Kwa hili Jenerali Uimwengu umewaacha mashabiki wako njia panda

Jenerali anajaribu tu kumkumbusha Kikwete kuwa dhamana ya kuchaguliwa (hata kama ni kwa kuchakachua - safari hii) kuwa kiongozi wa nchi ni dhamana kubwa amabayo kwa watu wengi ni sawa na kutafsiri kuwa anaonekana kama ni mkombozi. Na kwa mantiki hiyo, viongozi wengi hujisahau na kulewa madaraka, na kusahau dhima nzima ya wao kuwapo madarakani.

Pia amekwenda na dhana ya kunguru mwoga hukimbiza bawa lake; ili itakapotokea na kuonekana ameongea vibaya basi (kwa watu, hususani watawala) na ionekane si kwa dhamira mbaya. Muungwana anaomba radhi mapeeema. Yakiyomkuta huko nyuma yatosha; binadamu akiumwa na nyoka, akiona unyasi anaweweseka.

Labda sehemu ya pili ya hii barua, itatupatia mwanga zaidi. Ila hii iko kifasihi zaidi. Na tuisome tena na tena.
 
Jenerali anajaribu tu kumkumbusha Kikwete kuwa dhamana ya kuchaguliwa (hata kama ni kwa kuchakachua - safari hii) kuwa kiongozi wa nchi ni dhamana kubwa amabayo kwa watu wengi ni sawa na kutafsiri kuwa anaonekana kama ni mkombozi. Na kwa mantiki hiyo, viongozi wengi hujisahau na kulewa madaraka, na kusahau dhima nzima ya wao kuwapo madarakani.

Pia amekwenda na dhana ya kunguru mwoga hukimbiza bawa lake; ili itakapotokea na kuonekana ameongea vibaya basi (kwa watu, hususani watawala) na ionekane si kwa dhamira mbaya. Muungwana anaomba radhi mapeeema. Yakiyomkuta huko nyuma yatosha; binadamu akiumwa na nyoka, akiona unyasi anaweweseka.

Labda sehemu ya pili ya hii barua, itatupatia mwanga zaidi. Ila hii iko kifasihi zaidi. Na tuisome tena na tena.
 
Niliwahi kupata matatizo sana katika siku zangu za high school. Nilikuwa katika debate team (oh yeah, malumbano sijaanza leo) na katika philosophical debate kuna kitu kimoja kinaitwa "eminent criticism". Inajumuisha "rope a dope" style fulani, ambayo unaanza kwa kumsifia mpinzani wako, halafu mwisho unaweza kuonyesha kwamba hata baada ya sifa hizo za mpinzani wako bado ana mapungufu haya, haya na yale.

Wanaosikiliza vipindi vya bunge la Uingereza wanaweza kuwa familiar na jinsi wabunge wanaopinga serikali wanavyoanza kuibonda serikali kwa courteous, gracious remarks, halafu wanakwenda in for the kill. Sasa mimi nilivyoanza hivyo katika audience iliyonitegemea niende directly for the kill niliwapa a gasp watu wa team yangu, lakini by the time namalizia part yangu ya debate wakaelewa kwa nini nimefanya vile, ukim criticize mtu bila ya kuanza kusema chochote kuhusu uzuri wake unaweza kuonekana huna graces na umeamua ku focus kwenye ubaya tu, lakini ukimcriticize mtu baada ya ku point out uzuri, unaonyesha kwamba hata baada ya uzuri kuna mapungufu.

Tatizo letu leo, hata mtu akitoa diplomatic gracious remarks ambazo ni standard kwa wasomi, na zinaweza kuwa fluff, mtu anaonekana kama anafanya pandering. Tutafikia wakati hata states zinazotoa pongezi kwa Kikwete kushinda uchaguzi tutaziita za kifisadi, hatuendi hivyo. Mkubwa anasemwa vizuri tu akikosea, lakini kumnyima shikamoo yake kama head of state aliyechaguliwa na watu - however controversial, he is still the legal head of state - ni upungufu wa neema.

Kwa hiyo mimi sijaona cha msingi Ulimwengu alichomsifia JK, sanasana kwa wanaojua kusoma between the lines mpaka sasa Ulimwengu amesema kuhusu ahadi tu, na wala hajasema chochote kuhusu utekelezwaji wa ahadi kiufanisi.

Tusubiri kipande cha mwisho tujue vizuri anamalizia vipi, tusiwe kama watoto wa shule wasiojua "eminent criticism" ambao wakiona mtu kaanza na gracious remarks, climaxing the image of Kikwete in order to graphically juxtapose missed opportunities, sisi tunatafsiri kamuita Kikwete mkombozi, Ali akim-rope a dope mshindani wake raundi za mwanzo, wengine tunatafsiri kwamba kapigwa au kauza mechi, kabla hata ya kusubiri mpambano utakavyoisha.

Itakuwa si busara.
 
Kwa kuwa mazingira ya wakati huo na ya leo yanashabihiana sana, na kwa kuwa bado Barua ile Ndefu ya Wazi ina hoja ambazo zinatukumbusha yaliyopita na kututabiria yajayo, tunairejea barua hiyo ambayo maudhui yake yanabaki yaleyale hata kama imehaririwa hapa na pale kusahihisha makosa ya chapa.
Ni hapa tu Jenerali kachemsha kwa kudai mazingira ya sasa yanafanana na mazingira ya mwaka 2005. Kikwete wa mwaka 2005 hatukumjua na hakuna namna yoyote maudhui ya barua ya wakati huo yanaweza yakabaki yale yale hata yakihaririwa vipi. Nasubiri kusoma sehemu ya pili ya hii barua lakini kwa huu utangulizi, Jenerali amezua maswali ya utata kuliko majibu.

Mwaka 2005 ulikuwa wa matumaini lakini baada ya miaka mitano, Kikwete alichofanikiwa kwa kasi na ari ya ajabu ni kuwavunja mioyo Watanzania na kuzima ndoto zao. Binafsi sikumpigia kura kwa sababu sikuwa na sababu ya kufanya hivyo na kama kuna kitu najivunia hivi leo ni kumnyima hiyo kura ingawaje hilo halikuweza kumzuia huyu msanii kuingia ikulu.
 
Ulimwengu ni mwandishi mzuri mkuu, nadhani atakuwa ameandika kama MOCKERY au Joke fulani kumconscietize mkwere afumbue macho hata kama hataki kuyafumbua!
Hii ni mockery,kwanza Jenerali anasema anarudia kile alichokiandika miaka mitano iliyopita.Wakati huo mzee Mkapa ndo alikuwa anaondoka hivyo Jenerali na Watanzania kwa ujumla walimwona JK kama mkombozi kutoka kwenye mapungufu ya utawala wa Mzee Ben ambayo anayataja ni pamoja na kuongezka kwa bonde kati ya maskini wa kutupwa na matajiri wa kupindukia.Ushindi wa JK wakati huo ulidhiirisha imani na kiu ya wanainchi ya kupata mkombozi ambaye JK alionekana kubeba sifa zake.Miaka mitano baadaye Ulimwengu anamwandkia barua ileile sasa jifanye wewe ndo JK je idadi ya kura sasa hivi haionyeshi kuwa wengi wanatamani mkombozi mwingine?vita ya kupunguza pengo kati ya maskini na matajiri wa kutupwa limezalisha msamiati mpya wa Mafisadi hali ya kukata tamaa kwa maskini inaongezeka wengi wanatamani ndama wa shaba ndo maana hata kura hawapigi.Cha kujiuliza hapa je JK anatukomboa jutoka kwenye utawala wa nani?wakwake mwenyewe wa miaka mitano ilyopita?je JK huyu ndo yule ambaye Ulimwengu alimjua?JK kutukomboa kutoka kwenye utawala wa JK sasa hii si ndio MOCKERY yenyewe!!!Ulimwengu unatishaaa.
 
Jana nilisoma katika safu hizi, barua ndefu iliyoandikwa na Jenerali Ulimwengu kwa JK. Nianze kwa kukiri kwamba barua ya aina hiyo hiyo, niliwahi kuiona katika gazeti la Rai ama mwishoni mwa mwaka 2005 au mwanzoni mwa mwaka 2006. Kwa maoni yangu,barua hii ilipotokea kwa hiyo mara ya kwanza, ilikuwa inastahili. Lakini kwasasa, kwa baadhi yetu barua hiyo inatia kichefuchefu, kwani inapindisha ukweli ulivyo. Mwaka 2005 wakati JK anaingia madarakani watu wengi tuliamini ya kwamba sasa tumempata mkombozi wa kweli, ambaye angeliondoa nchi yetu katika shimo la ukoloni mamboleo, ambamo ilitumbukizwa na utawala wa Mkapa, na kuielekeza katika njia ya uhuru kamili kiuchumi. Miaka mitano ya uongozi wake, imekuwa ni ya kukatisha tamaa kwa yeyote yule mwenye mapenzi mema na nchi yetu. Chini ya uongozi wake siyo tu kwamba nchi yetu imeendelea kupoteza rasilimali nyingi kwa uporaji na matumizi mabaya ya serikali, lakini pia kuna kila dalili zinazodhihilisha ya kuwa nchi yetu kama taifa imepoteza mwelekeo.Hali hiyo imesababisha watu wengi kupoteza imani waliyokuwa nayo kwa JK. Kwanini basi, mtu kama Jenerali, kwa wakati huu tulionao, anaamua kupindisha ukweli huo na kuaanza kumuita JK mkombozi! naomba kwa yeyote mwenye jibu anitegulie kitendawili hicho.
Mimi naamini haujaisoma na kuielewa hilo toleo la kwanza barua hiyo:
Barua ndefu ya wazi kwa Jakaya
Kama umeisoma basi natilia mashaka uelewa wako au njia rahisi nikukuomba tu usubirie hadi hiyo barua itakapo kamilika ndio utoe maoni yako ila kwa haya ya leo huna jipya.
 
Nami nimesoma barua hiyo ndefu na kumshangaa sana Generali. Nimeona baadhi ya watu wanamtetea Generali kwamba labda wanaomlaumu eti hawajasoma barua yote. Hiyo siyo kweli kwani kama anavyokiri mwenyewe Generali, barua ni ileile aliyoitoa mwaka 2005 na akasisitiza kabisa kuwa maudhui ya barua yamebaki kama ilivyokuwa mwaka huo wa 2005. Jamani msimtetee sana kwani nae ni binadamu mwenye hulka kama binadamu wengine. Huenda kinachomsukuma nae ni uwezekano wa jk kumkumbuka katika ngwe yake hii ya mwisho. Bahati ya Salva Rweyemamu inaweza kumwangua nae pia japo siyo lazima kwa ulaji uleule. Kwa mtu makini haiingii akilini kuona barua ile ya mwaka 2005 eti maudhui yake yafanane na mwaka 2010 ambapo nchi imezingirwa na wingu la wasiwasi wa uhalali wa urais wa jk. Uhalali wenyewe unazungumwa katika maeneo mawili. Mosi, je, jk anajionaje anapotembea mitaani akiwa ni rais aliyechaguliwa na watu milioni 5 miongoni mwa watu wasiopungua 40 bila kujali umri wao!!!! Pili, hata ushindi wa asimilia 61 ya wananchi waliipiga kura, bado kuna fununu kwamba matokeo ya ubunge na urais yalichakachuliwa kwa lengo la kumrejesha madarakani jk. Sasa katika hali kama hiyo, ndipo Twaha Generali anaibuka na barua yake ndefu ambayo imejaa mapambo na sifa bandia kwa rais na ushauri lukuki wa namna ya kuweka mambo sawa kana kwamba hafahamu jinsi nchi ilivyopwaya chini ya uongozi wa jk. Ushahidi wa hoja hii ni makala zake nyingi tu anazoandika akipinga mambo mengi yanayofanywa na serikali ya jk.

Mwisho, nimalizie kwa jambo moja, kama kweli Generali yupo serious na barua yake hiyo ndefu, basi ccm itaendelea kutawala nchi hii milele na nguvu yake ambayo ndiyo siri ya ushindi huo ni 'njaa ya wananchi' wake na bahati mbaya njaa hiyo imemkumba hata mwandishi mahiri Generali.
 
Jana nilisoma katika safu hizi, barua ndefu iliyoandikwa na Jenerali Ulimwengu kwa JK. Nianze kwa kukiri kwamba barua ya aina hiyo hiyo, niliwahi kuiona katika gazeti la Rai ama mwishoni mwa mwaka 2005 au mwanzoni mwa mwaka 2006. Kwa maoni yangu,barua hii ilipotokea kwa hiyo mara ya kwanza, ilikuwa inastahili. Lakini kwasasa, kwa baadhi yetu barua hiyo inatia kichefuchefu, kwani inapindisha ukweli ulivyo. Mwaka 2005 wakati JK anaingia madarakani watu wengi tuliamini ya kwamba sasa tumempata mkombozi wa kweli, ambaye angeliondoa nchi yetu katika shimo la ukoloni mamboleo, ambamo ilitumbukizwa na utawala wa Mkapa, na kuielekeza katika njia ya uhuru kamili kiuchumi. Miaka mitano ya uongozi wake, imekuwa ni ya kukatisha tamaa kwa yeyote yule mwenye mapenzi mema na nchi yetu. Chini ya uongozi wake siyo tu kwamba nchi yetu imeendelea kupoteza rasilimali nyingi kwa uporaji na matumizi mabaya ya serikali, lakini pia kuna kila dalili zinazodhihilisha ya kuwa nchi yetu kama taifa imepoteza mwelekeo.Hali hiyo imesababisha watu wengi kupoteza imani waliyokuwa nayo kwa JK. Kwanini basi, mtu kama Jenerali, kwa wakati huu tulionao, anaamua kupindisha ukweli huo na kuaanza kumuita JK mkombozi! naomba kwa yeyote mwenye jibu anitegulie kitendawili hicho.

unadandia treni kwa mbele. Aliandika kuwa makala itaendelea toleo lijalo. Nani anajua kuwa atakuja na surprise gani? Navyomjua Jenerali kuna hoja anachokoza hapo na jibu utalipata nxt wk. Alitukumbusha ni jinsi gani jk alivyokuwa tarajio la ukombozi. Hata mi niliamini hadi nikashangaa kwa nini wapinzani wanasimamisha wagombea wa urais. Kama jk ana akili atakuwa anaumia moyo kwa kushindwa kutimiza matamanio ya watz na badala yake kuwa kituko. Ukimstaajabu Jenerali aliyeandika gazetini 2005 hujaona ya Bagenda aliyetunga kitabu kabisa akiamini kuwa jk ni tumaini lililorejea!
 
Jenerali aliandika barua hiyo 2006 hapo alikuwa anamuona JK kama mkombozi wa Taifa hili (Wengi wetu tulidhani hivyo) kuirudia ni kama kuamsha mjadala na kumkumbusha JK kwani iwavyo ndie Rais wetu hata kama kura zimechakuchuliwa yeye ndiye. kwa hiyo tusimlaumu Jenerali bali anatukumbusha tulikotoka kwa leo matumaini ya kuwa JK atatukomboa hayapo yupo kwa maslahi tuona hata Spika6 kachakachuliwa kwa sababu tu "AHHH NI MWANAUME!!!!" na bado mengi yanakuja
 
jana nilisoma katika safu hizi, barua ndefu iliyoandikwa na jenerali ulimwengu kwa jk. Nianze kwa kukiri kwamba barua ya aina hiyo hiyo, niliwahi kuiona katika gazeti la rai ama mwishoni mwa mwaka 2005 au mwanzoni mwa mwaka 2006. Kwa maoni yangu,barua hii ilipotokea kwa hiyo mara ya kwanza, ilikuwa inastahili. Lakini kwasasa, kwa baadhi yetu barua hiyo inatia kichefuchefu, kwani inapindisha ukweli ulivyo. Mwaka 2005 wakati jk anaingia madarakani watu wengi tuliamini ya kwamba sasa tumempata mkombozi wa kweli, ambaye angeliondoa nchi yetu katika shimo la ukoloni mamboleo, ambamo ilitumbukizwa na utawala wa mkapa, na kuielekeza katika njia ya uhuru kamili kiuchumi. Miaka mitano ya uongozi wake, imekuwa ni ya kukatisha tamaa kwa yeyote yule mwenye mapenzi mema na nchi yetu. Chini ya uongozi wake siyo tu kwamba nchi yetu imeendelea kupoteza rasilimali nyingi kwa uporaji na matumizi mabaya ya serikali, lakini pia kuna kila dalili zinazodhihilisha ya kuwa nchi yetu kama taifa imepoteza mwelekeo.hali hiyo imesababisha watu wengi kupoteza imani waliyokuwa nayo kwa jk. Kwanini basi, mtu kama jenerali, kwa wakati huu tulionao, anaamua kupindisha ukweli huo na kuaanza kumuita jk mkombozi! Naomba kwa yeyote mwenye jibu anitegulie kitendawili hicho.

naomba urudie kusoma hiyo makal tena, na tena, na tena labda mungu atakusaidia kuilewa kwani ina ujumbe mzito sana na inato maelekezo kwa watanzania walioibiwa kura zao ya nini kutarajia
.
 
Jana nilisoma katika safu hizi, barua ndefu iliyoandikwa na Jenerali Ulimwengu kwa JK. Nianze kwa kukiri kwamba barua ya aina hiyo hiyo, niliwahi kuiona katika gazeti la Rai ama mwishoni mwa mwaka 2005 au mwanzoni mwa mwaka 2006. Kwa maoni yangu,barua hii ilipotokea kwa hiyo mara ya kwanza, ilikuwa inastahili. Lakini kwasasa, kwa baadhi yetu barua hiyo inatia kichefuchefu, kwani inapindisha ukweli ulivyo. Mwaka 2005 wakati JK anaingia madarakani watu wengi tuliamini ya kwamba sasa tumempata mkombozi wa kweli, ambaye angeliondoa nchi yetu katika shimo la ukoloni mamboleo, ambamo ilitumbukizwa na utawala wa Mkapa, na kuielekeza katika njia ya uhuru kamili kiuchumi. Miaka mitano ya uongozi wake, imekuwa ni ya kukatisha tamaa kwa yeyote yule mwenye mapenzi mema na nchi yetu. Chini ya uongozi wake siyo tu kwamba nchi yetu imeendelea kupoteza rasilimali nyingi kwa uporaji na matumizi mabaya ya serikali, lakini pia kuna kila dalili zinazodhihilisha ya kuwa nchi yetu kama taifa imepoteza mwelekeo.Hali hiyo imesababisha watu wengi kupoteza imani waliyokuwa nayo kwa JK. Kwanini basi, mtu kama Jenerali, kwa wakati huu tulionao, anaamua kupindisha ukweli huo na kuaanza kumuita JK mkombozi! naomba kwa yeyote mwenye jibu anitegulie kitendawili hicho.

Tatizo la ngozi nyeusi ni "njaa". Wengi wetu tunaongozwa na njaa. Kumbuka uandishi wa Salva Rweyemamu na Muhingo Rweyemamu. Wengi wetu tulipigwa butwaa kusikia uteuzi wa hawa mabwana kwenye timu ya jk.
 
Ametuomba radhi mwanzo wa makala kuwa anarudia barua aliyomwandkia JK 2005 bila kubadili neno....tusimlaumu ila labda atujuve majibu ya barua yalikuwaje?ingawa mi nadhani hakujibiwa na ndio maana kakumbushia
 
JK aliingia mkenge alipokubali kushirikiana na wana mtandao ambao ndiyo hadi sasa hivi wamemfanya asiweze kufanya kazi. Kama angejua JK alikua anashinda bila hata hao wanamtandao kwa kipindi kile kwani alikua ametokea kupendwa na watanzania wengi. Ila sasa hivi wamemkaba shingoni hawezi kufanya kitu na anajikuta anakua mtumwa wa fikra zao na ufisadi wao. Jenerali hapa alikua anamkumbusha JK alikotoka, anajaribu kuonyesha alivyobadilika na sio anamsifia..!
 
Mkuu nafikiri hujaelewa mantiki ya Ulimwengu kurudiaile barua aliyomwandikia JK mwaka 2006 mara tu ya Jk kula kiapo cha kuiongoza Tanzania.

Ukiielewa kwa makini utagundua kwa nini Ulimwengu ameamua kuichapisha tena barua hiyo kwenye toleo la Raia Mwema la wiki iliyopita.

Jaribu kufuatilia makala ama hata mijadala ya Jenerali Ulimwengu na utagundua ni mtu wa calibre gani!!

Ndugu naona umesema vizuri kabisa! jamaa anaelewa achoandika , na kwa mtu anayeweza ku read between the lines ataelewa wazi, ukizingatia msimamo wake kwenye maandiko yake mbali mbali!!

Kwa uelewa wangu mdogo wa kifundi mchundo! ni kuwa jamaa hakufanya chochote huko nyuma, hali aliyokuta ni ile ile na labda imekuwa worse, hivyo barua ile ile ya 2006 iko valid leo!! jee nini maana ya hilo?
 
Nikiri mapema kuwa mimi binafsi ni shabiki wa jenerali ulimwengu.Ulimwengu ni role model wangu.Ile makala katika gazeti la RAIA MWEMA ni kweli iliwahi kutolewa mara tu baada ya JK kupata "ridhaa" ya kutawala.hapa niseme mambo mawili ambayo huenda yakasaidia kumwelewa jenerali

Mosi,Nikuwa baadhi ya maudhui ya barua hiyo ya wazi(makala) hayajafa na hayatakufa hata tutakapompata Rais wa kumi wa TZ.

Pili,Tumekimbilia kumjaji mapema ulimwengu hata kabla hajamalizia barua yake,kwani hatukusoma mwisho kuwa barua hiyo itaendelea wiki hii,naomba tuwe na subira tuone iwapo hitimisho la barua hiyo kama litakuwa limepitwa na wakati.Halafu wana jamvi tukumbuke kuwa changamoto zinazomkabili mama tanzania kwa sehemu kubwa ni zile zile tangu mwaka 2005!

Asahteni,mi mtembezi naendelea kutembea.
 
Jenerali aliandika barua hiyo 2006 hapo alikuwa anamuona JK kama mkombozi wa Taifa hili (Wengi wetu tulidhani hivyo) kuirudia ni kama kuamsha mjadala na kumkumbusha JK kwani iwavyo ndie Rais wetu hata kama kura zimechakuchuliwa yeye ndiye. kwa hiyo tusimlaumu Jenerali bali anatukumbusha tulikotoka kwa leo matumaini ya kuwa JK atatukomboa hayapo yupo kwa maslahi tuona hata Spika6 kachakachuliwa kwa sababu tu "AHHH NI MWANAUME!!!!" na bado mengi yanakuja

Nimeipenda hiyo ID na picha yako!unapendeza sana!inaonekana wewe ni msukuma!!!
 
hata mimi nilipoisoma nilishangaa kama imeandikwa na Jenerali Ulimwengu ninayemfahamu. Angekuwa kaandika Majid ningeelewa!!! Inawezekana labda ni ile ya 2006 ya gazeti ya Rai imewekwa kimakosa. Tusubiri labda wataomba radhi Jumatano hii. Otherwise, nitamwelewa Jenerali vibaya
 
Twaha Ulimwengu alipanda cheo katika medani ya habari na kuwa four-star General. Sasa anaporomoka na kuwa foot soldier, juzi aliandika lead story kwenye East African kama special correspondent!! Yaani from editor-in-chief of leading media house to a newspaper correspondent. Hii ya barua kwa JK nadhani anajipendekeza... amerudia hadithi ya walivyokutana Bulgaria, hivi kweli JK na English yake ilivyopinda na hoja nyepesi hali ilikuwaje alivyokuwa kijana hajapata exeperice? Bulgaria huko aliongea nini? ahahahahaha

Wakati fulani tuangalie threads zinazoletwa hapa kama zinabeba mantiki. Niliisoma makala hiyo na japo kwa sehemu ya kwanza tu hiyo unaweza kumwelewa ulimwengu, alikuwa anaeleza Kikwete aliyemfahamu na wengi tuliyomjua b4 2005 (na hata kumwona mwokozi) na kisha makala ijayo (kama alivyoichapisha mwaka 2005) atatoa hitimisho kama huyu ndo yule au vipi. Mwanzisha mada hakumwelewa, tunaochangia hatukusoma makala yenyewe, mwishowe ni kuchakachua kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom