Kwa hili la kufungwa Mbunge Lema 2015 nipo tayari kwa lolote nimechoka kuwa MWOGA

Joblube

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
369
151
Naomba nikiri kuwa mimi ni mtu mmoja wapo ambae nilikuwa mwoga sana kuwekwa ndani hata katika kutea haki. Lakini baada ya kisa hiki cha Lema nimegundua kuwa nipo utumwani hali nikiaminishwa kuwa nipo huru na nimegundua kabisa haki haitapatikana kwa kupewa bali nikuipigania. Tazama jinsi wanavyofanya katika kuandaa katiba mpya ni mchezo mtupu ili waendelee kubaki madarakani waendelee kuneemeka wao na watoto wao siisi ambao hatuna wa kumtegemea huko Serikalini waendellee kututawala badala ya kutuongoza, wamewatawala Baba zetu na sasa wanataka watoto wao watutawale na sisi ndio maana wanawarithisha watoto wao (Kipi Wairioba, Nape Mnauye, Husen Mwinyi, Ridhiwan Kikwete, Vita Kawawa NK). Sasa hivi wamebuni mbunu hata za kuwahonga viongozi wa makanisa wafanye kazi ya kuwasafisha na hasa baadhi ya makanisa ya kilokole kisa waendelee kututawala. Nachukua ushauri wa Lema kuanzaia leo hii ni heri kishi jela ukitetea haki kuliko kuishi uraiani kwa anasa huku ukisababisha matatizo kwa wengine kwa ufisadi. Watanzania wenzangu tutafakari na tuchukue. Tumeonewa kiasi cha kutosha, Tumenyanyaswa kiasi cha kutosha na tumepuuzwa kiasi cha kutosha unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe, tunyanyaswe na kupuzwa sasa nasema basi 2015 kama hakuna tumehuru na Katiba mpya yenye matakwa ya Watanzania nasema lolote na liwe nasema basi.

Mungu Ibarika Tanzania
 
Hapo kwenye katiba mpya lazima damu imwagike ndio ccm wataelewa watu wamechoka.
 
Back
Top Bottom