Elections 2010 Kwa Kukipenda Chama Changu (CCM) - Sitomchagua Kikwete Mwaka Huu (Octoba 2010)!

afrolife

Senior Member
Oct 27, 2009
154
102
I'm a youth, a CCM member, and one among the many victims of Jakaya's myths; infact i was on my final year (undergraduate) when this gentlemen visited the campus, and to be honest i was really turned on by him (kinda fan of him even before that day). Kutokana na ahadi zake na utendaji kazi wake katika wizara mbalimbali, nilijikuta nikimwamini sana na niliamini anaweza kuivusha Tanzania toka hapo ilipo. Bila kinyongo na kwa matumaini makubwa nikampa KURA yangu mwaka 2005!

Just to my surprise .... soon after taking the oath to the magogoni office, its only when i came to realize that i did a very serious and biggest mistake in my life ... the pandora box started to unveil itself! Mengi yamesemwa sana, naipenda sana CCM ya Kambarage, lakini pia nachukia sana mfumo wa CCM wa sasa pamoja na leadership style yake. Mambo mengi yamebadilika na viongozi hawa hawaambiliki na hawasikilizi wananchama wao kabisa! Its like wamejitengenezea mbingu yao peke yao ndani ya chama.

Mimi sio muumini wa mapinduzi nje ya chama kama wengine, naamini mabadiliko yanaweza kufanywa hata ungalipo ndani ya chama. Rais Kikwete amenivunja moyo sana, amenisononesha sana, na amenifanya nijisikie mnyonge sana ndani ya nchi yangu mama niipendayo. Nimeshakata shauri, kama chama (CCM) kitampitisha mh. Kikwete kuwa mgombea wao wa urais, basi kura yangu itaenda kwa kiongozi yeyote yule wa upinzani (hapa sitojali chama) au binafsi ambaye angalau ataonekana ana matumaini ya kutetea nchi yangu na rasilimali zake, pamoja na maslahi ya vizazi vya baadae. Nitashawishi mke wangu, wadogo zangu, rafiki zangu, jamaa zangu na ndugu zangu kutompigia huyu mheshimiwa kura ya Urais na mbunge yeyote mbovu atakayepitishwa jimboni kwangu. Ninaamini peke yangu kwa uchache sitokosa watu (kura) 20, na wengi wakifanya kama hivi basi naamini hiyo itakuwa ni adhabu tosha kwake na kwa wenzake wasiosikia vilio vyetu! Hata kama atashinda, basi si kwa kishindo tena na message itakuwa imeshakuwa delivered!

Sina nguvu ya kushindana na dola, lakini pia nina nguvu isiyoweza pokonywa na dola, nayo ni uwezo wa kuchagua mtu nimtakaye kuwa kiongozi wangu (rais, mbunge, diwani etc) kupitia KURA yangu, kwa utashi wangu! Huu si muujiza, inawezekana!!

Note: Najua wana-CCM wenzangu na wapenzi wa JK mtakuja kwa wingi kama nyigu kunipinga na kunikejeli, lakini huo ndio uamuzi wangu ... NO RETREAT!!
 
No surrender! why not, unatumia haki yako ya kiraia na kidemokrasia. Kura yako ikikosekana, ukichanganya na za wale laki tatu na nusu...aaaaaah si haba!
 
Excellent kaka, kaka yule mzee wa jiweni kwenye kahawa. Anajenga gorofa, ananunua vogue kwa story za kijiweni akitoka hapo anaenda home usingizi mzito kasahau kila kitu.
 
wenye maumivu kama Afrolife ni wengi tena sana. Sasa kwanini ujumbe huo usiwe shared na wanaCCM wengi, natumaini watatokea watu jasiri kama Shibuda wengi. Shibuda amejitokeza lakini hana mikakati ya kushawishi wana-CCM ili kumuunga mkono. Nasikitika kwamba CCJ imeanzishwa nje ya CCM ilitakiwa ianzishwe na ku-operate ndani humo humo. Siyo siri umoja wa kijinga wa wanaCCM utaendelea kutuweka pabaya.
 
Mko wachache sana kaka wa namna yako hapo kwa jembe na nyundo. Muda ulisema, unasema na utaendelea kusema.
 
wenye maumivu kama Afrolife ni wengi tena sana. Sasa kwanini ujumbe huo usiwe shared na wanaCCM wengi, natumaini watatokea watu jasiri kama Shibuda wengi. Shibuda amejitokeza lakini hana mikakati ya kushawishi wana-CCM ili kumuunga mkono. Nasikitika kwamba CCJ imeanzishwa nje ya CCM ilitakiwa ianzishwe na ku-operate ndani humo humo. Siyo siri umoja wa kijinga wa wanaCCM utaendelea kutuweka pabaya.

kwa uamuzi huu naamini nitakuwa nimemsaidia Mwenyekiti na Rais wangu kuondokana na aibu hii anayoibebesha serikali ya CCM ... it's enough!
 
Tekele wajibu wako,hiki ndicho kitu cha mana mbacho kinapima kuelimika kwako.Endelea kuwashawishi wengine popote ulipo
 
Nimeshakata shauri, kama chama (CCM) kitampitisha mh. Kikwete kuwa mgombea wao wa urais, basi kura yangu itaenda kwa kiongozi yeyote yule wa upinzani (hapa sitojali chama)

Atakuwa mgombea wa chama chenu ila wewe hautampigia. We si bado ni mwenzao?

Mimi simo.
 
Chama cha Mapinduzi ni chama cha WAKULIMA na WAFANYAKAZI.
Hili lipo kwenye katiba ya chama lakini chama kimeporwa na wafanyabiashara, wezi, mafisadi, mabepari na wengine wanaofanana na hao ambao ndio maadui wa chama tangu asili!
Wenye chama ambao ni wakulima na wafanyakazi hawana influence tena kwenye chama chao.
Hao waliopora chama wanakiongoza chama moja kwa moja au kupitia mawakala wao ambao wanachaguliwa na wanachama wenyewe kutokana na ujinga tu.
Kutomchagua Kikwete tu hakubadilishi chochote bali la muhimu ni kujitahidi kurudisha chama kwa wenyewe ambao ni WAKULIMA na WAFANYAKAZI wa Tanzania.
Uwezo wa kufanya hivyo upo kwa kuwa wengi ni wakulima na wafanyakazi wanaodhulumiwa na waliokuwa maadui wa chama enzi kikiasisiwa.
 
i like the motive, seems many are on the track, lets move people---------Afrolife you are the men, am supporting you 100%
 
Back
Top Bottom