Kwa hili JK unatutania!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Kikwete ataka kuziona ndege za ATCL angani
Mwandishi Maalumu
Daily News; Saturday,January 17, 2009 @21:15


"Ningependa hata tuanze kuruka Jumatatu kwa sababu ni dhahiri hatuwezi kuendelea kufanya kazi namna hii," alisema Rais Kikwete alipokutana na uongozi wa Wizara ya Miundombinu wakiwamo wakuu wa ATCL.

"Kutaneni haraka sana, yaani nyie ATCL, Wizara ya Miundombinu, na Wizara ya Fedha, ili kupata ufumbuzi wa mara moja utakaotuwezesha kuanza kutoa huduma zetu tena," Rais Kikwete aliwaambia viongozi hao juzi usiku katika mikutano yake na wizara mbalimbali kutathmini utendaji wa Serikali yake na mashirika yaliyoko chini ya wizara hizo kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake.

Katika mkutano huo uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete alisema ATCL inakabiliwa na changamoto mbili kubwa: moja ni kuhakikisha kuwa ndege zake zinarudi hewani mara moja, na pili ni kutafakari kwa kina nini hali ya baadaye ya kampuni hiyo ya ndege inayomilikiwa na Serikali.

"Tumepoteza nafasi na mapato. Hatuwezi kuendelea kusubiri tena. Je ni msaada gani na kiasi gani cha fedha mnahitaji kuweza kuanza tena kutoa huduma?," aliuliza Rais Kikwete katika mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na viongozi wa taasisi nyingine zilizoko chini ya Wizara ya Miundombinu, ikiwamo Mamlaka ya Usalama wa Anga (TCAA).

Rais alitoa maelekezo baada ya kuwa amepata maelezo ya kina kutoka kwa uongozi wa ATCL kuhusu matatizo ya karibuni ya kampuni hiyo, ambayo yalisababisha kuamriwa kusimamisha huduma kwa sababu ya kushindwa kutimiza masharti ya TCAA. "Nataka kujua kiini cha matatizo yetu ya karibuni mpaka tukasimamisha kurusha ndege zetu? Tulifikaje hapo?

Je tumetoka na kama tumetoka, tunafanya nini ili tusirudi kwenye matatizo hayo? Pili, nataka mnielezee mipango na hali ya baadaye ya shirika letu la ndege kibiashara," aliwaambia. Uongozi wa ATCL ulitoa maelezo ya kina na kufuatia mjadala ambao hatimaye ulifikia ukingoni mwa kikao kukubaliana kuhakikisha kuwa ATCL inaanza kutoa tena huduma zake haraka iwezekanavyo. Pamoja na kwamba ATCL imefunguliwa kuanza kutoa huduma zake, ndege zake hazijaanza kuruka kwa sababu mbalimbali ambazo ndizo Rais aliagiza zitafutiwe majawabu na ndege zianze kuruka tena haraka iwezekanavyo.

Pendekezo:
Kama tatizo lao ni pesa (kama Rais anavyoonesha kufikiria) napendekeza Serikali iwape ATCL bilioni 500!!! wataanza kuruka Jumatatu!
 
Mimi hiyo ya tuanze kuruka jumatatu ndio imenimaliza!!
 
Jk anaamrisha kama jeshini hahaha haya asubiri hizo hela aone zitakavyo m disappoint maana watatzitafuna hasa duu hy ndio yaitwa lala salamaaa......
 
Visingizio vya kushindwa au kutofanya jambo lolote kwa mtu mwenye mawazo ya kimasikini siku zote huwa ni ukosefu wa mtaji, ukosefu wa fedha au ukosefu wa fungu, vyovyote vile ili mradi kisingizio kilenge fedha.
Fedha halijawahi kuwa tatizo, tatizo kubwa kwa masikini wote duniani ni ukosefu wa ubunifu, mipango na utekelezaji wa mipango.
ATCL hawana Blue Print, ni vipi wataruka Jumatatu hii.
Hata kama ingekuwa ATCL wanasafiri kwa ungo, wangetakiwa kutoa Specification kwa msuka nyungo, si kila ungo unafaa kusafiria nyingine ni za kupepetea tu.

Siyo kazi ya MH Rais kuuliza ni shilingi ngapi zinahitajika ili shirika lifufuke.
Huku ni kukurupuka na kuddhani kwamba ili mradi wewe ni rais wa nchi basi unauwezo wa kuona na kutoa maoni sahihi.
Subiri wiki ijayo watamtajia tarakimu, siamekwisha wapa mwanya?

MH alitakiwa kuuliza kwa nini shirika limekufa! Baada ya kupata jibu alitakiwa kuunda jopo la wataalamu ili kujua ni vipi shirika linaweza kuundwa upya katika sura ya kibiashara.Pia kuhakikisha kwamba makosa yaliyoua shirika hayarudiwi tena.
Kama MH naye kabuma katika hilo angepeleka Muswada Bungeni kwa walio liunda shirika ili waone ni nini cha kufanya.

Maswali aliyojiuliza rais ni maswali ambayo Mkurugenzi na Bodi yake ndiyo wanastahili kujiuliza siyo yeye.

Tatizo la ATCL siyo fedha, tatizo la ATCL limo ndani ya uongozi wa shirika lenyewe, pia limo katika utepetevu wa sheria zinazoliunda shirika lenyewe na Donda ndugu liuwalo kila juhudi nchini Tanzania, UFISADI.

Huwezi kumpa uongozi wa Bodi ya shirika muhimu nyeti na gumu kuliongoza, shirika la ndege mtu kama Mustafa Nyang'anyi ukitegemea maajabu wakati mtu huyu siku zote ni kilaza wa nguvu. Kilichomfikisha hapo ni kujipendekeza tu.
Shule yenyewe tu alisoma kwa kulipua lipua, anagusa hapa na pale kesho anavaa joho na kofia picha nyingiiii.

Okay, Mwnyekiti wa bodi kashindwa yeye na bodi yake, bado tu Rais anang'ang'ania viongozi wa bodi iloshindwa wajipake wanja, au kama MH Obama alivyosema "Kumpaka Nguruwe lipstick" wao na ujinga wao na kujibadili na kuwa uwezo wa kutoa suluhisho.
Piga garagaza ua Nguruwe ni nguruwe tu hata akipakwa wanja ni pig tu.

MH Kikwete. Huku uhamishoni tunakoishi mtu au watu wakishindwa kazi kizembe kama walivyoshindwa akina Nyang'anyi, cha kwanza ni kuotesha nyasi kibarua au vibarua vyao cha pili ni kutafuta watu wenye uwezo,nia na maono ya kuifanya kazi hiyo na kuwapa kibarua cha kujenga upya pale vilaza waliposhindwa.

Nilitegemea Rais angechukua matatizo ya ATCL positively na kuamua kulisuka shirika letu la ndege upya na kulifanya liwe na sura ya limataifa inayoruhusu ukuaji, uwazi na utendaji unaoendana na karne hii ya 21.
Kifo cha shirika hili kimetokea kwa sababu kila kitu ndani ya ATCL hakiwezekani, shirika limejaa wanasiasa wababaishaji, walioshindwa katika siasa sasa wanalia pensheni kwenye shughuli nzito kama kuongoza shirika la ndege.

Kuongoza shirika la ndege kunataka mtu au watu wenye vichwa, siyo hao wapitao kila kona na majigambo wakidhani wana vichwa kumbe wamebeba matikiti maji juu ya shingo zao. hii hii hii!

MH Rais, hii niaibu ya kimataifa.
 
MH Kikwete. Huku uhamishoni tunakoishi mtu au watu wakishindwa kazi kizembe kama walivyoshindwa akina Nyang'anyi, cha kwanza ni kuotesha nyasi kibarua au vibarua vyao cha pili ni kutafuta watu wenye uwezo,nia na maono ya kuifanya kazi hiyo na kuwapa kibarua cha kujenga upya pale vilaza waliposhindwa.

Nilitegemea Rais angechukua matatizo ya ATCL positively na kuamua kulisuka shirika letu la ndege upya na kulifanya liwe na sura ya limataifa inayoruhusu ukuaji, uwazi na utendaji unaoendana na karne hii ya 21.
Kifo cha shirika hili kimetokea kwa sababu kila kitu ndani ya ATCL hakiwezekani, shirika limejaa wanasiasa wababaishaji, walioshindwa katika siasa sasa wanalia pensheni kwenye shughuli nzito kama kuongoza shirika la ndege.

Kuongoza shirika la ndege kunataka mtu au watu wenye vichwa, siyo hao wapitao kila kona na majigambo wakidhani wana vichwa kumbe wamebeba matikiti maji juu ya shingo zao. hii hii hii!

MH Rais, hii niaibu ya kimataifa.

Mwanakijiji,

Nina uhakika mkubwa sana, Mh. Rais anakitu kichwani mwake ambacho haikuwa wakati muafaka kukitoa...

Ukitaka kweli ndege ziruke haraka ili taifa lisiendelee kula hasara, ni vyema uache hao hao wabababishaji walirudishe hewani. kuliko kuanza kutikisa uongozi... nina uhakika by May, wengi hawatakuwepo kwenye hilo shirika.

Hoja yake ilikuwa ndege ziruke, alafu... tuangalie shirika litaendelea je... hii haimaanisha jamaa wamelala,,, mimi namwamini sana Dr. Shukuru ni mtu wa vitendo, result oriented, hapa tulipo kuna already wataalamu wanachunguza na watamletea report baada ya kukataa report ya nyanganyi...

Time will tell, vuta pumzi...

Mbona mlipiga makelele ya EPA na yakatokea...
 
Ina maana muda wote tangu ATCL ipate tatizo hakuwahi kukaa na hao jamaa wampe majibu ya hayo maswali?
Ana priorities zipi kama hili halikuwa mojawapo? Hivi jamaa amesoma Uchumi kweli?
Duh...
 
Jk anaamrisha kama jeshini hahaha haya asubiri hizo hela aone zitakavyo m disappoint maana watatzitafuna hasa duu hy ndio yaitwa lala salamaaa......

Nafikiri tatizo si JK bali msingi tuliojiwekea kuwa mwenye amri ni mmoja tu ,RAIS, na waliobaki ni wafatiliaji tu . Inashangaza kuona kuwa hali tuliyofikishwa na ATCL hakuna hatuwa yoyote ya kinidhamu iliyochukuliwa dhidi ya waliotupeleka hapa tulipo.

Angalau tungeona mtu mwenye dhamana kama waziri anachukuwa hatuwa basi labda tungejuwa kuwa waliopewa dhamana wanajali.

Kwa mpigo huu wa kuwa Rais awe mtaalamu wa kila fani nafikiri hatutoenda pahala. Na zitolew hizo bn500 na mtaalamu wa ubadhirifu na timu yake anazingojea.
 
Mwanakijiji,

Nina uhakika mkubwa sana, Mh. Rais anakitu kichwani mwake ambacho haikuwa wakati muafaka kukitoa...

Ukitaka kweli ndege ziruke haraka ili taifa lisiendelee kula hasara, ni vyema uache hao hao wabababishaji walirudishe hewani. kuliko kuanza kutikisa uongozi... nina uhakika by May, wengi hawatakuwepo kwenye hilo shirika.

Hoja yake ilikuwa ndege ziruke, alafu... tuangalie shirika litaendelea je... hii haimaanisha jamaa wamelala,,, mimi namwamini sana Dr. Shukuru ni mtu wa vitendo, result oriented, hapa tulipo kuna already wataalamu wanachunguza na watamletea report baada ya kukataa report ya nyanganyi...

Time will tell, vuta pumzi...

Mbona mlipiga makelele ya EPA na yakatokea...
Mkuu,hiyo post uliyoinukuu ni ya mwanakijiji kweli?
Or its some sort of obsession!!!
 
Jamani tanzania hapo hamna economists ??...hao ma prof chuo na all the bankers at bot and other institutions hawana hata draft ya tutatua hili tatizo?? solution ni kuondoa management ya juu yote na kuleta professionals from abroad for 5yrs while they train the remaining management intensely...then you ask them to re apply for their jobs while all positions are put open to the public wa compete na market!! ndo kilichobaki!! kuna vijana wapo wanaoweza kuendesha haya mashirika sema wanaishiwa kupewa desk jobs wizarani mpaka wana duwaaaa!! maoni tuu
 
Last edited:
solution ni kuondoa management ya juu yote na kuleta professionals from abroad for 5yrs while they train the remaining management intensely...then you ask them to re apply for their jobs while all positions are put open to the public wa compete na market!! ndo kilichobaki!! kuna vijana wapo wanaoweza kuendesha haya marika sema wanaishiwa kupewa desk jobs wizarani mpaka wana duwaaaa!! maoni tuu

From abroad??? This is a joke... right?? what do u mean by " professional from abroad"?
Mkuu kama nimekuelewa vizuri ..yaani waletwe watu kutoka nje kuja kufanya maajabu yepi? Nani kasema TZ hakuna wataalamu? tatizo limekuwa ni kushindwa kuweka mkakati mzuri kuwapata wazawa wenye historia ya utendaji mzuri, waendeshe taasis za umma.Mbona watz wamejaa tele kwenye private sector na hata mashirika ya kimataifa?Humuhumu JF kuna wataalam lukuki.WHY foreigners???

What needs to be done ni kutangaza kazi, watu watume maombi, wasailiwe na anayefanya vizuri na mwenye track record nzuri ya performance mahali kwinginewe apewe kazi on probation.Akivurunda pia atimuliwe.
 
Ziara ambazo mkuu ameanza zinadhihirisha udhaifu wake katika uongozi.Ni kweli kwamba maji yamemshinda na kinachoonekana hapa ameamua kufight mwenyewe.Hapa ndipo udhaifu wake unapoanzia,alitembela kla wizara na kutoa maelekezo. . .bahati mbaya wengi wa mawaziri wa wizara sasa si wale waliopokea maagizo by that time.mf Msollwa aliyepokea maagizo alipokuwa Elimu yupo kwingine na magembe aliyekuwa kwingine yupo elimu. anapofanya ziara hizi nilitegemea kuona kuona ama watu wanapongezwa kwa kazi au kuwajibishwa,badala yake Raisi amekuwa kama vile katibu mtendaji wa taasisi fulani kwa kushika mafaili na kuongoza vikao tena na Mashirika! Aibu! Badala ya Raisi kumwita Waziri ofisini ili atoe taarifa kaamua kwenda mwenyewe kuwafundisha wawekezaji jinsi ya kuwekeza! Baada ya miaka 3 anatembea kufuatilia maagizo aliyoyatoa, sasa anatoa maagizo mapya je baada ya miaka mingapi atafuatlia utekelezaji wa haya aliyoyatoa hususani kwa TRL na ATCL? Na mpaka amalize wizara zote na mashirika au taasisi zilizopo chini yake itachuku muda gani? Kwa utaratibu huu namshauri akifika katika wizara ya Elimu afanye kikao na bodi ya mikopo,kisha kikao na kila chuo cha eleimu ya juu.halafu vyou va ufundi,kisha akae kikao na kila shule ya sekondari,achilia mbali za msingi.Kwa utaratibu wa vikao hivi ninaona ni dalili ya kushindwa zaidi kuliko utendaji wake kam raisi!
 
Hata muwape bilioni 50000 hili shirika haliwezi kufufuka kwa sababu management yake haina capacity ya kumanage an AIRLINE period!! Binafsi ninawafahamu baadhi ya wajumbe wa bodi ya ATCL, ni watu wenye uwezo na ujuzi tosha na katika mazungumzo nao wao pia wanakili kuwa tatizo kubwa la ATCL ni udhaifu wa watendaji; kwahiyo hata ukibadilisha bodi na uongeze mtaji bila ya kubadilisha management utakuwa unatwanga maji kwenye kinu!! Kuipa management iliyopo fedha zaidi ni sawa na kujalibu kujaza maji kwenye pipa lililotoboka!!!
 
Ina maana muda wote tangu ATCL ipate tatizo hakuwahi kukaa na hao jamaa wampe majibu ya hayo maswali?
Ana priorities zipi kama hili halikuwa mojawapo? Hivi jamaa amesoma Uchumi kweli?
Duh...

Jamaa ni Mchumi mzuri tu, tatizo lake kuu ni kwamba haachi ushikaji kwani matatizo ya ATCL bad indicators zilijionyesha zamani saaana ambazo sio lazima uwe Mchumi kama yeye kwani hata mgambo wa pale Miono angekueleza jibu kuwa TOA MARA MOJA HUO UONGOZI! kwisha.Kwa wenzetu kitu kama hiki hawaruhusu"incopetent performance" katika kazi, wala kutoa nafasi ya wapuuzi wachache kuendelea kutia hasara, hivi ni huruma yake kuwa jamaa zake hao wana watoto? au washikaji watasota mtaani? kweli ana huruma lakini hiyo huruma iwe ni kule nyumbani Chalinze na sio kwenye ofisi ya watanzania na tayari alishatueleza kama sio kutudanganya kuwa he will be serious on issues, je hili la ATCL sio issue? jino likiuma unakunywa dawa ya kupoza na likizidi na kukunyima usingizi basi ng'oa lote mpaka mzizi na litupilie mbali utaweka hata la Bandia, that is ATCL
 
From abroad??? This is a joke... right?? what do u mean by " professional from abroad"?
Mkuu kama nimekuelewa vizuri ..yaani waletwe watu kutoka nje kuja kufanya maajabu yepi? Nani kasema TZ hakuna wataalamu? tatizo limekuwa ni kushindwa kuweka mkakati mzuri kuwapata wazawa wenye historia ya utendaji mzuri, waendeshe taasis za umma.Mbona watz wamejaa tele kwenye private sector na hata mashirika ya kimataifa?Humuhumu JF kuna wataalam lukuki.WHY foreigners???

What needs to be done ni kutangaza kazi, watu watume maombi, wasailiwe na anayefanya vizuri na mwenye track record nzuri ya performance mahali kwinginewe apewe kazi on probation.Akivurunda pia atimuliwe.

Labda hukunielewa sio kwa nia mbaya wala siasa...i am currently a masters student when professors and a number of experts from the business community come to my classes to give lectures, huwa najaribu sana kufikiria nyumbani and the stuff these guys talk about..they know their shit! Trust me..ndo maana nimeuliza hao wabongo experts wapo wapi?? i will give you an example of one of my telecoms law professor ambaye not only does he teach every week but he advises the chinese government , NASA and i can go on for ages...why cant our government hire people like this to come for 5yrs like i stated and train intensely..

naona unageuza post yangu kuwa kama nasema foreigners bora..lets jus be realistic sometimes...mashirika mangapi tumeyauwa??? Ma prof wangapi wa UD wanasit of soo many boards lakini kampuni bado zinakufa? I will have to agree na wadau hapo juu kwamba siasa na urafiki unaiua tanzania taratibu...by 2015 kwa kweli haitabiriki tutakuwa wapi as a nation...The EU saizi loves Rwanda its their pride and joy in Africa...sasa hivi tutaanza kwenda kuomba kazi kule even though they had the genocide not to long ago! inauma kwa kweli sometime...Good Governance and Accountability is the only way out...lasi ivyo tutazeeekea hapa JF kulalamika
 
Last edited:
Mkuu,naomba kutautiana nawewe katika hili.Please NO FOREIGNERS in solving this,sisi wenyewe tukijipanga vizuri inawezekana kabisa tukalikwamua shirika hili,tatizo hapa naona ni yaleyale ya kuoneana aibu,thus instead of firing someone we asks him,"how much do u want?".Kwa mwendo huu wa kutaka kuweka mvinyo mpya kwenye bilauri ya zamani hakika HATUTAFIKA!
BTW;
bado hatujausahau ule mzimu wa Net Group Solution,just think of how it costs us in dealing with them.
Itaendelea itakapobidi....
 
Mkuu,naomba kutautiana nawewe katika hili.Please NO FOREIGNERS in solving this,sisi wenyewe tukijipanga vizuri inawezekana kabisa tukalikwamua shirika hili,tatizo hapa naona ni yaleyale ya kuoneana aibu,thus instead of firing someone we asks him,"how much do u want?".Kwa mwendo huu wa kutaka kuweka mvinyo mpya kwenye bilauri ya zamani hakika HATUTAFIKA!
BTW;
bado hatujausahau ule mzimu wa Net Group Solution,just think of how it costs us in dealing with them.
Itaendelea itakapobidi....

Mheshimiwa NetGroup alex stewarts na upuuzi mwingine are not the foreign professionals im referring to..hivi kampuni are jokes, dili za wanasiasa..zingine hata a decent website hawana...hawana hata track record of work done elsewhere but wamepata contracts bongo...mimi naongelea legit experts internationally recognised...if u were in my shoes saizi nadhani ungenielewa vizuri through being fortunate enough to be lectured by these individuals ni hatari..sometimes mtu unaona aibu ku mention the state of affairs in your country.
 
Back
Top Bottom