Kwa hili serikali ni lazima itoe maelezo ya kina.

Deofm

JF-Expert Member
Feb 27, 2012
383
68
Dk. Slaa alidondosha machozi mbele ya hadhara alipokuwa akizungumzia madhila yanayowapata wafugaji kwa kugeuzwa chanzo cha fedha na baadhi ya askari wasiokuwa waaminifu.

Kiongozi huyo alifikia hatua hiyo baada ya kuanza kueleza namna mmoja wa viongozi wa wafugaji wilayani Kilosa alivyomfuata na kumweleza kuwa askari wa Jeshi la Polisi, mgambo na viongozi wa serikali za vijiji wanavyowanyanyasa na kuwadhalilisha wafugaji.

“Nikiwa Kilosa mjini juzi, nilifuatwa na kiongozi wa wafugaji akaniambia baada ya kukamatwa, wake zao au mabinti zao hufanyiwa vitendo vya udhalilishaji mbele ya macho yao, lengo likiwa ni kuwafanya wawakomboe kwa haraka katika mateso hayo, hii inasikitisha kuona Tanzania imefikia hapa,” alisema.

Huku akifuta machozi, Dk. Slaa alisema inasikitisha kuona watu waliopewa dhamana ya kuongoza ndio walio mstari wa mbele kuwanyanyasa na kuwatesa wananchi.
SOURCE: Tanzania Daima.
MY take;
hapo penye red panatisha, kama serikali haitajisafisha kwa kuwatafuta wahusika wa tuhuma hizi na kuwapeleka mahakamani naikijulikana ni kweli waliwadhalilisha wanawake basi hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yaobai itaaminika kuwa serikali ndio iliyowatuma kufanya hivyo. kwa hili wakae tarayari kwenda the hegi. kwani hata mmiliki wa mtanadao wa Wikileaks anashtakiwa kwa kosa la udhalilishaji wanawake.
 
Wafugaji (Masai) wa Kilosa ni wakorofi mno na mara huingiza mifugo yao katika mashamba ya wakulima kwa nguvu na mara nyingine huwa na bunduki ili kutisha wakulima. Yamewahi kutokea mapigano ya wakulima na wafugaji nia ni Wakulima kulinda mashamba yaona Masai kulazimisha kulisha mifugo katika mashamba ya wakulima. Ya kudhalilishwa siyajui hivyo siwezi kuyasemea.
 
...si nasikia kuna kaya ilifungwa jela kwa sababu ya kimada! Ndio tz mambo kimya kimya..
 
Wafugaji (Masai) wa Kilosa ni wakorofi mno na mara huingiza mifugo yao katika mashamba ya wakulima kwa nguvu na mara nyingine huwa na bunduki ili kutisha wakulima. Yamewahi kutokea mapigano ya wakulima na wafugaji nia ni Wakulima kulinda mashamba yaona Masai kulazimisha kulisha mifugo katika mashamba ya wakulima. Ya kudhalilishwa siyajui hivyo siwezi kuyasemea.
Katika utawala bora, mtu anapovunja sheria sio vizuri kuwadhalilisha watoto na mke wake , inawezekana hata yeye haungi mkono huo uvunjaji wa sheria uliofanywa na baba/mume wake. tunapokataza raia wasijichukulie seria mikononi nayo iwe ya kwanza kutekeleza kwa vitendo
 
hili mimi nakubaliana nalo kabisa nimewahi kuishi kijijini miaka ya nyuma kabisa askari polisi alimpenda rafiki yangu wa kike ambae nilikuwa najamiana nae, akanifanyia visa akasema mimi ni jambazi wakati nilikuwa nakibanda changu nauza oil nilikaa miezi 12 rumande na bahati nzuri yule msichana nae akamkatalia akampiga sana mpka leo ana alama kwenye jeraha. ki ukweli askari polisi wamekuwa miungu mtu huko kijijini na wengi hatujui sheria hizi yaani ninaposikia polisi tanzania ni matatizo sana, nimekuj kwenye nchi za watu yaani polisi kama huna kosa ni rafiki mzuri sana anakusikiliza na hata kama una kosa hawezi kuanza kukupiga ovyo ovyo kama kwetu ukienda kwenye kituo chao wanakuchukulia kama mtu mwenye kuhitaji msaada wa haraka the way wanavyokuhudumia sio hawa wetu ni mateso sana, jeshi linahitajika kufumuliwa upya
 
Katika utawala bora, mtu anapovunja sheria sio vizuri kuwadhalilisha watoto na mke wake , inawezekana hata yeye haungi mkono huo uvunjaji wa sheria uliofanywa na baba/mume wake. tunapokataza raia wasijichukulie seria mikononi nayo iwe ya kwanza kutekeleza kwa vitendo

Tatizo TZ hakuna utawala bora!
 
Dk. Slaa alidondosha machozi mbele ya hadhara alipokuwa akizungumzia madhila yanayowapata wafugaji kwa kugeuzwa chanzo cha fedha na baadhi ya askari wasiokuwa waaminifu.

Kiongozi huyo alifikia hatua hiyo baada ya kuanza kueleza namna mmoja wa viongozi wa wafugaji wilayani Kilosa alivyomfuata na kumweleza kuwa askari wa Jeshi la Polisi, mgambo na viongozi wa serikali za vijiji wanavyowanyanyasa na kuwadhalilisha wafugaji.

"Nikiwa Kilosa mjini juzi, nilifuatwa na kiongozi wa wafugaji akaniambia baada ya kukamatwa, wake zao au mabinti zao hufanyiwa vitendo vya udhalilishaji mbele ya macho yao, lengo likiwa ni kuwafanya wawakomboe kwa haraka katika mateso hayo, hii inasikitisha kuona Tanzania imefikia hapa," alisema.

Huku akifuta machozi, Dk. Slaa alisema inasikitisha kuona watu waliopewa dhamana ya kuongoza ndio walio mstari wa mbele kuwanyanyasa na kuwatesa wananchi.
SOURCE: Tanzania Daima.
MY take;
hapo penye red panatisha, kama serikali haitajisafisha kwa kuwatafuta wahusika wa tuhuma hizi na kuwapeleka mahakamani naikijulikana ni kweli waliwadhalilisha wanawake basi hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yaobai itaaminika kuwa serikali ndio iliyowatuma kufanya hivyo. kwa hili wakae tarayari kwenda the hegi. kwani hata mmiliki wa mtanadao wa Wikileaks anashtakiwa kwa kosa la udhalilishaji wanawake.
hakuna anyetaka wajisafishe kwanza wanamaji ya kutosha? mimavi imewatapakaa mwili mzima unafikiri itatoka vipi yanahitaji maji ya bahari zote kufanya hivyo na kamwe hawatatakata!
 
Mimi niliskia habari kama hizi huwa moyo unaniuma sana, kwanini watu waishi kama wapo utumwani.wakati mwingine huwa naanza kufikiria labda kwasababu hii nchi kwa eneo la ukubwa inaonekana ni kubwa sana kiasi kwamba serikali imeshindwa kusimamia. Sijui lakini kuna wakati huwa nawaza labda basi hii nchi igawanywe zipatikane nchi tatu ili tuwe na eneo dogo tu kwa ajili ya kurahisisha maendeleo na usimamizi.mfano nchi ya bsudan imegawanyika kwa amani kabisa zimekuwa nchi mbili na wameachana kwa amani kabisa na sasa tunaona south sidan ina serikali yake. Hayo ni mawazo yangu tu,maana huwa naona gdp ya mtz ni ndogo tunazindiwa hadi wa warundi kwa sababu ya uchache wa watu. Na sasa sensa inakuja usishangae kuambiwa tumefika 50 milion.
 
Back
Top Bottom