Kwa kuanzia tuuite mswada wa katiba kama Mswada wa Makinda

Pax

JF-Expert Member
May 3, 2009
268
87
Ndugu watanzania wenzangu popote pale mlipo, wengi wetu wenye nia njema na nchi yetu tumefadhaishwa sana na namna mambo yanavyopelekwa kuhusu katiba mpya. Tanzania tunahitaji katiba iliyotokana na maoni yetu sisi wananchi. Kwa bahati mbaya sana kuna watu wamelewa madaraka wakiamini kuwa wao wana akili kupita watu wengine wote, wakiamini kuwa wao walizaliwa ili watutawale na sisi tuwe watawaliwa maisha yetu yote. Nia na dhamira zao tumeshazielewa, kwa mtu yeyote mwenye uelewa ataona kwamba kuna usanii uliovuka mipaka na watu hawa wako tayari hata kutuharibia amani yetu alimradi watutawale tu.

Kwa kuanzia ili kuonyesha kuwa hatukubaliani na kinachofanyika naomba muswada na hata ukishakuwa sheria utambulike kama muswada au sheria ya Makinda kuonyesha kuwa sio wa wananchi wa Tanzania. So please lets refer to the Bill as Makinda's Bill and not otherwise as one way to voice our disagreements. Kila mtu akiuita kwa jina hilo nadhani ni one way ya kupeleka ujumbe hasa kwa wale wananchi wa vijijini. Nawasilisha
 
Back
Top Bottom