Kwa nini JK Alishtuka na KUSHANGAA Sana PINDI Wabunge wa CHADEMA Walivyotoka Bungeni

kwa mara ya kwanza maggid ameongea bila kupendelea upande wowote, mwanzo mzuri wa mapinduzi ya kifikra
 
Siamini kama ni Maggid nimjuaye mimi. Binafsi nilishasusia kusoma mada zake ila leo nkaamua kupita kidogo. Objectivity must always be a key to any analyst!
 
Maggid yuko hivyo siku zote ila huwa mnataka asikosoe mliko nyie!! ndivyo alivyo acheni kujishaua humu!
 
Baada ya urais wake atakuja juta kwanini alimteua Salva Rweyemamu kufanya kazi nae Ikulu!!
 
Ndugu zangu,


Nilipita Dodoma siku mbili kabla ya JK kuhutubia Bunge. Nilizisikia, fununu za uwezekano wa kutokea kwa tukio lile.


Juzi limetokea, Wabunge wa CHADEMA kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, mbele ya Rais wa nchi, mbele ya wawakilishi wa Jumuiya ya Kimataifa, Mabalozi na wengineo. Si habari mpya sana, ilitarajiwa, kwa jinsi mambo yanavyokwenda sasa. Tutayaona mengi mengine.


Baada ya tukio lile nilitarajia Rais angesonga mbele na hotuba yake bila kugusia jambo lile. Hilo la mwisho lingewasumbua sana CHADEMA. Hapana, Rais akagusia tendo lile. Katika nchi, Rais ni mmoja, lakini, kazi ya Urais ni ya wengi. Najiuliza, je, wasaidizi wake hawajua kabla kwamba lililotokea lingeweza kutokea ? Kama walilijua, basi, wangemsaidia Mkuu wa Nchi na kama hawakulijua, nalo ni tatizo.


Nani mshindi?
Katika siasa, lililotokea Dodoma ni sehemu ya mapambano ya kisiasa katika mfumo wa vyama vingi. Chama tawala hakina sababu ya kuogopa. Kianze sasa kuyazoea mazingira haya mapya. Tunachokiona ni mchezo wa kisiasa ambao, kama mechi ya mpira, unahitaji team work na wachezaji mahiri katika kufanikisha ushindi. Maana, tukio lile, kwa wakati huu, limeliongezea ponti kadhaa za kisiasa CHADEMA.


Watanzania wamelifuatilia, Jumuiya ya Kimataifa imelifuatilia. Ajenda ya haja ya uwepo wa Katiba Mpya imeharakishwa kufikishwa kwa umma katika kasi ambayo haikufikiriwa. Watu wanajadili. Ni ajenda ya umma kwa sasa, CCM wakibaki nyuma, CHADEMA wataonekana kwa umma ndio wenye dhamira ya kweli ya kuwasaidia.

Naam. Katika dakika hizi za mchezo huu wa kisiasa, CCM imerudishwa nyuma kwenye lango lake, wanajihami. Na kuna wanaojiuliza nani mshindi? Mchezo bado unaendelea, tusubiri tuone!


Maggid
Arusha,
Novemba 20, 2010

mjengwa
mkuu leo umeongea ukweli mtupu NIMEIPENDA HIII!
 
I can't believe kama brother Mjengwa ni wewe uliyeongea hayo.
Kuwa neutral kama ulivyo leo bro.
safi sana mkuu.
 
Dole mwanangu huo ni uandishi usio na waa hongera uko on track sasa. Thanx for your contribution.
 
Maggid yuko hivyo siku zote ila huwa mnataka asikosoe mliko nyie!! ndivyo alivyo acheni kujishaua humu!

Atajibiwa tu kama ataleta habari zisishawishi na zenye skewed opinion. Hapa watu bongo zinachemka
 
Akisema mnachotaka anasifiwa kwamba anajua uandishi, yupo neutral; akiikosoa CHADEMA mnamwita msaliti, mnafiki, wakala wa mafisadi, nk. Hebu muwe na uwezo wa kutazama pande za shilingi.
 
Nani mshindi?
Katika siasa, lililotokea Dodoma ni sehemu ya mapambano ya kisiasa katika mfumo wa vyama vingi. Chama tawala hakina sababu ya kuogopa. Kianze sasa kuyazoea mazingira haya mapya. Tunachokiona ni mchezo wa kisiasa ambao, kama mechi ya mpira, unahitaji team work na wachezaji mahiri katika kufanikisha ushindi. Maana, tukio lile, kwa wakati huu, limeliongezea ponti kadhaa za kisiasa CHADEMA.


Watanzania wamelifuatilia, Jumuiya ya Kimataifa imelifuatilia. Ajenda ya haja ya uwepo wa Katiba Mpya imeharakishwa kufikishwa kwa umma katika kasi ambayo haikufikiriwa. Watu wanajadili. Ni ajenda ya umma kwa sasa, CCM wakibaki nyuma, CHADEMA wataonekana kwa umma ndio wenye dhamira ya kweli ya kuwasaidia.

Naam. Katika dakika hizi za mchezo huu wa kisiasa, CCM imerudishwa nyuma kwenye lango lake, wanajihami. Na kuna wanaojiuliza nani mshindi? Mchezo bado unaendelea, tusubiri tuone!


Maggid
Arusha,
Novemba 20, 2010

http://mjengwa.blogspot.com

Hongera maggid...........................at least now you have seen the light...................keep it up...............................
 
Akisema mnachotaka anasifiwa kwamba anajua uandishi, yupo neutral; akiikosoa CHADEMA mnamwita msaliti, mnafiki, wakala wa mafisadi, nk. Hebu muwe na uwezo wa kutazama pande za shilingi.

Akiongea upotoshaji lazima turuke nae, hapa fikra zinachemka. Hata Makamba anajua
 
Akisema mnachotaka anasifiwa kwamba anajua uandishi, yupo neutral; akiikosoa CHADEMA mnamwita msaliti, mnafiki, wakala wa mafisadi, nk. Hebu muwe na uwezo wa kutazama pande za shilingi.

sasa umezungumza nini wewe ulitaka akija na zile za hovyo tuziite keki pia sio? mtu husifiwa kwa mazuri,
na hukosolewa kwa mabaya
 
Nungunungu soi kweli watu wanampinga sio kwasababu anasema wasichotaka ila maandiko yake wakati mwengine hayako neutral mkuu ila leo hajaegemea upande wowote ameongea hali halisi
Akisema mnachotaka anasifiwa kwamba anajua uandishi, yupo neutral; akiikosoa CHADEMA mnamwita msaliti, mnafiki, wakala wa mafisadi, nk. Hebu muwe na uwezo wa kutazama pande za shilingi.
 
Naona Maggid safari ya Arusha imeenda sawia bila kuzongwa na Bi Mkora

Leo umepima mizani ya fikra sawia kabisa.
 
hata kama alikuwa na taarifa huwa wanadharau wakijua ni utani tu,kila kitu ni utani tu!

Kama makamba alisema watanzania watasahau na 2015 "watasahau ahaadi zetu na watatupa kura tena''

na jk alisema "watatoka watarudi" so hata kama alitaarifiwa nadhani alisema "wazushi tu wale hawawezi"
 
Back
Top Bottom