Kwanini na ni namna gani Dr Idrissa Rashidi aliondoka TANESCO?

Mkuu,Inapokuja kuhusu Dr Idrissa huyu mtu kuna mapungufu anayo ila kiuongozi he is a person with credible image and highly professional. Mie namfahamu tangu NBC alikuwa mtu asiyependa mtu aonewe ofisini, anayependa usawa (hasa kwa wafanyakazi wa chini), mtu wa sala tano (nakumbuka kuna vikao NBC vikiifanyika ijumaa akawaambia jamaa wabadilishe utaratibu kwani ilikuwa ni siku anaenda kusali na hakupenda akose vikao hivyo). Kiufupi alikuwa ni mtu muadilifu na mwenye kutetea maslahi ya wanyonge. Ndio maana wakurugenzi wenzie walafi hawakuwa wakimpenda kwani alikuwa hapendi ufisadi.BOT alisafisha uchafu uliomo kiasi watoto wa vigogo waliotumwa kulinda maslahi ya baba zao pale walikuwa wakiona cha moto, amesaidia kuifanya banking system ya tanzania iwe ni stable kwa kuhakikisha ule utaratibu wa vimemo na wanasiasa kuingilia taratibu na uendeshaji wa kibenki zinapotea. Alifinya mianya ya ufisadi pale BOT (hata scandal ya radar SFO wamemtuhumu isipokuwa nilitarajia wangelimfikisha mahakamani ndio tungelijua ukweli uko wapi) ijapokuwa sina uhakika kwani naye binaadamu na hakuna mtu msafi.Tanesco aliendeleza rekodi yake aliyotoka nayo nyuma kwa kusafisha ufisadi uliokuwa unaendelea pale Tanesco. Baadhi ya wakurugenzi na wanasiasa hawakupenda hilo kwa sababu wajuazo wenyewe. Waulizeni wafanyakazi wa kawaida wa Tanesco wanamuonaje Dr Rashidi ndio utakapopatwa na mshangao ila viongozi wenzie walikuwa hawampendi. Ndio sababu aliamua kukaa pembeni awaachie shirika liwafie wenyewe.Ukisoma thread moja ilianzishwa na Tausi Mzalendo utafahamu kuwa tatizo la umeme nchini sio vyanzo vya umeme bali Tanesco inasumbuliwa na gonjwa sugu la UFISADI!!!! Mtu kama Dr Rashidi anakuwa left in the middle of the mess. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema If you think education is expensive try ignorance ndio matokeo ni haya umeme tunakatiwa masaa 24 na watu tunabakia bado tunavumilia, senegal wametangaziwa mgao tu wameandamana, kweli sisi watanganyika ni watu wavumilivu sana!!!!!
Kaka thanks huyu jamaa ni kichwa na uwezo wake aufichiki, kapigwa mizengwe yetu yakitanzania full stop, hii nchi naona bora waliokwepo milembe wanajijua wao vichaa sie wengine tumebaki tupo tupo tu
 
The Stigs said:
Hii ndiyo namna 99.999% ya waTZ wanavyofikiria. Fisadi, Fisadi, fisadi....

Mtazamo wa namna hii unajenga jamii ya watu wasioweza kufanya lolote. Wanabaki kuangaliana, nani anafanya ufisadi. Mwishoni mnakuaja hata kusingiziana wasio na hatia.

Tuko tayari kuwavumilia watendaji wabovu wasio na ufanisi eti tu kwa sababu siyo mafisadi. Wewe unamjua fisadi anafanana vipi lakini?

The Stigs,

..lakini how do u justify walichofanya Dr.Rashid na Chenge ktk ununuzi wa rada?

..kwasababu wanabongo sana basi waaachiwe tu wajinafasi kwa ufisadi kila wanapojisikia?

..inasikitisha kwamba mara kwa mara, wasomi wetu, tena wale wazuri kwelikweli,ndiyo wametutenda vibaya nchi hii.
 
Yes ni mtendaji mzuri lakini tayari ana kovu ambalo hata akipewa cheo gani kwa sasa
  • Trust ya watu walio chini yake haiwezi kuwa juu kama za amani na hiyo itaathiri utendaji wa sehemu yeyote atakayokuwepo
The only thing kinachoweza kumsaidia labda CDM wachukue nchi naye anaweza kusema ukweli wote wa jinsi may be alivyoshinikizwa ushiriki kwenye UFISADI na magamba.

Form there atakuwa dr Idris rashid ambye watu watamuamini. Right now may be naogpa kutoa ukweli wa sequence za event za mambo ya ufisadi yaliypfanyika chini yake pale BOT.

So kundoka kwa taneceo na kutfanikiwa kwakwe ni sbabu ya wingu na mzimu wa BOT.

Otheriwise angeperform vizuri

The Stigs,

..lakini how do u justify walichofanya Dr.Rashid na Chenge ktk ununuzi wa rada?

..kwasababu wanabongo sana basi waaachiwe tu wajinafasi kwa ufisadi kila wanapojisikia?

..inasikitisha kwamba mara kwa mara, wasomi wetu, tena wale wazuri kwelikweli,ndiyo wametutenda vibaya nchi hii.

Muu Ndiyo yale yale kama ya Lowasa Vs Pinda. Kwa hiyo kuna watu wanataa tuwe na sheria mbili wa uwatazama viongzi wasio waaminifu. Kama ni mchapakazi tumpotezee. Kama sio mchapakazi basi ndio tupige kelele.mhhhhhhh

Wananchi hata hawajui vigezo gani muhimu vya kuchagua wabunge. Tumeshadanganywa tungalie vyeti kama ndio kitu muhimu.... mhhhhh
 
The Stigs,

..lakini how do u justify walichofanya Dr.Rashid na Chenge ktk ununuzi wa rada?

..kwasababu wanabongo sana basi waaachiwe tu wajinafasi kwa ufisadi kila wanapojisikia?

..inasikitisha kwamba mara kwa mara, wasomi wetu, tena wale wazuri kwelikweli,ndiyo wametutenda vibaya nchi hii.


Ni kwamba inabidi kuachana na hii tabia ya kutanguliza ufisadi, ufisadi, ufisadi kwenye kila jambo tunalozungumza. Yaani, hakyanani; kuna siku atatokea mtu atayesema kuwa fulani hafai kuwa Best Man wa harusi kwa sababu ni fisadi!

Tumekuwa vipofu. Vichwa vyetu vimejaa takataka za fisadi, fisadi, fisadi, mpaka tunaboa.

Sasa hapa tunamzungumzia mtu aliyejijengea heshima kubwa ya ufanisi katika kuongoza mashirika makubwa. Sijui kama kuna wengine wengi wa calibre yake, labda nitajie. lakini watu wanaelekea kule kule; fisadi, fisadi, fisadi... napita jamani.
 
The Stigs said:
Ni kwamba inabidi kuachana na hii tabia ya kutanguliza ufisadi, ufisadi, ufisadi kwenye kila jambo tunalozungumza. Yaani, hakyanani; kuna siku atatokea mtu atayesema kuwa fulani hafai kuwa Best Man wa harusi kwa sababu ni fisadi!

Tumekuwa vipofu. Vichwa vyetu vimejaa takataka za fisadi, fisadi, fisadi, mpaka tunaboa.

Sasa hapa tunamzungumzia mtu aliyejijengea heshima kubwa ya ufanisi katika kuongoza mashirika makubwa. Sijui kama kuna wengine wengi wa calibre yake, labda nitajie. lakini watu wanaelekea kule kule; fisadi, fisadi, fisadi... napita jamani.

The Stigs,

..you have a point, but I feel like you blaming the victims and not the perpetrators of ufisadi.

..waliotufikisha hapa ni hao hao kina Rashid,Chenge,Mkapa,Yona,Mramba,Magufuli,Karamagi,Lowassa,Msabaha... ambao wanachanganya usomi,utendaji mzuri, na ufisadi.

..labda topic ingebadilishwa na kuwa titled " The non ufisadi side of Dr.Rashid " hapo ungetu-limit wale tunaozongwa na rekodi yake ya ufisadi.

 


The Stigs,

..you have a point, but I feel like you blaming the victims and not the perpetrators of ufisadi.

..waliotufikisha hapa ni hao hao kina Rashid,Chenge,Mkapa,Yona,Mramba,Magufuli,Karamagi,Lowassa,Msabaha... ambao wanachanganya usomi,utendaji mzuri, na ufisadi.

..labda topic ingebadilishwa na kuwa titled " The non ufisadi side of Dr.Rashid " hapo ungetu-limit wale tunaozongwa na rekodi yake ya ufisadi.

Joka kuu,

Labda nikutolee uvivu nikuulize mkuu katika tuhuma zote alizotuhumiwa Dr Rashid ni ngapi amefikishwa mahakamani? Elewa mkuu ukiwa kiongozi tuhuma na lawama haziepukiki. Kuna mama mmoja NBC ya zamani walimtuhumu we kama fisadi ilipokuja kugundulika alizushiwa tayari alikuwa ameshahama kwenda benki nyengine. Nilifurahi SFO walipomtuhumu Dr Rashid nilitegemea watamfikisha mahakamani kwani siri zingelifichuka nyingi hilo halikufanyika labda tusaidie wewe Dr Rashid alishiriki vipi na wapi katika Radar?
 
fisadi sijui sio fisadi sisi haituhusu...tatizo nitupo gizani tunafanyaje kama wananchi kuwapush hawa viongozi ambao sijui´tuwaitaje...wazembe...s.t.u.p.i.d..narrow minded.....tugome kwenda kazini? Ama tufanyeje..sauti isikike
 
Nimemkumbuka Dr Idrissa baada ya mgao huu mkali wa umeme. Kufuatia rekodi yake nzuri akiwa BOT na kwa mujibu wa watu waliofanya naye kazi TANESCO Dr Rashidi ninaamini aangepewa mamlaka ya kutosha na rasilimali angeweza kuligeuza shirika hili kufanya kazi kwa ufanisi na sina shaka tatizo la umeme linalotukabili sasa lisingekuwa kubwa kiasi hiki. Binafsi namuona Dr Rashidi kama mtu mwenye vision na anayeweza kufanya maamuzi magumu na kuyasimamia.

Ni kwa nini Dr Rashidi aliondoka/aliondolewa TANESCO ilihali alikuwa mtu muafaka to turn around this Company?

Naomba kujua wadau!
Hili jizi kubwa kabisa tena sana, lililokwapua fedha za rada ndio mnasema ni kichwa? Ebo! mmelogwa?
 
Joka kuu,

Labda nikutolee uvivu nikuulize mkuu katika tuhuma zote alizotuhumiwa Dr Rashid ni ngapi amefikishwa mahakamani? Elewa mkuu ukiwa kiongozi tuhuma na lawama haziepukiki. Kuna mama mmoja NBC ya zamani walimtuhumu we kama fisadi ilipokuja kugundulika alizushiwa tayari alikuwa ameshahama kwenda benki nyengine. Nilifurahi SFO walipomtuhumu Dr Rashid nilitegemea watamfikisha mahakamani kwani siri zingelifichuka nyingi hilo halikufanyika labda tusaidie wewe Dr Rashid alishiriki vipi na wapi katika Radar?
Hajafikishwa kortini kwa sababu wanaoongoza nchi ni mafisadi wenzake. Angekuwa China sasa hivi angekuwa marehemu. Eti linajifanya ni jitu la sala wakati ni jizi zoefu!
 
Joka kuu,

Labda nikutolee uvivu nikuulize mkuu katika tuhuma zote alizotuhumiwa Dr Rashid ni ngapi amefikishwa mahakamani? Elewa mkuu ukiwa kiongozi tuhuma na lawama haziepukiki. Kuna mama mmoja NBC ya zamani walimtuhumu we kama fisadi ilipokuja kugundulika alizushiwa tayari alikuwa ameshahama kwenda benki nyengine. Nilifurahi SFO walipomtuhumu Dr Rashid nilitegemea watamfikisha mahakamani kwani siri zingelifichuka nyingi hilo halikufanyika labda tusaidie wewe Dr Rashid alishiriki vipi na wapi katika Radar?

Kumfikisha kiongozi wa umma mahakamani kukabiliana na mkono wa sheria ni jambo linalohitaji utashi wa kisiasa. Kama hakuna hili hata kuwe na kiasi gani cha ushahidi hili haliwezi kutokea. Kwa msingi huo kutofikishwa kwake mahakamani (kama ilivyo kwa baadhi ya watuhumiwa) hakumaanishi kuwa hana hatia bali ukosefu wa utashi wa kisiasa.

Pamoja na kusema hayo hapo juu nakiri sijui chochote kuhusiana na Dr Rashid hivyo sijui kama ni fisadi ama la.
 
He did make a lot of 10% during his tenure, so he's rich he was in Tanesco from Bank of Tanzania... so he collects some Greens and leave as every other official in that Government after Azimio la Zanzibar no one cares about the country called Tanzania.

NO ONE GAVE A DAMN ANYMORE WHO CARES!!!

Hili azimio la zanzibar ni nini? liliitishwa lini na makusudi yake ni yapi? naomba mwelewa anifahamishe
 
Wamekumislead. Kile ni kifaa.

Na hata kama alikuwa na mapungufu yake, cha muhimu ni kuwa chini yake umeme ulikuwa unapatikana, period.

Yaani ni mjanja kumshinda Kiranja mkuu? kijana chunga kauli zako, zitakufikisha pabaya! Muulize kiranja mkuu kwa nini alitimuliwa tanesco kabla ya kupiga longolongo JF.

Tatizo la umeme nchini haliwezi kutatuliwa na mtu mmoja Dr. rashid peke yake, nadhani hapa kuna hidden ajenda....... lol!!
 
Joka kuu,

Labda nikutolee uvivu nikuulize mkuu katika tuhuma zote alizotuhumiwa Dr Rashid ni ngapi amefikishwa mahakamani? Elewa mkuu ukiwa kiongozi tuhuma na lawama haziepukiki. Kuna mama mmoja NBC ya zamani walimtuhumu we kama fisadi ilipokuja kugundulika alizushiwa tayari alikuwa ameshahama kwenda benki nyengine. Nilifurahi SFO walipomtuhumu Dr Rashid nilitegemea watamfikisha mahakamani kwani siri zingelifichuka nyingi hilo halikufanyika labda tusaidie wewe Dr Rashid alishiriki vipi na wapi katika Radar?

Mkuuu nakushauri sikiliza huyu proffesor wa Havard alafu utapa jibu


Kama huna muda then soma hii kisa
mama mmoja ana mapesa mengi. Nyumbani kwake bomba limeharibika linavuja. Anakuja fundi anacheki anamwambia kurekebisha tatizo atahitaji ununua vifaa na gaharama ya ufudi wake alipwe milioni 4. Kutokana na bibi kutokujua mambo ya ufundi na sababu ana pesa wanazomtumia wanae walio ulaya anamwambia fundi waende beki akamchukulie hizo miloni 4.

Kufika benki yule mama anajza fomu ya kuchukua milioni nne. Muhudumu wa benki anamuuliza za nini mbona sio kawaida yako . Yule mama anamwambia ni za kutengeneza bomba. Muhudumu wa benki anapiga simu polisi....... Anyway simaliiziii story.

Hapa kuna hoja hii
  • Kisheria unaweza kuwa huna kosa lakini kimaadili (ethics) ukawa na kosa Yule fundi hana kosa sbabu mkataba wa makubalno kati yake na mama wamekubaliana lakini kimaaadili ya ufundi ni Kosa.
  • Pia ukiangali hizo clip utaona professor anauliza kuna tofauti gani kati ya outright lie and misleading truth. Na anatolea mfano wa Clinton na Lewinsky.
So usiruhusu tu mambo ya kisheria yawe ndo mwisho wa kuhoji kwako.

Dr Idriss ni kiongzi mzuri lakini inawezekana ni CCM walimtumia na kumcfaua. Kama yeye mwenyewe hayuko tayari kujisafisha huo mzimu atakuwa nao kama alivyo nao Mkapa, Mramba na Chenge.

Kufungwa kwa jalada lao SFO doest mean they are clean.
 
Last edited by a moderator:
sababu ya Iddriss Rashid kuondoka Tanesco ni za kibinafsi zaidi.Wakati fulani Idriss alikuwa Mkurugenzi wa Vodacom wakati Ngeleja alikuwa mwanasheria wa voda,walikuwa na mahusiano mabaya sana.
Malima alitemwa Bot wakati Iddriss alivyokuwa pale.
Balaa likaja Iddriss alipoteuliwa kuwa mkurugenzi wa tanesco akawa katikati ya wabaya wake;NGEREJA waziri wa nishati na madini,MALIMA naibu waziri.Wakamtimua kwa aibu sana sote tunakumbuka,katika kulipiza kisasi. HII NDO BONGO;FITNA FITNA
 
Kuna wakati mwanasiasa mmoja wa Kambi ya Upinzani aliwahi kusema Watanzania ni watu wa ajabu sana, "Umeme ukikatika wanafurahia na Umeme ukirudi wanafurahia pia" kuwabadilisha watu altitude si kazi ndogo.

Karata naomba jina la huyu mwanasiasa
 
Mkuuu nakushauri sikiliza huyu proffesor wa Havard alafu utapa jibu


Kama huna muda then soma hii kisa


Hapa kuna hoja hii
  • Kisheria unaweza kuwa huna kosa lakini kimaadili (ethics) ukawa na kosa Yule fundi hana kosa sbabu mkataba wa makubalno kati yake na mama wamekubaliana lakini kimaaadili ya ufundi ni Kosa.
  • Pia ukiangali hizo clip utaona professor anauliza kuna tofauti gani kati ya outright lie and misleading truth. Na anatolea mfano wa Clinton na Lewinsky.
So usiruhusu tu mambo ya kisheria yawe ndo mwisho wa kuhoji kwako.

Dr Idriss ni kiongzi mzuri lakini inawezekana ni CCM walimtumia na kumcfaua. Kama yeye mwenyewe hayuko tayari kujisafisha huo mzimu atakuwa nao kama alivyo nao Mkapa, Mramba na Chenge.

Kufungwa kwa jalada lao SFO doest mean they are clean.


Mkuu,

Sijasema kuwa Dr Idrissa sio fisadi ila nachosema anatuhumiwa kuwa fisadi. Anachozungumza huyo hapo (Professor wa Harvard) just technically is a burden of proof . Kwenye Civil lawsuits kama hizi za ufisadi the burden of proof lies on the accuser. Sasa kama SFO walikuta katika account ya Dr Rashid kuna $600,000 waprove kama hizo hela zimetokana na ufisadi wa radar? Venginevyo inabakia tuhuma tu zilizoshabihiana na majungu.

Tunapojadili utendaji, na umakini na uzalendo wa huyu jamaa namuunga mkono Zitto kwa kauli yake he is the best CEO we have in Tanzania so far.
 
Last edited by a moderator:
sababu ya Iddriss Rashid kuondoka Tanesco ni za kibinafsi zaidi.Wakati fulani Idriss alikuwa Mkurugenzi wa Vodacom wakati Ngeleja alikuwa mwanasheria wa voda,walikuwa na mahusiano mabaya sana.
Malima alitemwa Bot wakati Iddriss alivyokuwa pale.
Balaa likaja Iddriss alipoteuliwa kuwa mkurugenzi wa tanesco akawa katikati ya wabaya wake;NGEREJA waziri wa nishati na madini,MALIMA naibu waziri.Wakamtimua kwa aibu sana sote tunakumbuka,katika kulipiza kisasi. HII NDO BONGO;FITNA FITNA

Ukweli ukidhihirika uongo hujitenga. Time will tell!!!
 
Nimekugongea senks.Chini ya Idrissa, hali tuliyonayo isengeweza kukatiza. Hii ndiyo tofauti ya Kiongozi anayeendesha kwa kutafuta matokeo na Kiongozi anayeogoza kwa kufuata taratibu tu.
Kwakweli Idrissa alikuwepo NMB muda mdupi tu kabla hajateuliwa kwenda TANESCO. Huo muda mfupi aliokaa NMB impact yake ilikuwa felt mpaka kwa watu wa chini kabisa. Idrissa is the MAN no matter what anybody says. Binadamu wate wanamapungufu lakini Idrissa ni mtu mzuri sana anatetea watu wa chini anamsimamo hayumbishwi na ni very analytical anajua anapodanganywa etc etc. Uzuri wake pia sio mtu wakusikiliza majungu. Alivyoondika NMB watu hasa wa chini walisikitika sana. NMB wamekuja hao wa Dutch wanasikiliza majungu vibaya mno kutoka kwa hao hao watanzania wenzetu ambao wako nao karibu. Matokeo yake ni kwamba watu innocent wananyanyaswa wanaacha kazi etc etc. Wa Dutch wanaajiri ma CD wao wanaowaokota barabarani nakuwalipa mishahara mikubwa. Watanzania wenzetu ndio wanaowaunganishia. Rate ya employee turnover ni kubwa mno toka walivyokuja hao wa Dutch (Bas Nierop na wenzake) lakini ndivyo wanavyopenda ili walete machangu doa kufill hizo gaps wakisaidiwa na Imani Kajula)pamoja nakuwagawia 10 percent. Idrissa tunamlilia mpaka mwisho!!
 
Back
Top Bottom