Kwa nini kina mama wengi hawawapendi wake au wachumba wa watoto wao

Joyceline

JF-Expert Member
Jan 9, 2009
1,010
166
Nimekuwa nikionana wamama wengi hawawapendi wake au wachumba wa watotot wao wa kiume bila sababu maalumu hii inasababishwa na nini.
Kuna kijana mmoja (true story0alilelewa kwenye kituo cha watoto yatima tangu mwaka 1978, amekuwa mkubwa akaamua kumtafuta mama yake, mama yake alimpeleka hapo kituoni akiwa na siku tatu baada ya kushidwa kumtunza sasa ametafuta kuulizia hapo kituoni sister aliyempokea miaka hiyo huyo sister amesharudi ulaya akamwelekeza mwanamke alivyo na alisema yeye ni wa wapi. kijana kamtafuta kampata, alivyompata akamtuma mchumba kwa sababu yeye alikuwa mgonjwa binti akaenda kufika akakuta mama ana hali mbaya sana hana hata kanga za kujifunga watoke. msichana kakimbia duka la jirani kaleta pea ya vitenge na kitambaa cha kichwa na viatu, alipofika mama kamwambia unaleta dharau nimekuomba uninunulie nguo unaniona mimi maskini. walipofika kwa mtoto wake akamwambia huyu ni nani aksema ni mchumba wangu akamwambia simtaki akaulizwa kwa nini akasema nimeamua simtaki na hapa kwako siondoki ndo nimeshafika, chagua mimi au yeye, kumbuka hajamuona tangu ana siku tatu. huyo mama ana mume na waotot watatu. nini kilisababisha ni kwamba ana roho mbaya ni tabia yake au? maana anadai waotot wake wengine wamemkimbia hawataki kumsaidia hata 500 hawampi
 
That is because they think whoever their son or daughter is dating is just not good enough. I don't know why that is but it-is-what-it is. At the end of the day your parent ain't the one who is going to be married to your spouse. So he or she can have their opinion but unfortunately they won't be the decider on whom I'm going to be with.
 
Hapa inaonesha mama ndio mwenye matatizo na hiyo ni tabia yake hadi wanae wakamkimbia. Hawezi kuanza kumchukia binti wa watu hata hajamjua vizuri.
 
Hapa inaonesha mama ndio mwenye matatizo na hiyo ni tabia yake hadi wanae wakamkimbia. Hawezi kuanza kumchukia binti wa watu hata hajamjua vizuri.

Huwezi kuamini ndo kamuona ndani ya lisaa anamchukia, anauliza nyumba ya nani? gari la nani? jamaa akamjibu mimi hapa natuzwa na huyu dada sina kitu (amemdanganya) akanyamaza kimya yaani ni mshari sijawahi kuona ameulizwa hicho ndo kilichokuleta hapa? alifikiri mtoto wake ni legelege alivyokuta ana msimamo akanywea, lakini mama mshari najua hapo ameenda kupanga plan B hawezi kushidwa. amasema mimi nataka mtaji sh. kadhaa amepewa ameondoka sijui what next
 
Mama zetu wengi huingiwa na hofu ya aina ya wakwe zao kwa sababu ya ubinafsi na wakati mwingine ni kweli huwa sahihi ktk jitihada za kuwaokoa vijana wao wasiingie mlango wa kutokea......kwani wengi wao huwaza maisha ya baadae (wanapozeeka) na ikumbukwe kuwa kwa familia za kibantu mtoto wa kiume ndio huwa mwenye jukumu la kutunza wazazi.

tatizo letu vijana nao siku hizi tumekua civilized kiasi cha kwamba hatuangalii ht nn cha kufanya na kwa mazingira yapi. Mf binti unapelekwa ukweni kwa mara ya kwanza na ni kijijini sn na ht wakwe zako wenyewe hawako civilized km ww, ukiwa umejibana kwenye sin jeans wategemea nn hapo km si kukatawaliwa hapo hapo???

Tuwaeleweshe tu vizuri nanyi wakaka muwe mnawashauri wachumba wenu kufanya yale yatakayoendana na family yako coz u know ur background!
 
Kwa kufuata maelezo yako hapo juu ,
inaonesha huyo mama hana upendo wa dhati kwa wanaye wa kuwazaa, ndiyo maana pia imekuwa rahisi sana kwake kumchukia huyo mchumba wa mwanaye wa kiume,japo huyo dada ameonesha upendo kwa mama mkwe wake.
Kutokana na kutokuwa na upendo moyoni mwake kwa watoto wake ndiyo maana hata watoto wake wa kuwazaa hawako karibu naye,pia
ndiyo maana hata yeye ilikuwa rahisi kwake kumpeleka mwanaye kwenye kituo cha kulelea watoto yatima pasipo kuwa na mawasiliano na hicho kituo mpaka mwanaye binafsi amefanya jitihada za kumtafuta mwanaye,lakin siyo mama kumfuata mwanaye japo alikuwa anafahamu yupo wapi.

Wamama / wababa wengi (siyo wote) wana sifa ya kuzaa tu, lakin wamepungukiwa na sifa ya ulezi, ambayo inahitaji sana kujitoa,kujituma ,upendo,uvumilivu. Huyu mama anasifa ya kuzaa tu,(ni mama mzazi tu).

Huyu mtoto wa kiume awe makini sana na tabia ya mzazi (mama)wake la sivyo atakuwa anamharibia mahusiano yake na kila atayetaka awe mpenzi/mchumba au mke. Afahamu na kutambua nafasi ya mpenzi/mke/mchumba wake ipo wapi na ya Mama yake ipo wapi. Mama atabaki kuwa mama hawezi kuwa mke hata siku moja ,vilevile Mke atabaki kuwa Mke hawezi kuwa Mama, japo anaweza kufanya majukumu kama ya mama.

JAPO NI KWELI KUWA WAZAZI WETU NI MUNGU WETU WA HAPA DUNIANI ,YATUPASA KUWAHESHIMU LAKIN PIA TUWE MAKIN SANA TABIA ZAO KATIKA MAHUSIANO YETU. WAZAZI WETU SIYO MALAIKA WANA MAPUNGUFU NA UDHAIFU WAO YATUPASA KUOMBA,KUPOKEA HEKIMA NA BUSARA KATIKA MAAMUZI YETU DHIDI YA WAZAZI WETU KATIKA MAISHA YETU YA KILA SIKU.
 
Mama wa aina hiyo mara nyingi wanasababisha watoto wao wa kiume wasiwe na furaha katika maisha ya kimapenzi,
manake muda mwingi atapenda kufanya yanayompendeza mama yake na siyo mke/mpenzi wake.
Huyo mwanaye awe makini sana na mama yake, siyo mama mwenye tabia nzuri. ila kwa vile ni mama yake aendelee kumheshimu lakin siyo kumkubalia kila kitu/jambo atakalo kwa 100%.
 
Kwa mama mwenye mapenzi angetakiwa amuulize maisha yake, tangu mdogo aliishije? ikiwezekana amwambie baba yake ni nani? mara ya kwanza kauliza huyu msichana ni nani akaambiwa ni mchumba wangu eti ahaha nilifikiri ni mke, kumbe bado hujamuona
 
huyo mama hana maadili kwa watoto wake afai na uenda alikuwa waluwalu kimtindo ni kumchukulia powa ila ni kuwa naye mbali kimtindo
 
Mimi nadahni kitu cha kuzingatia ni kwamba unaolewa kwa sababu umependwa na mtu mmoja; Mumeo. Usiwe na expectations kuubwa kuwa utapendwa na kila mtu wa familia ya mumeo. Kikubwa ni KUHESHIMIANA. Mimi siwezi sema mama mkwe ananipenda au ananichukia kwa sababu I dont care, ila simdharau namchukulia kama mama yangu na namshukuru saaana kunizalia kipenzi cha roho yangu. Ukianza kupeleleza sana kama unapendwa au unachukiwa ndo ugomvi unapoanza. Na kingine ni vema kumpa nafasi mama mkwe kuwa karibu na mwanae kwani wamama wengine wanahisi mke anawa replace na ndio hapo wanaanza kukufanya kama mke mwenza. SIoni wivu mume wangu akiwa karibu na mama yake kwani yeye ana nafasi yake na mimi nina nafasi yangu kwa jamaa na hawezi ni replace na mimi sina uwezo wa kum-replace.
 
Wazazi huwaonea WIVU sana watoto wao!

Baba umwonea WIVU mtoto wa KIKE & Mama umwonea WIVU mtoto wa KIUME! Ni maumbile tu . . .
 
Very true. Mimi nina mfano hai, baba yetu alikuwa hapendi kabisa tuolewe na alikuwa akilia siku ya harusi.
Ahamini kama tunakokwenda tutakuwa handled with care! Mother on the other hand huwa yuko critical kwa wakwe zake wa kike kuliko kwa wame zetu. Utasikia wale kwao sijuhi wana tabia hii ile. Ooh mama yake alikuwa anamcontrol baba yao na huyu mkwe atamcontrol mwanangu. Ni kweli wivu upo.

Wazazi huwaonea WIVU sana watoto wao!

Baba umwonea WIVU mtoto wa KIKE & Mama umwonea WIVU mtoto wa KIUME! Ni maumbile tu . . .
 
A lot of mothers are so jealousy against their sons's wives,they are just afraid that their sons are going to pay a lot of unnecessary attention to their wives and forget ev'thing about their mothers,they are trying to turn back the hand of time,the way they suffered while taking care of their lovely sons but the fortune falls to somebody else(the outsider) to enjoy the fruits that their sons toiled for.
 
Back
Top Bottom