Kwa hili Pinda umeboronga!! Mpira hauendeshwi ki-CCM!!

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
WAZIRI MKUU, Mizengo Pinda, amehoji sababu ya timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars kutokuwa na mchezaji kutoka Tanzania Visiwani.

Pinda alihoji hali hiyo jana bungeni akiunga mkono kauli ya Mbunge wa Dimani, Zanzibar, Hafidhi Ali Tahir, aliyelalamikia kitendo cha Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), chini ya Rais wake Leodegar Tenga, kuwa amekuwa ikiibagua Zanzibar katika mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

“Mimi naunga mkono kauli ya Tahir, kuna tatizo gani ukimchukua mchezaji mmoja kutoka Zanzibar na kuleta kwenye timu ya taifa, lazima tuhakikishe tunaimaliza Muungano kwa kuondoa malalamiko madogo madogo kama hayo,” alisema Pinda.

Pinda alitoa kauli hiyo jana, akifanya majumuisho ya mjadala wa hoja bajeti ya ofisi yake, mjini Dodoma.

Juzi, Tahir ambaye amepata kuwa refa aliyevaa beji ya Fifa, alimshambulia Tenga kuwa ni mbabe na mbaguzi kwa kutoishirikisha Shirikisho la soka Zanziabr (ZFA) katika mambo ya kimataifa.
Alisema, ubabe wa Tenga umesababisha Zanzibar ishindwe kushiriki mashindano ya Copa CocaCola nchini Afrika Kusini na kutoingizwa katika timu ya soka ya taifa inayonolewa na Brazil Marcio Maximo.

Source: Tanzania Daima
 
Last edited:
Ni hoja ya msingi la sivyo wawape ruhusa wazenji waunde timu yao kama ilivyo kwa scotland na England ndani ya ufalme wa kiingereza.
 
Sio mpila ni mpira. Sijaona hapa Pinda ameboronga kivipi? Fafanua!

Sorry nilimaanisha mpira. Wewe unaona ni sawa kwamba basi hata kama wachezaji kutoka zenji hawana sifa basi waingizwe tu kwenye timu ya taifa ilimradi tu wanatimiza matakwa ya muungano??
 
Sorry nilimaanisha mpira. Wewe unaona ni sawa kwamba basi hata kama wachezaji kutoka zenji hawana sifa basi waingizwe tu kwenye timu ya taifa ilimradi tu wanatimiza matakwa ya muungano??

Mimi sikubaliani na wachezaji kuingizwa kwenye timu bila kuwa na sifa. Lakini pia siamini kwamba Zanzibar hakuna mchezaji hata mmoja mwenye sifa ya kuingizwa Taifa Stars! Niambie kama Maximo amewahi kwenda Zenj kuangalia wachezaji wanaofaa kuingizwa Taifa Stars na akakosa.
 
WAZIRI MKUU, Mizengo Pinda, amehoji sababu ya timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars kutokuwa na mchezaji kutoka Tanzania Visiwani.

Pinda alihoji hali hiyo jana bungeni akiunga mkono kauli ya Mbunge wa Dimani, Zanzibar, Hafidhi Ali Tahir, aliyelalamikia kitendo cha Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), chini ya Rais wake Leodegar Tenga, kuwa amekuwa ikiibagua Zanzibar katika mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

“Mimi naunga mkono kauli ya Tahir, kuna tatizo gani ukimchukua mchezaji mmoja kutoka Zanzibar na kuleta kwenye timu ya taifa, lazima tuhakikishe tunaimaliza Muungano kwa kuondoa malalamiko madogo madogo kama hayo,” alisema Pinda.

Pinda alitoa kauli hiyo jana, akifanya majumuisho ya mjadala wa hoja bajeti ya ofisi yake, mjini Dodoma.

Juzi, Tahir ambaye amepata kuwa refa aliyevaa beji ya Fifa, alimshambulia Tenga kuwa ni mbabe na mbaguzi kwa kutoishirikisha Shirikisho la soka Zanziabr (ZFA) katika mambo ya kimataifa.
Alisema, ubabe wa Tenga umesababisha Zanzibar ishindwe kushiriki mashindano ya Copa CocaCola nchini Afrika Kusini na kutoingizwa katika timu ya soka ya taifa inayonolewa na Brazil Marcio Maximo.

Source: Tanzania Daima
Pinda kaboronga nini sasa hapo mkuu,kwani aliyosema ni uongo?,ni ukweli mtupu,ni vema Taifa Stars iwe na sura za pande zote mbili za Muungano maana Zanzibar kuna wachezaji wengi tu wazuri wenye sifa ya kuchezea Taifa Stars.Pia yaliyoelezwa kuhusu Leodgar Tenga ni ukweli mtupu,jamaa(Tenga) anachemka sana kuiongoza TFF(ikiwa ni pamoja na kuitenga ZFF).....Binafsi sijaona ishu yoyote ya uCCM hapo mkuu zaidi ya Ukweli mtupu ulioongelewa na PM
 
Pinda kaboronga nini sasa hapo mkuu,kwani aliyosema ni uongo?,ni ukweli mtupu,ni vema Taifa Stars iwe na sura za pande zote mbili za Muungano maana Zanzibar kuna wachezaji wengi tu wazuri wenye sifa ya kuchezea Taifa Stars.Pia yaliyoelezwa kuhusu Leodgar Tenga ni ukweli mtupu,jamaa(Tenga) anachemka sana kuiongoza TFF(ikiwa ni pamoja na kuitenga ZFF).....Binafsi sijaona ishu yoyote ya uCCM hapo mkuu zaidi ya Ukweli mtupu ulioongelewa na PM

Hili jambo Maximo alisha litolea maelezo kwamba hawezi kuchukua wachezaji mahali ambapo hakuna mfumo wa ligi inayoeleweka. U-CCM wa pinda unakuja anaposema wachukue walau mchezaji mmoja kutoka zenji ili kuondoa kero ndogo ndogo za muungano. Mwafaka umewashinda wanauzunguka leo wanataka waingize siasa kwenye timu ya taifa, hilo no na kama maximo ananisikia awatolee nje hao wataharibu timu.
 
Solution ni kwa Zanzibar kuwa na timu yao. Maana hata UK kuna timu ya England, Scotland na Wales. Ingawa wote ni ndani ya UK or Great Britain. Hivyo Zanzibar timu yao huru na kura yao huru ndani ya FIFA as well. Ugomvi kwisha.
 
Ukweli ni kwamba hakuna mfumo mzuri wa kupata wachezaji wa kuunda timu ya Taifa, tunakosa mascout wa kupita mikoani na kutambua vipaji. Siamini kwamba Zanzibar ukiacha Nadir Haroub na Abdi Kassim hakuna vijana wengine wenye uwezo wa kuichezea timu yetu ya Taifa.
 
Nadhani mzee Pinda hakujua kwamba kwenye timu ya taifa kuna wachezaji kama Nadir Haroub na Abdi Kassim kutoka Zanzibar. Naamini angejua hivi asingeunga mkono hoja hafifu ya mbunge huyo. Timu ya taifa haiundwi kwa kutoa nafasi za UPENDELEO wa KIKANDA au KIMKOA bali inaundwa kwa kufuata kipaji cha mchezaji husika tu.
 
Back
Top Bottom