kalamata
Senior Member
- Apr 16, 2011
- 144
- 29
...Wakati anaendesha kipindi cha jambo Tanzania leo tarehe 02.jul.12 pale Dodoma kwa kweli Dada yangu huyu hakua katika vazi la sitara kwa mujibu wa silka na desturi zetu watanzania na hata katika tasnia ya habari,nasema hivyo kwa sababu gani?kwa sisi watanzania tuliolelewa katika maadili mazuri,na ninaamini pia dada Rahel yumo,ni vibaya sana mwanamke anapovaa nguo fupi hadi MAGOTI yake kuonekana waziwazi,haswa anapokua mbele ya wanaume watu wazima.Kwa alie tazama Jambo Tanzania ya leo atathibitisha hayo,dada Rahel alivaa gauni fupi mno kiasi cha kuonyesha miguu yake hadi magoti kua wazi mno kiasi cha kuonyesha mapaja yake,jamani wanaotetea haki za wanawake wapo wapi?samahani dada Rahel kama nitakua nimekukwaza.Nyie waandishi wa habari mjue mnaheshimika sana katika jamii.naomba muwe mfano mzuri,nyinyi sio ma-miss.jiheshimuni haswa kwenye mavazi.