Kwa mawazo yako una ipa miaka mingapi CCM

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Kila mmoja ana fikra na muono kwa jinsi hisia za siasa miongoni mwa wananchi wa Tanzania zinavyopanda chati,tuweke tofauti na jazba pembeni,ili kila mmoja wetu aweze kutoa maoni yake ,unafikiria CCM inaweza kukaa madarakani kwa muda gani(Mungu anajua zaidi)Lakini na sisi binadamu tunaweza kukisia kutokana na hali inavyokwenda.

Kwa upande wangu sioni ukaribu wa kuiondoa CCM madarakani kipimo nilichokitumia ni chaguzi zilizopita zinaonyesha vigogo hawawezi kuondolewa kwa kura za upinzani hata siku moja ,CCM imejikita kila sehemu na uchaguzi unapochanganyika na upinzani kuwania madaraka ya kiserikali(Ubunge) huwepo mipango maalumu ambayo upinzani hawana ubavu nayo na kuifanya CCM iondoke na ubingwa ,na CCM wanapokuwa katika ugombeaji huo hupima nguvu zao na huongezwa za ziada pale wanapoona pana shaka na ushindi.

Ninachotaka kukisema ni hizi nguvu za ziada ambazo huwapeperusha wapinzani na wasijue la kufanya,kwa kutoa mfano hai ambao umetumika mara zaidi ya Tatu ni Uchaguzi wa wapemba huko CCM inatumia nguvu hizi kwa dhahiri kabisa(Polisi,jeshi,usalama wa Taifa) na ndio mpaka leo inaendelea kuwepo ,sasa kwa hali inavyokwenda hapa Bongo imefikia wakati nguvu hizo nazo kutumika kikamilifu kama kule visiwani au zaidi ,ndipo nikasema sitegemei ukaribu wa kuing'oa CCMmadarakani kwa sera hizi za kutaja ufisadi na kuwataja mafisadi ,hizi sera hazina mshiko wa kuiondoa CCM madarakani.

Napenda wapinzani mulielewe hili wala halina mabadala,mtasomba wapiga kura wengi.au kwa lugha sanifu mtawateka wengi tu,lakini CCM haishughuliki kwa kuona wamepoteza wapiga kura na kuwasababishia kupoteza kiti,wana uhakika wa kujinyakulia kwa kutumia vyombo vilivyodhibitiwa na serikali yao,CCM haitakuwa tayari kuona wanaipoteza serikali wakati kila kitu wancho na sababu wanazo,hivyo mtasubiri sana.
 
Kama hawataanza kuwashughulikia mafisadi na kurekebisha mikataba mibovu hawawezi kukaa zaidi ya miaka saba (7). Inaweza kuwa chini ya hapo na si vinginevyo.
 
unanichekesha sana hapo ^^ ! kwani imetumia muda kuwa madarakani ? times that number by two labda ndio kunaweza kukawa na uwezo baada ya miaka hiyo kuondoka, LABDA !!

lakini tena kwa kampeni hizi chafu, i guess not any time soon !
 
Kama hawataanza kuwashughulikia mafisadi na kurekebisha mikataba mibovu hawawezi kukaa zaidi ya miaka saba (7). Inaweza kuwa chini ya hapo na si vinginevyo.

Nani awashugulikie mafisadi ?? Halafu ndani ya miaka saba mbona itakuwa kurasa imeshageuka na watu wanasoma mbele,Usitegemee kama CCM watashughulikia fujo za wapinzani juu ya kuliwa na kutoweka mali za Taifa kwani kila mmoja wao ana chota kivyakevyake sidhani kama iko siku mwenzetu ataweza kutunyooshea kidole kusema yule ndie na yule sie na atakae fikia hapo huyo si mwenzetu tena.
Mfano hai ni ule uliopita wa vigogo kuhusika na biashara ya unga hii skendo haipo tena au mmeisikia kutajwa,Muungwana alipelekewa ,polisi wanayo .sasa mbona hakuna wa kuwauliza wamefika nayo wapi majina ya vigogo si kila mkiuliza mnaambiwa uchunguzi unafanywa sasa baada ya miaka saba ndio unapata jibu.Na yako mambo mengi na haya sasa tutakwenda nayo kwa ahadi za uchunguzi unafanywa,kama uchunguzi unafanywa inabidi wahusika waliotajwa wawekwe ndani ili uchunguzi ufanywe wasije wakaharibu huo uchunguzi wenyewe kwa kulishia.Lakini mambo haya wamo wenzetu hivyo sera ya kulindana hapa ndio inapochezwa na miaka inakatika,si leo wala kesho tusitegemee kuanguka kwa CCM,nasema hiyo ni ndoto na wapinzani kucheza na wananchi.
 
...just remember Mrema alivyowamwaga Temeke kwenye ule uchaguzi maalum huku CCM yote ilihamia kupiga kampeni huko na mamilioni yote hayakusaidia...hamna lolote mnashinda vijijini tuu na kutumia wizi mtupu mtaondoka soon
 
Hata Ian Smith wakati wa ukombozi Zimbabwe alisema baada ya miaka 100 ndio waafrika wataongoza lakini ni yeye aliyeachia madaraka. Funny eh! Huu ni mfano hai, wanna say something?
 
Ni kweli baada ya miaka mia maana hivi sasa hakuna Muafrika anaeongoza isipokuwa kuna watawala na watawaliwa,CCM ni Mfalme wa Nchi hii na ndani yake mna wafalme wadogo wadogo wengi tu,au unataka kusema balozi wa nyumba kumi hatesi,ipo kazi ndugu zanguni mtaimba na kucheza sana,CCM itapigana kufa kupona lakini roho yake ni ya Paka na kwa hizi tararira za upotoshaji wa wananchi hazitafua dafu,na ukweli mkitaka msitake hamfiki nazo mbali,jitahidini kuzitetea kwa nguvu zenu zote,kila kona na kila sehemu mtawekwa sawa,hao mabalozi wamekuja juu ni juzi juzi tu wameekwa kitako wakapewa maneno yao,kama mtawasikia tena,sidhani.
 
kipi kilichopotoshwa kwa wananchi?au nawe ushapewa fungu kutetea ufisadi kwenye forum?
 
Mwiba,
Unataka kutuambia kwamba hizo mbinu chafu ndizo mnazotumia kushinda?

Kama ndivyo, ina maana wananchi walishawachoka lakini mnakwiba kura? na kama hivyo ndivyo je unadhani mbinu hizo zitadumu milele? (Njia ya muongo siku zote ni fupi)

Ni matarajio yangu kwamba kama michezo michafu inatumika basi kiama cha ccm kiko karibu sana. Rejea hotuba ya Lowassa Arusha.
 
Mwiba,
Unataka kutuambia kwamba hizo mbinu chafu ndizo mnazotumia kushinda?

Kama ndivyo, ina maana wananchi walishawachoka lakini mnakwiba kura? na kama hivyo ndivyo je unadhani mbinu hizo zitadumu milele? (Njia ya muongo siku zote ni fupi)

Ni matarajio yangu kwamba kama michezo michafu inatumika basi kiama cha ccm kiko karibu sana. Rejea hotuba ya Lowassa Arusha.

Hakuna kitu mbinu chafu katika biashara ya siasa na ndio ikaitwa siasa,tafuta kamusi ya kiswahili utazame maana ya neno siasa,vyama vya upinzani vimeshindwa kulielewa neno hili na ndio mnalalamika kwamba kuna mchezo mchafu unaochezwa na CCM ndiomkawa mnashindwa vibaya sana ,jamani CCM inafanya siasa na kwenye siasa kila kitu kinakubalika,hivyo ushindi wa CCM unatumia mbinu kali na za kisasa katika kujipatia ushindi ukiwemo wa che.Naona siasa itawashinda wapinzani na kusambaratika,hizi ni mbinu ambazo kama hazitadumu milele basi zitazuka mpya,msitegemee kabisa yaani hata likitokea tetemeko la ardhi na vinara na wapambe wao wa ccm wakafa basi watazuka wengine watakao isimamisha bendera ya CCM na kuendelea kutesa kwa awamu kama walivyo hawa waliopo sasa ambao mwisho wao ni kufa mmoja mmoja huku wengine wakizaliwa nahisi kama bwana mungu ameibariki Tanzania kutawaliwa na CCM mpaka kiyama sasa nyie mnavyoonekana mnashindana na maamuzi ya mungu kitu ambacho kwa waumini wanajua kabisa haiwezekani kumshinda mungu si mlisikia kuwa hata kikwete ni chaguo la mungu alilowachagulia CCM na ukweli alishinda kwa ushindi wa kishindo tokea mwanzo.
 
Ukweli ni kwamba CCM itaendelea kuwepo madarakani kwa muda mrefu kutokana umahiri wa kujibadilisha na kuendana na hali halisi.
Alikuwepo Mwenyekiti Alhaj Mwinyi na safu kamambe kabisa ya vigogo. Akaondoka na baadhi wakaondoka.
Akaja Mwenyekiti Mkapa na safu yake, naye kaondoka.
Sasa amekuja Mwenyekiti Kikwete naye anapanga safu yake, wakati wake ukifika naye ataondoka.
Tujiulize wanaoshindana na CCM wamejibadilisha mara ngapi?
Hivi kweli mko kwenye mbio za vijiti, timu moja inapokezana, lakini timu zingine zimeng'ang'ania mkimbiaji huyohuyo mmoja, siatachoka?
Kwa mantiki hii basi vyama vya kupinga na CCM vijibadilishe vichukue sura za kitaifa zaidi na visiendelee kuwa taasisi za binafsi au wateule wachache wanaotaka madaraka na wala si kuiletea nchi hii maendeleo.
 
Mimi kutokana na jinsi ninavyoona nimeangaia mambo mawili

Watu waliowengi wamechoka CCM lakini wakichoka wanazua vioja, tatizo kubwa tulionalo pamoja hata na wasomi wakichukia hata mambo ya kujiandikisha kupiga kura hawafanyi hivyo.

CCM itaondoka tu ktk kipindi hata cha miaka 3 ijayo lakini watu wakielimishwa nini maana ya Tanzania utaifa, watu wakiwa na uzalendo hata wana CCM waliowengi watasaidia kuleta mapinduzi ya kweli ndani ya chama chao.

Lakini bila kuwa na elimu nzuri ya nini maana ya kupiga kura na nini maaana ya uzalendo mkuu sahau, hata wasomi wa nchi yetu wamekata tamaa na kuachana na mambo ya siasa sana sana kwa mfano vijana wanatafuta mahala pa kukimbilia hili wagange njaa.

Pili CCM inaweza kuondoka kwa kutumia hila mbali mbali kama zile mafisadi wanazotumia hizi ndizo mimi nategemea ziokoe nchi ya watanzania.

Ukiangalia wenzetu wa kenya walivyoteketeza kanu sina uhakika kama watanzania pamoja na chuki iliyojengeka kuhusu CCM kama tutaleta ya wakenya siku za karibuni.

Mimi, wewe hapo tupo tukisuburi mbowe, Lipumba na Mrema eti ndiyo walete mapinduzi ya kweli Tanzania na kuwaachia walioweka mirija wadhalilishe nchi yetu.KUNA MTU MMOJA AMESEMA KWAMBA KUMSEMA MTU FULANI NI KUMTUKANA HATA YEYE. MTU YEYOTE ambaye hataki kujiheshimu hataheshimiwa kamwe.

Sana sana watu wengi wamechoka na UFISADI wa waziwazi(makusudi) bila hatua zozote kinachohitajika ni kuwasha kiberiti tu na kuna siku kitawaka tu.
 
Hoja ya ufisadi haina nguvu, kwani katika list of shame hakuwataja wapinzani ambao ni mafisadi. Sasa kama wewe ni fisadi na hujajitaja kwenye hiyo list na unajulikana kabisaunadhani hii hoja itakwenda wapi? halafu ka-hoka kenyewe ni very light katika ulingo wa siasa. Kumbuka Mabomu ya Chavda, Milioni 900, he he he ilikuwaje?
Wanachofanya wapinzani ni sawasaw na kujenga nyumba isiyokuwa na msingi, wanakimbilia kuezeka wakati wakijua nyumba haina msingi. Reverend aliwaambia ukweli kama madai ya ufisadi ya ushahidi hawna haja ya kusimama kwenye majukwaa waendee mahakamani na vilevile ili kujenga nyumba imara ni lazima kuwe na msingi imara, walilie marakebisho ya katiba. Otherwise I love CCM kwani wanajua mbio za wapinzani wao hazizidi speed 50 wakati wao wako 120.
 
Hoja ya ufisadi haina nguvu, kwani katika list of shame hakuwataja wapinzani ambao ni mafisadi. Sasa kama wewe ni fisadi na hujajitaja kwenye hiyo list na unajulikana kabisaunadhani hii hoja itakwenda wapi? halafu ka-hoka kenyewe ni very light katika ulingo wa siasa. Kumbuka Mabomu ya Chavda, Milioni 900, he he he ilikuwaje?
Wanachofanya wapinzani ni sawasaw na kujenga nyumba isiyokuwa na msingi, wanakimbilia kuezeka wakati wakijua nyumba haina msingi. Reverend aliwaambia ukweli kama madai ya ufisadi ya ushahidi hawna haja ya kusimama kwenye majukwaa waendee mahakamani na vilevile ili kujenga nyumba imara ni lazima kuwe na msingi imara, walilie marakebisho ya katiba. Otherwise I love CCM kwani wanajua mbio za wapinzani wao hazizidi speed 50 wakati wao wako 120.

kumbe hiki kitu sio mimi tu niliyekiona, nilisema hawa watu wanataka bubble gum development, na wanataka walale leo kesho waamke matajiri kitu ambacho hakitatokea leo wala kesho !

it takes hard work and determination !
 
kwa kifupi alikuwa akimaanisha hao mafisadi mbona hawajajitaja ?? kwani wao nao hawafanyi ufisadi ?
 
Mzee katika Mafungu ya MAFISADI umepewa/umetengewa kiasi gani? Nani katika upinzani ni FISADI? naomba majibu

Hapo sasa ndipo tunapokusea mtu akiwa na mawazo tufauti anaambiwa kapewa kiasi... sasa hao wa vyama vya ushindani nao wamepewa kiasi gani, tuache hii haijengi...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom