2013
JF-Expert Member
- Aug 2, 2011
- 11,358
- 6,059
Hapo ndipo chadema mlipotea na hamtarudi kwenye mstari tena! Kuamini kwamba lowassa kwa kuwa ametoka ccm atachukua nchi kwa urahisi! Mkasahau itikadi yenu na kuitupa na sasa hatuwaamini tena. Subirini maporomoko wa kutisha 2019 serikali za mitaa na 2020 uchaguzi mkuu. Nani atawaamini vigeugeu. Mara leo hii ni nyeusi na haisafishiki kabisa. Tena mna ushahidi wa kutosafishika! Tena ni heshima kwa mungu kuitupa hiyo nyeusi. Mara, hapana! Ni nyeupe haina doa! Macho yetu hayakuona vizuri tulikosea jamani! Ubababishaji gani huu! Ccm oyeee! Hapa kazi tu!! Bla bla huko huko ufipa!!
Naona unanimilikisha chama. Mi nimetoa mchanganuo na sio ushabiki wa vyama.Anyway sioni haja ya ku apologize kwa kutokueleweka vyema.
Hoja kuhusu itikadi:-
Dk slaa aliwahi kunukuliwa akisema kazi ya chama cha siasa ni kuchukua dola. Cdm haiko pale kua mpinzani milele. Na mkakati wa kumchukua el, ulilenga kuidhohofisha ccm wakati wa uchaguzi. Ili wachukue dola. Sidhani kama kuna itikadi bora zaidi ya hiyo ya kuchukua dola. Ccm wamekua wakishinda uchaguzi pasi kua na itikadi ya maana miaka yote. Hii inamana wanajua kua swala sio itikadi bali ni kumiliki dola. Na mbinu yao imefanya kazi miaka yote.
Swala la upinzani kufa litaathiri watanzania wengi na nchi. Manake ccm unayoijua inakwenda kutawala kila mahali. May be hii itakua furaha yako kwa muda, lakini kumbuka maendeleo ya taifa lolote duniani.. Ni pamoja na kuwepo kwa strong and effective opposition political party.
Naamini bado hujajua kwanni dunia inataka siasa za ushindani. Unadhani swala ni cdm ama ccm swala ni maendelo na ustawi... Kama ccm wataingiza wengi bungeni jua kua hoja zote zitapita bila kupingwa bungeni. Na wewe kama mtazania usiye tabaka tawala uko katika hatari ya kutonufaika na keki ya taifa ikiwa hoja hizo hazina maslahi mapana ya kitaifa.