Otorong'ong'o
JF-Expert Member
- Aug 17, 2011
- 37,440
- 25,582
Habari zenu wadau wa jf? nimekuwa nikijiuliza siku zote why arusha? arusha ndo mji unaojulikana kama tha CAPITAL SAFARI CITY OF EAST AFRICA, THE GENIVA OF AFRICA, na pia ndo mji wa KITALII TANZANIA. pia ndo mji wenye agencies nyingi za kimataifa moja wapo ni ICTR, mahakama inayoshughulikia haki za binadamu ndo makao makuu hapa arusha.Napia tumeshuhudia mikutano mingi ya kimataifa ikifanyikia Arusha. Kwa maana nyingine Arusha ni kama kioo kwa taifa, Lakini cha kushangaza ni kwamba hili jiji halina bara bara. si bara bara za ndani ya jiji wala si bara bara za nje. Miundo mbinu ni mibovu sijapata kuona, vumbi kila mahali. Arusha kuna msongamano mkubwa wa magari lakini ni kama serikali hailioni hili halafu tunauita ati ni mji wa kitalii? Au ndo magamba wameamua kutukomoa kwa kumcgagua mbunge Lema, au ndo wanatukomoa kwa kuichagua CDM kama chama tawala Arusha? hii sarikali inaboa kweli jamani>