIRIKA MHE. PROF J. MAGHEMBE, S.L.P 9192, DAR ES SALAAM