BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
Jana nilikuwa nimesimama kwenye kituo kimoja cha Daladala nikisubiri Usafiri wa kwenda City Centre. Nilikuwa mkabala na meza mbili za wauza magazeti na nikajikuta nikifanya kautafiti kadogo tu nikiandika kwenye karatasi nililokuwa nalo. Katika muda wa dakika 35 nilizosimama pale:
Meza ya Kwanza:
Watu wapatao 35 walisimama kusoma vichwa vya habari vya magazeti;
Kumi na moja katika yao wakanunua magazeti.
Sita kati yao walinunua magazeti ya Udaku -Kiu, Ijumaa, Hamu,Risasi, Sani nk.
Wawili wakanunua Mwananchi
Mmoja akanunua Raia Mwema
Mmoja akanunua MwanaHalisi
Mmoja akanunua Tanzania Daima.
Kati ya hawa Kumi na moja walionunua magazeti, sita walikuwa wanawake ambao kati yao Wanne walinunua magazeti ya Udaku.
Meza ya Pili:
Watu 41 walisimamakusoma vichwa vya habari vya magazeti.
Tisa kati yao wakanunua magazeti.
Watano kati yao wanunua magazeti ya Udaku.
Wawili wakanunua MwanaHalisi
Mmoja akanunua Rai Mwema
Mmoja akanunua gazeti la michezo la Dimba
Kati ya Tisa walionunua magazeti Watatu walikuwa wanawake ambao wote walinunua magazeti ya Udaku.
Ninafahamu kuwa hii haiwezi kuchukuliwa kama kigezo cha namna yoyote lakini hata tukichukulia kwa sehemu niliyokuwa, ina maana kuwa watanzania wanapenda zaidi kusoma magazeti ya Udaku kuliko magazeti kama Raia Mwema, MwanaHalisi na Mwananchi ambayo yangewasaidia kufungua Bongo zao.
Ni wazi kuwa Watanzania bado tuna Safari ndefu mno ya kujikomboa.
Meza ya Kwanza:
Watu wapatao 35 walisimama kusoma vichwa vya habari vya magazeti;
Kumi na moja katika yao wakanunua magazeti.
Sita kati yao walinunua magazeti ya Udaku -Kiu, Ijumaa, Hamu,Risasi, Sani nk.
Wawili wakanunua Mwananchi
Mmoja akanunua Raia Mwema
Mmoja akanunua MwanaHalisi
Mmoja akanunua Tanzania Daima.
Kati ya hawa Kumi na moja walionunua magazeti, sita walikuwa wanawake ambao kati yao Wanne walinunua magazeti ya Udaku.
Meza ya Pili:
Watu 41 walisimamakusoma vichwa vya habari vya magazeti.
Tisa kati yao wakanunua magazeti.
Watano kati yao wanunua magazeti ya Udaku.
Wawili wakanunua MwanaHalisi
Mmoja akanunua Rai Mwema
Mmoja akanunua gazeti la michezo la Dimba
Kati ya Tisa walionunua magazeti Watatu walikuwa wanawake ambao wote walinunua magazeti ya Udaku.
Ninafahamu kuwa hii haiwezi kuchukuliwa kama kigezo cha namna yoyote lakini hata tukichukulia kwa sehemu niliyokuwa, ina maana kuwa watanzania wanapenda zaidi kusoma magazeti ya Udaku kuliko magazeti kama Raia Mwema, MwanaHalisi na Mwananchi ambayo yangewasaidia kufungua Bongo zao.
Ni wazi kuwa Watanzania bado tuna Safari ndefu mno ya kujikomboa.