ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 925
Mzee waupako Mchungaji Anthony Lusekelo amelalama kuwa udini unaoendelea kushamili umetengenezwa na unatokana na viongozi waliomfuatia Mwalimu Nyerere kupuuza vyanzo vya chuki za kidini tokea mwaka 1985. Akizungumza katika kipindi chake cha Utashinda kinachorushwa na TV ya Channel Ten, Mchungaji Lusekelo amesema "leo hii unamkuta Mwislamu au Mkristo amebeba Quran upande mmoja na Biblia upande mwingine na kukashifu dini ya mwenzake". Amesema ukristo au uislamu utatoweka lakini Tanzania bado itakuwepo. Kwake Tanzania inaweza kuwepo bila uislamu au ukristo.
Amelaumu sana Serikali na viongozi wake wakuu kwa kukosa fikra na maamuzi ya kukemea chuki zilizoanza kuibuka kwenye udini ikiwemo mihadhara ya dini na Radio zinazorusha matangazo ya kukashifu dini za wengine na viongozi kwa ujumla. Lusekelo amelaani kitendo cha Waislamu wachache kujichukulia sheria mikononi na kuamua kuchoma makanisa kwa kisa cha mtoto kukojolea msaafu. " Sisi wakristo ni waoga na tunaupendo wa Mungu, kama tungejibu na kuanza kuchoma misikiti hali ingekuwaje!?" Alihoji Lusekelo. Mzee wa upako amesema anampongeza sana Kamanda Kova na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambao ni waislamu kwa kauli walizotoa mara baada ya vurugu za uchomaji makanisa zilizoanzia Mbagala. Lusekelo anahoji" kama mtoto amekojolea msaafu, kwa nini asingechukuliwa na kupelekwa kwenye kanisa lake ili mchungaji wake aeleze iwapo kafundishwa afanye hivyo na makanisa badala ya waislamu kuanza kuchoma makanisa yote bila kujali mhusika ni wa dhahebu gani?". Mzee wa upako amesema wakristo watajuaje kama kweli huyo mtoto ni mkristo au hajapandikizwa ili kuleta vurugu? "Kama alikojolea msaafu basi waislamu nao kwa maana ya kulipiza kisasi wangekojolea biblia badala ya kuanza kuchoma makanisa utadhani huyo mtoto katumwa na wakristo afanye hivyo" amesema Mzee wa Upako.
Amelaumu sana Serikali na viongozi wake wakuu kwa kukosa fikra na maamuzi ya kukemea chuki zilizoanza kuibuka kwenye udini ikiwemo mihadhara ya dini na Radio zinazorusha matangazo ya kukashifu dini za wengine na viongozi kwa ujumla. Lusekelo amelaani kitendo cha Waislamu wachache kujichukulia sheria mikononi na kuamua kuchoma makanisa kwa kisa cha mtoto kukojolea msaafu. " Sisi wakristo ni waoga na tunaupendo wa Mungu, kama tungejibu na kuanza kuchoma misikiti hali ingekuwaje!?" Alihoji Lusekelo. Mzee wa upako amesema anampongeza sana Kamanda Kova na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambao ni waislamu kwa kauli walizotoa mara baada ya vurugu za uchomaji makanisa zilizoanzia Mbagala. Lusekelo anahoji" kama mtoto amekojolea msaafu, kwa nini asingechukuliwa na kupelekwa kwenye kanisa lake ili mchungaji wake aeleze iwapo kafundishwa afanye hivyo na makanisa badala ya waislamu kuanza kuchoma makanisa yote bila kujali mhusika ni wa dhahebu gani?". Mzee wa upako amesema wakristo watajuaje kama kweli huyo mtoto ni mkristo au hajapandikizwa ili kuleta vurugu? "Kama alikojolea msaafu basi waislamu nao kwa maana ya kulipiza kisasi wangekojolea biblia badala ya kuanza kuchoma makanisa utadhani huyo mtoto katumwa na wakristo afanye hivyo" amesema Mzee wa Upako.