Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Gazeti moja leo limeripoti kwa urefu maoni ya wabunge hawa wawili machachari, wakitetea madereva wa wabunge walipwe na serikali.
Kwa maoni yangu siwaungi mkono hata kidogo. Ni wakati huu ambapo tunapigia serikali kelele kuwa ipunguze matumizi kwenye magari ya watendaji wake ikiwemo kuondolewa kwa madereva binafsi kwenye payroll ya serikali. Ni wakati huu ambapo napendekeza kuwa katika nchi hii, wawepo watu watano tu wenye madereva binafsi, yaani raisi na makamu wake, waziri mkuu, spika na jaji mkuu. Watendaji na viongozi wengine wote, wajiendeshe wenyewe au waajiri madereva wenyewe katika safari zao za kila siku, isipokuwa kwa safari za kikazi nje ya maeneo yao ya kazi ambapo watatumia madereva wa ofisi na gari za ofisi (maximum cruiser-mkonga).
Kwa hiyo wakati tayari tukiona kuwa mzigo wa mamia ya magari na madereva serikalini ni mkubwa, itakuwa ni ajabu kama tukiamua kujiongezea tena mzigo wa madereva 320 wa kulipwa na serikali!!!
Makamanda Zitto, na Deo nawakubali sana, but katika hili... no no no...
Kwa maoni yangu siwaungi mkono hata kidogo. Ni wakati huu ambapo tunapigia serikali kelele kuwa ipunguze matumizi kwenye magari ya watendaji wake ikiwemo kuondolewa kwa madereva binafsi kwenye payroll ya serikali. Ni wakati huu ambapo napendekeza kuwa katika nchi hii, wawepo watu watano tu wenye madereva binafsi, yaani raisi na makamu wake, waziri mkuu, spika na jaji mkuu. Watendaji na viongozi wengine wote, wajiendeshe wenyewe au waajiri madereva wenyewe katika safari zao za kila siku, isipokuwa kwa safari za kikazi nje ya maeneo yao ya kazi ambapo watatumia madereva wa ofisi na gari za ofisi (maximum cruiser-mkonga).
Kwa hiyo wakati tayari tukiona kuwa mzigo wa mamia ya magari na madereva serikalini ni mkubwa, itakuwa ni ajabu kama tukiamua kujiongezea tena mzigo wa madereva 320 wa kulipwa na serikali!!!
Makamanda Zitto, na Deo nawakubali sana, but katika hili... no no no...