Kwa nini CHADEMA inashindwa kuelewa kwamba CCM ndio wabaya???

Masauni

JF-Expert Member
Aug 15, 2010
386
58
Tumekuwa tukisikia kwenye vyombo vya habari kuhusu migogoro inayoikumba Chadema kwa sasa, baadhi ya viongozi wa chadema wameamua kuhama Chama!! na yote hii ni mbinu ya CCM kuvunja nguvu za Chadema, na kwa kiasi fulani wameshazivunja!! Kibaya zaidi Chadema wamekuwa wakitoa matamko ya ajabu ajabu tu kwenye vyombo vya habari, mara Shibuda na wenje, mara Zito na Mbowe ilimladi ni vurugu tu. Nitoe ushauri kwa Chadema Msiongelee migogoro yenu kwenye vyombo vya habari, tatueni matatizo kimya kimya, fanyeni siri kubwa. CCM wanamigogoro mingi sana lakini wanajitahidi kutoongelea kwenye vyombo vya habari hata vyombo vya habari vikijitahidi kuibua migogoro yao bado watakaa kimya. Chanzo cha matatizo sio Zito, huyo kijana anatumiwa tu na CCM. solution sio kumu attack ZITO, dawa ni kuwa na strategy za kuwa attack CCM na Vibaraka vyake kina CUF, NCCR,TLP na mapesa. Hakikisheni CCM haipenyezi mkono wake ndani ya CHADEMA. Msipo mtambua adui yenu ni nani, huyo adui ana hasira za kujeruhiwa katika uchaguzi atawamaliza tu. Leo anamtumia zito, kesho mnyika keshokutwa ataanza kuwatumia dada zetu wa viti maaluma ambao nadhani hao ndo rahisi kabisa kutumiwa. NAOMBA KUWASILISHA
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom