Huo ni ukweli mtupu hasa pale mnapopata raisi asyiyekuwa na uchungu na nchi,si muwajibikaji,si jasiri kufanya maamuzi magumu na anaendekeza sera isiyo rasmi ya kulindana.Matokeo yake mtajikuta wote kuanzia mkuu wa kaya mpaka mwananchi wa kawaida wote mnakuwa walalamikaji tu na hakuna wa kuchukua hatua.Mbaya sana.Akichezesha taya na mwandishi wa TBC1 Marin hassan,dr benson bana alitamka wazi kabisa kwamba tatizo sio mawaziri wapya bali ni mfumo mzima wa uteuzi,alisitiza kwamba tutapoandika katiba mpya swala la rais kupewa madaraka ya uteuzi wa kila kitu ndio unaokwamisha uwajibikaji ndani ya serikali,safi sana Dr Bana kwa kuliona hilo.
Nawasilisha