IsangulaKG
JF-Expert Member
- Oct 14, 2010
- 706
- 386
Tanzania imekuwa na waandishi wa Vitabu wengi sana na mara nyingi Vitabu hivi huongelea matukio ya kihistoria kama vile Uhuru, Ujamaa n.k na wengine huandika 'novel' zilizojaa hadithi za kusisimua na kuogofya na mazingira ya 'kufikirika' tu ambayo hayawezi kumjengea babu yangu kule uwezo wa kufikiri.
Wiki iliyopita katika kutafuta Vitabu vya Watanzania nikakutana na hiki kinachoitwa 'SINDANO INAYOVUJA-A leaking Needle, kitabu cha mtanzania ambacho kimechambua sekta ya Afya na Kupendekeza Mbinu Bora za kuiboresha, Mbinu ambazo kama zingetekelezwa labda tusingekuwa tunaongelea Mgomo wa madaktari sasa
Bofya Hapa: Amazon.com: SINDANO INAYOVUJA (A Leaking Needle) (Swahili Edition) (9781468156898): Kahabi G Isangula: Books
Jambo la kusikitisha ni kwamba Maarifa yaliyomo humu yaliyoandikwa na Mtaalamu huyu kwa Lugha ya KISWAHILI kwa kuwalenga Watanzania yatapita hivi hivi abda kwa kuwa sisi ni WAZEMBE wa kusoma VITABU vya KUFIKIRISHA akili zetu( Hii inadhihirika na watu humu JF wasivyopenda kusoma Post za kufikirisha akili zao kwa ushaidi kuwa watu wanao peruzi ukurasa wa 'Great Thinkers' ni wachache mno ukilinganishwa na kwenye 'mahusiano' 'Celebrity' na 'siasa') au kwa sababu ya DHARAU kwa waandishi wa Kitanzania na KUTOTHAMINI CHA NYUMBANI.
Mimi nimeshanunua nakala yangu, shukrani kwa CRDB Tembocard Visa iliyoniwezesha kununua kitabu hiki toka Amazon.
Waweza kuungana nami au ukaungana na kundi nililotaja hapo juu.
Wiki iliyopita katika kutafuta Vitabu vya Watanzania nikakutana na hiki kinachoitwa 'SINDANO INAYOVUJA-A leaking Needle, kitabu cha mtanzania ambacho kimechambua sekta ya Afya na Kupendekeza Mbinu Bora za kuiboresha, Mbinu ambazo kama zingetekelezwa labda tusingekuwa tunaongelea Mgomo wa madaktari sasa
Bofya Hapa: Amazon.com: SINDANO INAYOVUJA (A Leaking Needle) (Swahili Edition) (9781468156898): Kahabi G Isangula: Books
Jambo la kusikitisha ni kwamba Maarifa yaliyomo humu yaliyoandikwa na Mtaalamu huyu kwa Lugha ya KISWAHILI kwa kuwalenga Watanzania yatapita hivi hivi abda kwa kuwa sisi ni WAZEMBE wa kusoma VITABU vya KUFIKIRISHA akili zetu( Hii inadhihirika na watu humu JF wasivyopenda kusoma Post za kufikirisha akili zao kwa ushaidi kuwa watu wanao peruzi ukurasa wa 'Great Thinkers' ni wachache mno ukilinganishwa na kwenye 'mahusiano' 'Celebrity' na 'siasa') au kwa sababu ya DHARAU kwa waandishi wa Kitanzania na KUTOTHAMINI CHA NYUMBANI.
Mimi nimeshanunua nakala yangu, shukrani kwa CRDB Tembocard Visa iliyoniwezesha kununua kitabu hiki toka Amazon.
Waweza kuungana nami au ukaungana na kundi nililotaja hapo juu.