Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Ninauliza hivyo cause, wakati nilipokuwa katika mchakato wa umiliki wa silaha, niliitwa katika kamati ambayo ilijumuisha mwenyekiti wa mtaa na wajumbe wapatao saba, Swali la kwanza nililoulizwa na kamati lilikuwa..Wazo la umiliki wa silaha umelipata wapi?? umepewa ushauri na mkeo au ni wazo lako mwenyewe? Nikajibu ni wazo langu mwenyewe, yakafatia maswali mengine.... Kikao kilipoisha mwenyekiti wa mtaa akaniambia kuwa nimejibu vizuri sana, na laiti ningesema nimepewa ushauri na mke na nisingepata kamwe leseni ya silaha.
Tukiacha hayo...pia nimewahi kumsikia mara nyingi sana Baba wa Taifa akikataza waTz wasiwe ni watu wa kufata ushauri wa wake zao... na kuna kipindi alimkaripia
sana rais wa
awamu ya pili (Ali Hassan Mwinyi) kuwa anaendesha nchi kwa kufata ushauri wa Mke!!
Sasa jamani tusipofata ushauri wa mke...tufate ushauri wa nani?? Na inasemekana pia
Katika kila mafanikio ya Mwanamme, basi kuna mwanamke nyuma yake
Tukiacha hayo...pia nimewahi kumsikia mara nyingi sana Baba wa Taifa akikataza waTz wasiwe ni watu wa kufata ushauri wa wake zao... na kuna kipindi alimkaripia
sana rais wa
awamu ya pili (Ali Hassan Mwinyi) kuwa anaendesha nchi kwa kufata ushauri wa Mke!!
Sasa jamani tusipofata ushauri wa mke...tufate ushauri wa nani?? Na inasemekana pia
Katika kila mafanikio ya Mwanamme, basi kuna mwanamke nyuma yake