Kwa hili la waalimu na sensa ya watu na makazi,kazi ipo?

HAKI USAWA

New Member
Apr 19, 2012
3
1
KUNA TAARIFA ZA KUAMINIKA KUTOKA VYANZO MBALIMBALI KUWA SERIKALI IMEWAONDOA WAALIMU KATIKA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA SENSA;
kUTOKANA NA HABARI HIZI BAADHI YA WAALIMU WAMEAMUA KUONGOZA MGOMO WA KUTIHESABIWA KATIKA SENSA HIYO INAYOTARAJIWA KUFANYIKA TAREHE 26/08/12.
HII NI HABARI KUTOKA KWA WAALIMU HUSIKA,NA WAALIMU WAMEINGIA KWENYE MGOMO BARIDI,AMBAO NI HATARI KWA WANAFUNZI;SIJUI SERIKALI HII INAWAZA NINI KATIKA HAYA.
 
Unachosema chaweza kuwa sahihi kwa sababu inasemekana mkuu wa wilaya wa hapa Meatu iliyoko mkoa mpya wa Simiyu alipokea taarifa kutoka kwa mkuu wa mkoa kwamba aondoe majina ya waalimu waliogoma, yaani ambao hawakufika kazini siku mgomo unaanza, ambayo ndiyo siku pekee waliyotembelea mashule na kuchukua orodha ya walimu ambao hawakufika kazini. Na kwa kuthibitisha hili, kwenye shule mmoja iliyokuwa kinara wa mgomo wilayani hapa wamechaguliwa waalimu wanne tu kati ya kumi na saba ambao ndo waalimu pekee waliokutwa dshuleni siku ya mgomo kuanza. Waalimu hawa hawakugoma, siku zote walikuwa wanakwenda kazini japo walikuwa hawafundishi. Kioja kingine kilichofanyika kutokana na kuwaondoa waalimu hawa ni kupanga wasimamizi na makarani wa sensa katika maeneo ambayo hawaishi. Wa kata A amepelekwa kata B, wa kijiji A kapelekwa kijiji B na wa kitongoji A kapelekwa Kitongoji B; kiyu ambacho ni kinyume na na taratibu za sensa. Karani anatakiwa atoke eneo husika analoishi.
 
Back
Top Bottom