Ushabiki wa vyama hauna maana ndugu zangu.tufungue macho yetu, masikio yetu na akili zetu tuangalie mambo ya msingi yanayogusa taifa letu kwa ujumla wake.
Angalia rasilimali zilizoko nchini zimetumika kwa kiasi gani na zimemnufaisha nani?
Angalia usimamizi wa sera na mipango ya serikali iliyoko madarakani sasa na utekelezaji wa ahadi tunazopewa kila siku zimetufikisha wapi?
Karibu miaka 50 ya uhuru bado tunadanganyika, hatujiamini, hatujapata elimu ya kutosha na fikra zetu kweli bado ni butu kiasi cha kushindwa kuingia mikataba yenye tija kwa taifa letu au tunafanywa mazoba?
TULIWAVUMBIKA CCM WAKIWA WABICHI TUKAJISAHAU WAKAIVA KUPITILIZA SASA TUKIJIFANYA MABINGWA WA KUVUMBIKA WATATUOZEA MIKONONI TUNUKE WOTE.MWENYE AKILI HAWEZI KUFANYA HIVYO.
Nani leo hii anaweza kuniambia serikali ya kikwete imewafanya nini mafisadi waliofichuliwa na bunge, kama si ubabaishaji ili mradi siku ziende na kiini macho cha kesi mahakamani ziishie kiholela.hivi kweli mbona kibaka mtaani akiiba haambiwi arudishe na iwe ndio amesalimika? Iko wapi kesi ya zombe aliyoingia nayo kikwete kwa mbwembwe tukapambiwa kwenye magazeti kuwa ni jambazi na sasa anakula good time. Hivi kweli anayeiba mabilioni ya fedha na kulisababishia taifa hasara ndiye wa kufungwa miaka miwili tu? Huyu si ni sawa na mbakaji wa uchumi wa nchi? Tunakwenda wapi jamani na udanganyifu huu? Taifa hili lililojengewa misingi mizuri na j.k.nyerere ya kuchukia rushwa, misingi ya kuheshimiana na misingi ya kutokuwa na ubaguzi wa aina yoyote,taifa lenye amani inayoridhisha inashangaza kuendelea kuwa masikini ilihali tuna rasilimali za kutosha.
HAPA SASA NAKUMBUKA STATEMENT YA BALOZI WA MAREKANI HAPA NCHINI ALIPOSEMA TANZANIA ISIPOJICHUNGUZA KWA NINI HAIENDELEI WAKATI INAPATA MISAADA MINGI NA INA RASILIMALI NYINGI KULIKO NCHI NYINGI ZA AFRIKA HAITAKAA IENDELEE DAIMA. AKUTUKANAYE HAKUCHAGULII TUSI.KWA MTU MWENYE AKILI NA BUSARA HILI NI TUSI.
Unajua mimi siamini kabisa kuwa akili zetu zimelala kiasi kwamba tunashindwa kutambua ya kuwa kuna wazembe wengi sana huko serikalini, wanaofanya kazi ilimradi wapate mshahara, hawatumii profession zao kutatua challenges (changamoto) zinazolikabili taifa.hawa hawatufai jamani.lets be serious ndugu zangu black is black and white is white,lets call spade, a spade ndipo tunaweza kuona mabadiliko. Ccm inafahamu kuwa katika taasisi za elimu ya juu, wanafahamu nini wanaambiwa na wanajua kutafakari. Wanapodanganywa wanajua tumedanganywa na penye ukweli wanajua huu ni ukweli, halikadhalika maeneo ya mjini.hawana mtaji huko. Wanakimbilia vijijini na ngoma zao wakapate wa kuwadanganya. Kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania imeishia wapi? Mimi sihoji watanzania kupewa maisha bora ila ni mazingira gani watanzania wamewekewa ili wajitafutie maisha bora? Yako wapi?
My friends, taifa hili linahitaji ukombozi wa kweli.utakaotutoa kwenye mikataba mibovu isiyokuwa na tija kwa taifa, utakaowakurupua mafisadi wote huko serikalini, utakaopunguza matumizi makubwa ya serikali na kuelekeza fedha hizo katika maendeleo, ukombozi wenye kutoa dira kuu ya taifa na si kushabikia uanachama. Wewe unayesoma ujumbe huu una nafasi yako ya kuleta mabadiliko. Jiulize umelifanyia nini taifa lako la tanzania? Hata kwa kulichagulia kiongozi bora tu anayeonesha uhai katika kupambana kwa vitendo na matatizo mengi ya nchi yetu. Lets Wake up and dare for change!!
Angalia rasilimali zilizoko nchini zimetumika kwa kiasi gani na zimemnufaisha nani?
Angalia usimamizi wa sera na mipango ya serikali iliyoko madarakani sasa na utekelezaji wa ahadi tunazopewa kila siku zimetufikisha wapi?
Karibu miaka 50 ya uhuru bado tunadanganyika, hatujiamini, hatujapata elimu ya kutosha na fikra zetu kweli bado ni butu kiasi cha kushindwa kuingia mikataba yenye tija kwa taifa letu au tunafanywa mazoba?
TULIWAVUMBIKA CCM WAKIWA WABICHI TUKAJISAHAU WAKAIVA KUPITILIZA SASA TUKIJIFANYA MABINGWA WA KUVUMBIKA WATATUOZEA MIKONONI TUNUKE WOTE.MWENYE AKILI HAWEZI KUFANYA HIVYO.
Nani leo hii anaweza kuniambia serikali ya kikwete imewafanya nini mafisadi waliofichuliwa na bunge, kama si ubabaishaji ili mradi siku ziende na kiini macho cha kesi mahakamani ziishie kiholela.hivi kweli mbona kibaka mtaani akiiba haambiwi arudishe na iwe ndio amesalimika? Iko wapi kesi ya zombe aliyoingia nayo kikwete kwa mbwembwe tukapambiwa kwenye magazeti kuwa ni jambazi na sasa anakula good time. Hivi kweli anayeiba mabilioni ya fedha na kulisababishia taifa hasara ndiye wa kufungwa miaka miwili tu? Huyu si ni sawa na mbakaji wa uchumi wa nchi? Tunakwenda wapi jamani na udanganyifu huu? Taifa hili lililojengewa misingi mizuri na j.k.nyerere ya kuchukia rushwa, misingi ya kuheshimiana na misingi ya kutokuwa na ubaguzi wa aina yoyote,taifa lenye amani inayoridhisha inashangaza kuendelea kuwa masikini ilihali tuna rasilimali za kutosha.
HAPA SASA NAKUMBUKA STATEMENT YA BALOZI WA MAREKANI HAPA NCHINI ALIPOSEMA TANZANIA ISIPOJICHUNGUZA KWA NINI HAIENDELEI WAKATI INAPATA MISAADA MINGI NA INA RASILIMALI NYINGI KULIKO NCHI NYINGI ZA AFRIKA HAITAKAA IENDELEE DAIMA. AKUTUKANAYE HAKUCHAGULII TUSI.KWA MTU MWENYE AKILI NA BUSARA HILI NI TUSI.
Unajua mimi siamini kabisa kuwa akili zetu zimelala kiasi kwamba tunashindwa kutambua ya kuwa kuna wazembe wengi sana huko serikalini, wanaofanya kazi ilimradi wapate mshahara, hawatumii profession zao kutatua challenges (changamoto) zinazolikabili taifa.hawa hawatufai jamani.lets be serious ndugu zangu black is black and white is white,lets call spade, a spade ndipo tunaweza kuona mabadiliko. Ccm inafahamu kuwa katika taasisi za elimu ya juu, wanafahamu nini wanaambiwa na wanajua kutafakari. Wanapodanganywa wanajua tumedanganywa na penye ukweli wanajua huu ni ukweli, halikadhalika maeneo ya mjini.hawana mtaji huko. Wanakimbilia vijijini na ngoma zao wakapate wa kuwadanganya. Kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania imeishia wapi? Mimi sihoji watanzania kupewa maisha bora ila ni mazingira gani watanzania wamewekewa ili wajitafutie maisha bora? Yako wapi?
My friends, taifa hili linahitaji ukombozi wa kweli.utakaotutoa kwenye mikataba mibovu isiyokuwa na tija kwa taifa, utakaowakurupua mafisadi wote huko serikalini, utakaopunguza matumizi makubwa ya serikali na kuelekeza fedha hizo katika maendeleo, ukombozi wenye kutoa dira kuu ya taifa na si kushabikia uanachama. Wewe unayesoma ujumbe huu una nafasi yako ya kuleta mabadiliko. Jiulize umelifanyia nini taifa lako la tanzania? Hata kwa kulichagulia kiongozi bora tu anayeonesha uhai katika kupambana kwa vitendo na matatizo mengi ya nchi yetu. Lets Wake up and dare for change!!