The Hunter
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 1,049
- 305
Nakumbuka uliposimama na kuishawishi serikali Kuongeza ushuru wa mafuta ya taa kwamba ndo solution ya tatizo la uchakachuaji,niwazi hukufikiri sana ushauri wako kwani Kama ungefanya utafiti kidogo ungegundua athari za ushauri wako huo usio wa kisomi kwa watanzania wa maisha ya chini wengi wao wakiwa pale kyela, mbinga, likuyufusi, turiani, na sehemu Nyingine nyingi.Leo watanzania wanaponunua nusu lita ya mafuta ya taa kwa Tsh 1000. lazima tukukumbuke na tuzidi kuwalaani wanamagamba wote.Wote tunajua uchakachuaji na athari zake, lakini wanaofanya hivyo ni wahuni wachache ambao kama mngekuwa na dhamira ya kweli, mngeweza kuwadhibiti, Tatizo wachakachuaji ni miongoni mwenu wanamagamba,kwani nyie ndo wamiliki wa gas stations.