Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Mkapa roads zanzibar,
Moja inatokea njia ya Amani kupitia Darajabovu mpka Bububu, hii aliifungua Mkapa na inaitwa Mkapa road.
Nyengine inaotokea Kisiwandui kuelekea Michenzani pia inaitwa Mkapa road.
Haikutosha kuna Shule ya walimu kisiwani Pemba inaitwa Benjamin W. Mkapa.
Mbali na utitiri wa vibanda vya kupiga soga vinavyoitwa "maskani za chama, vilivyotapakaa katika vichochoro mbalimbali vya Manispaa ya zanzibar ambavyo vingi tu vinaitwa kwa jina lake.
"Maskani ya Mkapa" linasomeka bango moja lililotundikwa katika moja ya vibanda hivyo katika eneo la Darajani.
ukiuliza. Jibu ni kuwa ni kumuenzi Mh. Mkapa kwa blah blah blah...
Hapana tatizo kumuenzi kiongozi, tatizo ni kwa lipi kiongozi huyo aenziwe?
Kwa mtu kama Mkapa anaenziwa kwa lipi zanzibar?
kwa kuwachagulia wazanzibar mtu wa kuwaongoza asiechaguo lao?
Kama amiri jeshi mkuu, kusabisha mauwaji ya kutisha Jan 27/01, kwa raia wasiokuwa na hatia?
Hivi?! Hakuna watu walioifanyia makubwa zanzibar wakastahili kupewa majina ya barabara na shule hizo?
Basi hata Aboud Jumbe Mwinyi hana hata kichochoro au kibanda cha kuuzia urojo kilichopewa jina lake?
Au J.Okello, kahatarisha uhai wake 1964 kwa kuifurusha madarakani serikali halali ya wazanzibar, hata ile kambi ya "janjaweed" ya kule Hanyegwamchana, haijapewa jina lake? is it fair kweli?
Nani katika vitoto vya siku hizi zanzibar vinamjua Abdulrahman Mohammed Babu? dunia inamjua wazanzibar wenyewe hawamjui! shame.
Wapi pana kumbukumbu ya maulamaa na wasomi wa zanzibar kama akina Omar bin Sumeit ambao nchi za n'gambo hukoo zimeweka kumbukumbu zao lakini kwa zanzibar walipotokea na kutoa utumishi wao uliotukuka hawana alama yoyote.
Nani katika vizazi vya leo anamfahamu kanali Ali Mahfoudh(jamadari), hukoo Msumbuji wanamuimba na kumuenzi kwa mchango aliotoa kwa FRELIMO katika mapambano na wakoloni, kwao zanzibar kitovu chake kilikozikwa, hakuna hata uwanja wa kuchezea judo uliopewa jina lake.
Ipo wapi alama ya mwanasiasa SK. Ali Muhsin Barwan(zaim)aliemfunza Nyerere "the saint", siasa ya usawa na umoja wa kweli wa Kiafrika kule Ghana 1950s,japo ile skuli ya kidongo chekundu ingetosha kumuenzi.
Si sawa hata kidogo kuona kuwa mashujaa wote hawa na wengine ambao sikuwataja hapa waliofanya mengi ya kustahali kuenziwa katika uhai wao wote visiwani alama zao zinapotea na vizazi vya leo haviwajui, na badala yake wanakuja watu wa siku mbili tatu na udhalimu juu, wanaekewa alama za kuwakumbuka milele.
Hata Mungu hayupo radhi na ndo maana wanasibika sasa.
Moja inatokea njia ya Amani kupitia Darajabovu mpka Bububu, hii aliifungua Mkapa na inaitwa Mkapa road.
Nyengine inaotokea Kisiwandui kuelekea Michenzani pia inaitwa Mkapa road.
Haikutosha kuna Shule ya walimu kisiwani Pemba inaitwa Benjamin W. Mkapa.
Mbali na utitiri wa vibanda vya kupiga soga vinavyoitwa "maskani za chama, vilivyotapakaa katika vichochoro mbalimbali vya Manispaa ya zanzibar ambavyo vingi tu vinaitwa kwa jina lake.
"Maskani ya Mkapa" linasomeka bango moja lililotundikwa katika moja ya vibanda hivyo katika eneo la Darajani.
ukiuliza. Jibu ni kuwa ni kumuenzi Mh. Mkapa kwa blah blah blah...
Hapana tatizo kumuenzi kiongozi, tatizo ni kwa lipi kiongozi huyo aenziwe?
Kwa mtu kama Mkapa anaenziwa kwa lipi zanzibar?
kwa kuwachagulia wazanzibar mtu wa kuwaongoza asiechaguo lao?
Kama amiri jeshi mkuu, kusabisha mauwaji ya kutisha Jan 27/01, kwa raia wasiokuwa na hatia?
Hivi?! Hakuna watu walioifanyia makubwa zanzibar wakastahili kupewa majina ya barabara na shule hizo?
Basi hata Aboud Jumbe Mwinyi hana hata kichochoro au kibanda cha kuuzia urojo kilichopewa jina lake?
Au J.Okello, kahatarisha uhai wake 1964 kwa kuifurusha madarakani serikali halali ya wazanzibar, hata ile kambi ya "janjaweed" ya kule Hanyegwamchana, haijapewa jina lake? is it fair kweli?
Nani katika vitoto vya siku hizi zanzibar vinamjua Abdulrahman Mohammed Babu? dunia inamjua wazanzibar wenyewe hawamjui! shame.
Wapi pana kumbukumbu ya maulamaa na wasomi wa zanzibar kama akina Omar bin Sumeit ambao nchi za n'gambo hukoo zimeweka kumbukumbu zao lakini kwa zanzibar walipotokea na kutoa utumishi wao uliotukuka hawana alama yoyote.
Nani katika vizazi vya leo anamfahamu kanali Ali Mahfoudh(jamadari), hukoo Msumbuji wanamuimba na kumuenzi kwa mchango aliotoa kwa FRELIMO katika mapambano na wakoloni, kwao zanzibar kitovu chake kilikozikwa, hakuna hata uwanja wa kuchezea judo uliopewa jina lake.
Ipo wapi alama ya mwanasiasa SK. Ali Muhsin Barwan(zaim)aliemfunza Nyerere "the saint", siasa ya usawa na umoja wa kweli wa Kiafrika kule Ghana 1950s,japo ile skuli ya kidongo chekundu ingetosha kumuenzi.
Si sawa hata kidogo kuona kuwa mashujaa wote hawa na wengine ambao sikuwataja hapa waliofanya mengi ya kustahali kuenziwa katika uhai wao wote visiwani alama zao zinapotea na vizazi vya leo haviwajui, na badala yake wanakuja watu wa siku mbili tatu na udhalimu juu, wanaekewa alama za kuwakumbuka milele.
Hata Mungu hayupo radhi na ndo maana wanasibika sasa.