Kwa mara ya kwanza ninakwenda kuipigia kura CCM 2020

Hii ni kauli ya mfanyakazi mmoja wa ngazi za juu anayefanya kazi taasisi ya bodi ya ugavi hapa nchini(PSPTB).

Leo nimetembelea bodi ya ugavi kwa mambo yangu binafsi na nikiwa hapo nilifanikiwa kubadilishana mawazo na baadhi ya wafanyakazi ila nilichokigundua kinachozungumzwa maofini juu ya magufuli kwa wafanyakazi wa serikali ni tofauti kabisa na mijadala ilivyo humu mitandaoni.

"Kwa mara ya kwanza ninakwenda kuipigia kura CCM 2020"Hii ilikua ni kauli ya afisa huyo ambaye alisema tangu ameanza kupiga kura hajawahi kuipigia kura CCM kutokana na mambo yake ya hovyo ila kwa sasa Magufuli amekua kivutio kikubwa.

Aliongeza kwakusema,"Siwezi kumchagua raisi tofauti na Maguli kwani kura yangu siwezi kui risk kumpigia kura raisi tofauti nisiyefahamu atakuaje baada ya kua raisi".

Mwisho afisa huyu alisema na hapa namnukuu,"Tutarajie 2020 Maguli kushinda kwa zaidi 80% kwani kwa sasa huyu ndiye pekee aliyeonesha dira kuivusha nchi".

Hii ndio hali ya maofisini na kuhusu vijijini mapenzi kwa Magufuli ni zaidi ya hali ilivyo mijini wananchi huwaelezi chochote kuhusu Maguli.

Nimeona niliseme hili ili huyu inaeitwa Lowasa na wafuasi wake wajipange vizuri uchaguzi ujao ama waahirishe ili pesa za kampeni ziweze kujenga hata makao makuu ya chama.
Hali ya maofisini wakati umezungumza na mfanyakaz mmoja tu halafu unaconclude kwa kuonyesha ni ofisi zote
 
Walijua wewe ni nyoka wakakupaka mafuta kwa mgongo wa chupa kulinda vibarua vyako.
Saikolojia yangu ni nzuri sana kutambua uongo na ukweli hasa ninapokua ana kwa ana na muhusika.Lakini pia mi ni mtu wa kawaida kabisa sina mahusiano yoyote na.serikali ya Magufuli
 
Acha kuwasingizia wafanyakazi sema wewe ndio utampigia vijana Wa ccm mnajifariji tu wananchi wanajua baya Na zuri subirini matokeo
 
Kwani unafikiri akili yake bado iko sawa na miaka ya nyuma? Hujui mtu akizeeka na akili inachoka? Zamani alikuwa kijana mwenye ndoto safi ndio maana alikuwa anaikataa ccm, sasa kazeeka akili IMECHOKA ndio maana anafikiri kizembe zembe, mawazo yake hayana tofauti na LYATONGA, Lyatonga huyu wa sasa si yule wa 1995 na sababu ni UZEE, kumbukumbu kwisha kichwani.
Kuna point hapa..!
 
CHADEMA mwaka jana ingemsimamisha Dr. Slaa ingetoa changamoto kuliko wanavyofikiria. Tatizo lao ni kutojiamini tu. Hilo ndilo linafanya Chama chao kipoteze mwelekeo hivi sasa. Hakina mvuto na hata ukiwauliza mtaani kama wanamjua Katibu Mkuu wa CDM watamtaja Dr. Slaa!! Huyo wa sasa sijui anafanya nini!! Na sijui anaitwa nani??
Bao la mkono baba
 
Bao la mkono baba
Watu walitekwa kiakili kwamba wataibiwa kura kwa kauli ya bao la mkono! Haikuwa na maana hiyo. Hivi tuwe wakweli kama kweli CCM ingeamua ishinde kwa kuiba kura au hila nyingine wapinzani mngepata wabunge na madiwani wangapi? Ni woga wenu tu. Kipigo kilikuwa halali maana wapinzani hawakuwa na haja ya kwenda IKULU na wala hawakujiandaa kuchukua dola mwaka 2015 ndio maana waliokoteza hata baadhi ya wagombea dakika za mwisho!!
 
Ki ukweli mheshimiwa rais Magufuli ni rais wa namna yake katika enzi hizi. Watu wasiomjua bado wataendelea kumpinga, lakini baada ya muda mfupi yule aliyempinga atakuja kujutia kauli zake. Ninathubutu kusema hivi kwa sababu nina imani baada ya miaka hata 3 tu ya mwanzo Tanzania itakuwa imepiga hatua kubwa sana za maendeleo. Wananchi wanataka maendeleo siyo porojo au kauli za ovyo ovyo tu. Siku zote mwenye njaa anashibishwa kwa chakula siyo kwa maneno matamu au vinginevyo.
 
Back
Top Bottom