Kwa NEC hii mpya, CCM inakwenda kufa - Dr. Slaa

Hivi Fisadi kiwembe(Slaa) kazaliwa wakati gani? Kabla ya Uhuru ama baada ya Uhuru. Manake kuna kauli kuwa waliozaliwa kabla ya Uhuru hawana tena nafasi katika Uongozi nchini hapa, kwa mjibu wa Mbunge mmoja CDM.
 
Slaa afikirie kwanza Chadema kinavyomfia kwa ubinafsi na roho ndogo yake!!
 
Huyu mzee hana sera ingine zaidi ya ufisadi? analia sana.....aseme mengine...hawa ni watuhumiwa sio mafisadi.....tumechoshwa na sera zake za ufisadi ufisadi....
Wewe hufahamu kuwa ufisadi ndio namba one ya kuuwa uchumi kwenye nchi nyingi za Africa? Ona Botswana ambapo ufisadi ni wa kunusa; wanavyoendelea; Angola wamepigana miaka yote hiyo; lakini sasa hatuwafikii hata kidogo. Yamkini wewe ni mteja wao ndio maana unaona vibaya mtu anayeshupalia ufisadi. Pole
 
Nadhani sasa Dr. Slaa anahitaji kupatiwa msaada wa kuwekewa "political advisor" atakayemshauri aseme nini na wapi!.

Siku zote nawashauri Chadema tena ushauri wa bure kuwa by 2015, "hit single" ya "ufisadi" itakuwa imedrop sana kwenye "top of the charts" hivyo sasa lazima watafute single nyingine waanze kuipandisha kwenye chart ili by 2015 ndio i hit on top of the charts!.

Nimewashauri Chadema waachane kabisa na CCM!. in 2015 CCM matters very little!, wao waweke concentrations zao where it matters most!.
 
Kikwete kamtengenezea njia Lowassa awe rais 2015 na Chenge awe waziri mkuu
Mkuu Mikela, mimi ni mtetezi mkubwa wa EL ila hii move kwenye NEC, nina wasiwasi na JK, he might be playing the Greeks way!. " I Fear the Greeks, especially when they bring gifts!".
 
Mimi nadhan Slaa amesukumwa na mihemko ya kisiasa tu. CCM na ujambazi , uhuni, ubakaji, udhulumaji na uchafu wao, bado ni MBUYU mzito kuukata. Huo ndio ukweli
Mkuu Mzito Kabwela, huu ndio ukweli mchungu!. CCM ni Mbuyu kongwe, japo unaoza from inside huku ukichipua matawi mapya outside!. Kuna nondo nimeinasa mahali, 2015 ni CCM tena!.
 
siyo huyo mzee tu ata mimi nauchukia ufisadi kuliko kitu chochote dunia. kwahiyo anachofanya huyo mzee hakosei, ni watanzania wengi sana tunalia kila siku kuhusu ufisadi na hicho ndiyo pekee kitakacho iuwa CCM. wakiiba kura kama kawaida yao tuna wapiga mawe kama vibaka. tumeisha wachoka sana
Kwa mnaodhania CCM itakufa natural death kwa ufisadi, bi sawa na fisi anayemfuatilia binadamu akijiaminisha mikono imelegea na karibu itaanguka!.
 
CCM is dead..CDM wanaweza shinda 2015 CCM wakisimamisha yeyote anayeitwa Fisadi kwa kunyooshea mafisadi kidole tuu biashara inaisha.
 
Wakuu,
Ni aibu kuona chama kinaendeshwa bila nidhamu. Na kama nidhamu ipo, basi wale ambao hawana nidhamu ndani ya chama wawajibishwe. Bila hiyvo, uongozi wa CCM wa Taifa lazima uwajibishwe kwa kutoleta nidhamu sio ndani ya Chama tu, bali hata serikali inayoshikilia na kuendesha. Kwa mlolongo huo. Kwani bila hiyo nidhamu-inaacha mianya mingi amabko ufisadi unaendelea.

Kuna umuhimu wa Mtanzania/Mwananchi ambae ndie amemweka CCM madarakani, awajibike kwa kudai nidhamu. Na hili laweza kufanyika wakati wa Uchaguzi ujao na sio kwa njia nyingine kama Chama cha CCM hakiwezi kujiwajibisha chenyewe.

Kuna mfano mzuri ambao umetokea hivi karibuni huko Uchina-wamebadilika.....http://www.nytimes.com/2012/09/29/w...om-chinas-communist-party.html?ref=world&_r=0

Kuhusu DK. Slaa, sioni kama kuna jipya: Wananchi wengi wanaliona, wanasema, lakini hawana fursa kama yake kuweka hadharani na kunukuliwa na magazeti.

haya ni maoni yangu.
 
Hii ni kawaida ya maumbile kuwa kadiri unavyozeeka uwezo wako wa kufikiria unarudi chini. Sasa jamii inazidi kuona hakuna sababu ya kuweka madarakani watu kama Slaa ambaye tayari uwezo wake umeanza kuwa wa kizee. Ccm inamhusu nini,yeye anatakiwa azungumzie cdu yake. Hii inazidi kunipa uhakika kuwa Zitto will be the best candidate for presidency 2015
 
Dr Slaa hajakaa kutafakari mustakabali wa CDM kwani chenyewe kinachungulia kaburi.
 
CDM acheni harakati mfanye siasa kila siku ni mafisadi tuuuuuuuuuu, mkipewa nchi mkathibiti mafisadi then? Elezeni mipango ya kuendeleleza nchi na kuhudumia wananchi. Kushika dola sio mchezo huwezi kwenda pale na agenda moja tu ya kudhibiti ufisadi.
 
Gamba at work!... Kazana uongezewe posho a Lumumba!

ID zetu zinatusaidia.....huu mhemko wa kushabikia upinzani wakati hujui manufaa yake ...People Power People Power ukimuuliza kwanini sababu anazo toa hazielewi....negative hata kwa vitu vilioko wazi.....mahaba niue....haya utapewa udiwani wa kuteuliwa chadema wakishika 2025.
 
Back
Top Bottom