Kwa nini hata wanawake hutumia majina ya viungo vyao nyeti kutukana!!

Gosbertgoodluck

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,855
401
Jamani kama kuna jambo linalonikera basi ni hii tabia ya kutumia majina ya viungo nyeti vya wanawake kutukana. Utakia mtu bila aibu mbele ya hadhara anamtukana mwenzie eti k.... mamako. Ajabu ni kwamba kuna wakati nilimsikia dada fulani akimtusi mvulana kwa tusi hilo hilo!! Hivi ni kwa nini tunawadharirisha mama zetu kiasi hiki!? Kwa kweli hii ni laana tena laana kubwa sana!
 


Ubarikiwe sana kwa kutuheshimu asubuhu yangu imekuwa njema



The Following User Says Thank You to Gosbertgoodluck For This Useful Post:

Dena Amsi (Today)​
 
Jamani kama kuna jambo linalonikera basi ni hii tabia ya kutumia majina ya viungo nyeti vya wanawake kutukana. Utakia mtu bila aibu mbele ya hadhara anamtukana mwenzie eti k.... mamako. Ajabu ni kwamba kuna wakati nilimsikia dada fulani akimtusi mvulana kwa tusi hilo hilo!! Hivi ni kwa nini tunawadharirisha mama zetu kiasi hiki!? Kwa kweli hii ni laana tena laana kubwa sana!

ni kweli inakera. nafikiri wanatumia viungo vya mama kutokana na sensitivity yake. ikitokea mwanamke na mwanaume wanatemea uchi, ni most likely kuwa kwa mwanamke watu watakuwa sensitive zaidi. ndio maana hata mwanaume atembee kifua na mapaja yote nje, hutasikia mtu anatia neno, ila iwe hivyo kwa mwanmke, utasikia hata watu wakisema "ana laana huyu"!

kwa kuwa tusi ni neno linalotamkwa kwa lengo la kuudhi au kuumiza roho, basi atukanaye huchgua hapo kwenye viungo vya wakina mama kwani ndipo sensitive zaidi na mtu yoyote anayejiheshimu na kumheshimu mama yake hataweza kuvumilia si tu kuona, kushika nk kiungo cha mama yake, bali hata kusikia kikitajwa. nafikiri hata daktari akijikuta anatakiwa kumtibu mama yake sehemu hizo, itabidi kutafuta msaada wa daktari mwingine

Glory to God
 
ni kweli inakera. nafikiri wanatumia viungo vya mama kutokana na sensitivity yake. ikitokea mwanamke na mwanaume wanatemea uchi, ni most likely kuwa kwa mwanamke watu watakuwa sensitive zaidi. ndio maana hata mwanaume atembee kifua na mapaja yote nje, hutasikia mtu anatia neno, ila iwe hivyo kwa mwanmke, utasikia hata watu wakisema "ana laana huyu"!

kwa kuwa tusi ni neno linalotamkwa kwa lengo la kuudhi au kuumiza roho, basi atukanaye huchgua hapo kwenye viungo vya wakina mama kwani ndipo sensitive zaidi na mtu yoyote anayejiheshimu na kumheshimu mama yake hataweza kuvumilia si tu kuona, kushika nk kiungo cha mama yake, bali hata kusikia kikitajwa. nafikiri hata daktari akijikuta anatakiwa kumtibu mama yake sehemu hizo, itabidi kutafuta msaada wa daktari mwingine

Glory to God

kwa hilo nakubaliana nawe, pili maumbile ya mwanamke na ya mwanaume hayafanani kwa mvuto! Tumeona maumbile mengi ya wanawake na wanaume ukitukanwa kwa kiungo cha mwanamke then uvute picha ilivyo lazma utaghadhibika tofauta na yakiume!
 
Hii ni dunia nzima huko america hutumika "Mother F*c*er" kwa wanaume na wanawake
 
kwa hilo nakubaliana nawe, pili maumbile ya mwanamke na ya mwanaume hayafanani kwa mvuto! Tumeona maumbile mengi ya wanawake na wanaume ukitukanwa kwa kiungo cha mwanamke then uvute picha ilivyo lazma utaghadhibika tofauta na yakiume!

Mimi bado nafikiri kuwa hiyo ni laana tu. Kimsingi, hakuna binadamu ambaye hajazaliwa na Mama. Hata Bwana na Mwokozi Yesu Kristo alizaliwa na Mama. Sasa inakuwaje lile eneo tulilopita sote wakati wa kuzaliwa litumike kama tusi la kumuudhi mwenzio!! Wanadamu tumefika mahali tunakejeli uumbaji mtakatifu wa Mungu!! Ndiyo maana magonjwa hatari yanaendelea kutugaragaza na tusipobadilika tutaangamia kabisa.
 
Mimi bado nafikiri kuwa hiyo ni laana tu. Kimsingi, hakuna binadamu ambaye hajazaliwa na Mama. Hata Bwana na Mwokozi Yesu Kristo alizaliwa na Mama. Sasa inakuwaje lile eneo tulilopita sote wakati wa kuzaliwa litumike kama tusi la kumuudhi mwenzio!! Wanadamu tumefika mahali tunakejeli uumbaji mtakatifu wa Mungu!! Ndiyo maana magonjwa hatari yanaendelea kutugaragaza na tusipobadilika tutaangamia kabisa.

hapo kwenye bold, nadhani unaikimbia homework yako kaka.

ni kweli inamkera kila mtu, kusema ni laana pekee, haitoshi, labda utuambie nani alimlaani nani hadi matusi yanayoaminika kuwa makali na ya kuudhi zaidi yakaelemea huko kwenye kiungo cha mama. hata kusema wote tulipita hapo haitoshi, najua wengine hasa waliozaliwa kwa mikasi ya upasuaji hawakupita. labda ungetumia maziwa ambayo wengi wamenyonya, ila pia wengine hasa waliopoteza wazazi wakati wa kuzalia hawakunyonya nk. lakini hata kwa hayo bado uatakuwa umekimbia homework yako. pia kumbuka kuwa tusi ni socially defined na linategemea hisia za atukanae na atukanwae

umedadisi sababu na inakuwaje na maoni ndio kama hivyo kuwa source ya haya matusi kumuelemea mama yaweza kutazamwa kiantropolojia zaidi na hapo hutakwepa suala la fermine sensitivity.

fikiria hivi, kati ya mwanume na mwanamke, nani sensitive zaidi ya mwingine, ukipata jibu mwnamke, jiulize tena hivi, katika mwili wa mwanamke ni sehemu gani sensitive kuliko nyingine, halafu jiulize tena katika wanawake wote nani sensitive zaidi kwako ukipata jibu kuwa ni mama yako, basi hutoshindwa kuelewa how sacred is this organ, hasa iliyo kwenye mwili wa mama yako na kwa nini ntu anayetaka kukudhi atakutukania hilo.

ni kama vile mtu anayekufuru dini fulani ili kuwaudhi waamini wa dini ile, hupenda zaidi kukufuru fundisho kuu la imani na sensitive ya dini nyingine na sio mafundisho madogo madogo

haya mambo yana mizizi yake katika saikolojia na hayakutokea kwa nasibu bali yametokana na mchakato wa kiantropolojia

nafikiri sasa umenielewa.

Glory to God
 
hapo kwenye bold, nadhani unaikimbia homework yako kaka.

ni kweli inamkera kila mtu, kusema ni laana pekee, haitoshi, labda utuambie nani alimlaani nani hadi matusi yanayoaminika kuwa makali na ya kuudhi zaidi yakaelemea huko kwenye kiungo cha mama. hata kusema wote tulipita hapo haitoshi, najua wengine hasa waliozaliwa kwa mikasi ya upasuaji hawakupita. labda ungetumia maziwa ambayo wengi wamenyonya, ila pia wengine hasa waliopoteza wazazi wakati wa kuzalia hawakunyonya nk. lakini hata kwa hayo bado uatakuwa umekimbia homework yako. pia kumbuka kuwa tusi ni socially defined na linategemea hisia za atukanae na atukanwae

umedadisi sababu na inakuwaje na maoni ndio kama hivyo kuwa source ya haya matusi kumuelemea mama yaweza kutazamwa kiantropolojia zaidi na hapo hutakwepa suala la fermine sensitivity.

fikiria hivi, kati ya mwanume na mwanamke, nani sensitive zaidi ya mwingine, ukipata jibu mwnamke, jiulize tena hivi, katika mwili wa mwanamke ni sehemu gani sensitive kuliko nyingine, halafu jiulize tena katika wanawake wote nani sensitive zaidi kwako ukipata jibu kuwa ni mama yako, basi hutoshindwa kuelewa how sacred is this organ, hasa iliyo kwenye mwili wa mama yako na kwa nini ntu anayetaka kukudhi atakutukania hilo.

ni kama vile mtu anayekufuru dini fulani ili kuwaudhi waamini wa dini ile, hupenda zaidi kukufuru fundisho kuu la imani na sensitive ya dini nyingine na sio mafundisho madogo madogo

haya mambo yana mizizi yake katika saikolojia na hayakutokea kwa nasibu bali yametokana na mchakato wa kiantropolojia

nafikiri sasa umenielewa.

Glory to God

Uchambuzi murua. Bila shaka umeeleweka tena vizuri sana.
 
Nikimnukuu Notorius BIG akilaumu akisema "Shit my mama got kid in the west" hii nayo ilitokana na mama yake kutumia hicho kiungo.
 
ni kweli inakera. nafikiri wanatumia viungo vya mama kutokana na sensitivity yake. ikitokea mwanamke na mwanaume wanatemea uchi, ni most likely kuwa kwa mwanamke watu watakuwa sensitive zaidi. ndio maana hata mwanaume atembee kifua na mapaja yote nje, hutasikia mtu anatia neno, ila iwe hivyo kwa mwanmke, utasikia hata watu wakisema "ana laana huyu"!

kwa kuwa tusi ni neno linalotamkwa kwa lengo la kuudhi au kuumiza roho, basi atukanaye huchgua hapo kwenye viungo vya wakina mama kwani ndipo sensitive zaidi na mtu yoyote anayejiheshimu na kumheshimu mama yake hataweza kuvumilia si tu kuona, kushika nk kiungo cha mama yake, bali hata kusikia kikitajwa. nafikiri hata daktari akijikuta anatakiwa kumtibu mama yake sehemu hizo, itabidi kutafuta msaada wa daktari mwingine

Glory to God

Asilimia kubwa ya Binadamu wana utamadumi wa kuwapenda na kuwaheshimu Mama zao zaidi kuliko Baba zao kwa kuwa huwa kuna true love kati ya mama na mwana pasipokujali jinsia. Ili umkere zaidi adui yako ndo maana watu hu-opt kumtukana mama wa adui ili achukie zaidi.
Ukichunguza utagundua kwamba hata reaction ya mtu aliye karibu zaidi na mama yake anapotukanwa ni tofauti na ambaye hakupata bahati ya kuwa karibu na mama katika kukua kwake. Huyu aliyejaaliwa kuwa karibu na mama anaweza hata kukuua ukimtukania mama.
 
kwani viungo hivyo vinapotumiwa kusifia haikeri?
msisahau watu hutumia viungo hivyo hivyo kusifia
 
Jamani kama kuna jambo linalonikera basi ni hii tabia ya kutumia majina ya viungo nyeti vya wanawake kutukana. Utakia mtu bila aibu mbele ya hadhara anamtukana mwenzie eti k.... mamako. Ajabu ni kwamba kuna wakati nilimsikia dada fulani akimtusi mvulana kwa tusi hilo hilo!! Hivi ni kwa nini tunawadharirisha mama zetu kiasi hiki!? Kwa kweli hii ni laana tena laana kubwa sana!

Ku.... mamake walakhi mijitu inayopenda kutukania viungo vya mama zetu huwa inaniudhi kweli yaaani basi tu nashindwa uwezo wa kuiangamiza ipotee kwenye uso wa dunia hii.
 
Back
Top Bottom