Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Wakati wa kumaliza Mkutano wa 20 wa Bunge Wabunge walimlalamikia aliyekuwa Spika wa Bunge hilo Samwel Sitta, kuwa TAKUKURU inawafuatilia majimboni wakati wanatoa misaada ili kutimiza ahadi zao. Baada ya kutaka ufafanuzi toka kwa AG kuwa vijana wa Hoseah waachwe kufanya kazi zao, Sitta aliongeza kusema kuwa misaada ya kutolewa usiku inatia mashaka! Muda si muda mkewe Sitta alidakwa na TAKUKURU usiku guest akiwa na simu kadhaa mpya zikiwa kwenye maboksi yake, fedha taslim zaidi ya 1m/- na bahasha nyingi za kuwekea "vijisenti" hivyo! Hata kama hujaenda shule, akili za kawaida zitakuambia mazingira hayo yanaashiria nini! Cha kushangaza ni pale Sitta anapothibitisha ule usemi "mkuki kwa nguruwe..." kwa kusema eti hataacha "mambo haya yaishe hivi hivi" akiwa na maana kuwa ata-deal na maofisa wa TAKUKURU waliomdaka mkewe! Mimi simwelewi huyu "mpambanaji" wa ufisadi anapokuwa na double standard! Au "upambanaji" wake ulikuwa kuhusu Richmond peke? Au tuseme kuwa vita ya ufisadi inapambanwa "kibinafsi?"