Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Napenda sana kusoma yale tunayoandika humu JF (Pamoja na mabandiko yangu) na wakati mwingine hujipa muda wa kutafakari kama kweli sisi kama ndiyo wahifadhi na wamiliki halali wa Lugha ya kiswahili tunaijua lugha yenyewe Ipasavyo.
Kuna toafuti kubwa sana kati ya Maneno, sentensi, na mtumizi sahihi ya Lugha. Kuna wakati unaweza kusoma bandiko la mtu hadi unafikia hitimisho kwamba inawezekana mwandishi wa bandiko hilo anadhani kila neno huunda sentesi na kila sentensi hutengeneza aya inayoeleweka.
Wakati mwingine kunakuwa na sentensi nyingi zinazounda aya isiyo na muunganiko, msawaziko, mtiririko wa wazo, uwiano wa hababri yenyewe na mwisho wa siku hata kusudio la mwandishi halieleweki. Ndani ya hayo yote mwandishi anatumbukiza maneno ya Kiingereza au ya mitaani bila ya kuonyesha kwamba maneno hayo si sehemu ya Lugha Rasmi iliyotumika kwenye uandishi wake.
Wakati mwingine hata matumizi sahihi ya herufi ua maneno hakuna. Nadhani ni wakati sasa hapa JF tuwe mfano wa matumizi bora ya Lugha yetu ya Kiswahili. Mdharau chake Mtumwa!!
Kuna toafuti kubwa sana kati ya Maneno, sentensi, na mtumizi sahihi ya Lugha. Kuna wakati unaweza kusoma bandiko la mtu hadi unafikia hitimisho kwamba inawezekana mwandishi wa bandiko hilo anadhani kila neno huunda sentesi na kila sentensi hutengeneza aya inayoeleweka.
Wakati mwingine kunakuwa na sentensi nyingi zinazounda aya isiyo na muunganiko, msawaziko, mtiririko wa wazo, uwiano wa hababri yenyewe na mwisho wa siku hata kusudio la mwandishi halieleweki. Ndani ya hayo yote mwandishi anatumbukiza maneno ya Kiingereza au ya mitaani bila ya kuonyesha kwamba maneno hayo si sehemu ya Lugha Rasmi iliyotumika kwenye uandishi wake.
Wakati mwingine hata matumizi sahihi ya herufi ua maneno hakuna. Nadhani ni wakati sasa hapa JF tuwe mfano wa matumizi bora ya Lugha yetu ya Kiswahili. Mdharau chake Mtumwa!!