HII NI MAKALA KATIKA GAZETI LA ANNUR LA LEO, UK 4
KWA HILI DK NDALICHAKO ANAHUSIKA
Nimeisoma makala katika gazeti la annur la februari 24 yenye kichwa cha habari " mchawi wa Zanzibar sio Joyce Ndalichako". Mwandishi wa makala hayo ambae alijitambulisha kama mwandishi maalum amejaribu kuonyesha mambo mengi yanahusu kushuka kwa elimu Zanzibar na kubwa zaidi amedai kwamba wanafunzi wa Zanzibar hawapaswi kumlaumu katibu mtendaji wa baraza la mitihani (NECTA) kwa matokeo ya shule zao.
Binafsi nakubaliana na baadhi ya hoja ya hoja za mwandishi wa makala hayo hasa katika swala zima la kuporomoka kwa maadili ya vijana, watoto hata wazazi kwa ujumla, lakini pia la mfumo wa elimu wa visiwani unahitaji ufanyiwe utafiti (research), kwa mfano hapo miaka ya nyuma wanafunzi wanaofanya vizuri darasa la saba na kuchaguluwa kujiunga na shule maalum (michepuo) walikuwa wakifanya vizuri sana katika mtihani wa kidato cha nne cha sita,Lakini sasa licha ya kuwa hivyo lakini imepungua kwa kiasi kikubwa.
Kwa mtazamo wa harakaharaka, wanafunzi wengi sasa wanaofanya vizuri ni wanafunzi wanaotoka shule za mjini Unguja, hizi ni shule za serekali kama Lumumba, Benbella, Kiponda , shule ya Ufundi Mikunguni ambayo mwkaa huu imekubwa na fagio la NECTA na shule ya Biashara Mombasa. Kwa upande wa shule za watu binafsi (private)au mashirika ni ni shule kama SOS, sunny Medrasa ,shule ya wanawake Al ihsani , high view na Lauret ambazo mwaka huu nazo zimekumbana an fyagio la Chuma la NECTA.
Kwa upande wa kisiwa cha Pemba shule zinazoleta afueni ni shule ya Utaani ya Wete ,shule ya ya Ufundi Kengejana shule maarufu ya Fidel-Castro iliopo chake Chake .
Hii ni changamoto kubwa kwa wazazi , serekali na wanafunzi kwa ujumla, hapa unatakiwa ufanyike Utafiti wa kina kwanini hali hii inazidi kuongezeka siku hadi siku huku wazee wakitumia gharama kubwa ya kuwasomesha watoto wao kwa matumaini ya kujikomboa kielimu.
Lakini juu ya matokeo ya 2011 kwa upande wa Zanzibar, hapa ni wazi Dk Ndalichako anahusika, sijawahi kuona matokeo ya kushangaza ya mtihani wa taifa yakitolowa kama ilivyotokea haya ya 2011 hapa Tanzania ,nimetembelea nchi nyingi na pia kusikiliza vyombo vingi vya habari vya kimatifa lakini sijasikia popote pale baraza la mitihani lilitumia mkokoto wake kupata matokeo ya mtihani wa taifa kama ulivyotumika 2011.nimesoma darasa la kwanza hadi kumaliza shahada ya pili ya masmo yangu sijabahatika kuona Chuo au taasisi yoyote nchini imetoa matokeo ya mtihani kama ilivyofanya NECTA.
, Wanafunzi 52 wa chumba kimoja wanafutiwa matokeo na anabaki mmoja!, wanafunzi 150 wa shule moja wanafutiwa wanabaki 10 tena hao waaliobaki wanaambulia daraja la nne!,shule moja inafutiwa, shule ya jirani haiguswi hata kidogo !huku Katibu mtendaji wa NECTA anatamka kwamba NECTA ni chombo makini katika utendaji wake!Upi utendaji ulioutuka wa NECTA hapa, ni kuwafutia watoto huku baraza hilo likishtumiwa na kila mdau kwamba kimeshindwa kusimamia mitihani kwa umakini?
Ukiskiliza mijadala mingi kwenye mitandao utagundua wasiokuwa waislam wanasema waislam hawana uwezo wa kusoma ndio maana shule za Zanzibar na za waislam matokeo yao sio mazuri. Lakini tujiuliza?Lakni tujiulize jee waislam hawasomi katika mitihani ya NECTA tu?mbona mitihani ya NACTE (Baraza la vyuo vya ufundi) hufanya vizuri sana? Mbona wanabaohataika kuingia vyuo vikuu na daraja la Tatu la NECTA hufanya vizuri ? Jee Chuo kikuu cha waislam Morogoro kinaendeshwa na wasiokuwa waislam? mbona vyuo vikuu vya Zanzibar navyo vimejaa waislam na Wazanzibar huku wengine wakikosa nafasi? Mbona idadi kubwa ya wakufunzi wa vyuo hivyo vya Zanzibar ni waislam na vinaendeshwa kwa uwezo mkubwa pengine hata hivi vyuo vikuu vya madhehebu ya dini?
Nilipata kuongea na wanafunzi waliofanya mtihani 2011, waliofutiwa na waliobahatika kupenya kwenye tundu la NECTA. Wengi wamefikia hatua ya kuwataka walimu sasa watumie njia ya kuwafundisha wanafunzi wao jinsi ya kuujibu mtihani uliovuja ili majibu yasilengane kati ya mwanafunzi na mwanafunzi, wanaamini NECTA haiwezi tena kufanya mtihani uwe salama. Jee hali ikifikia hivi, nini tutegemee taifa letu kielimu?
.Uaminifu kuanzia baraza la mitihani hadi kumfikia mwanafunzi wanataka uchunguzwe kwa makini, Baraza la mitihani linatakiwa litupiwe jicho kali na wabunge , wanaharakati na hata vyombo vya habari, vyenginevyo tutegemee maafa makubwa ya elimu kwa vijana wetu, sio kwa upande wa Zanzibar hata Tanzania bara. Ni vigumu kupatikana mtihani Zanzibar usivuke bahari.
Inaonekana NECTA haipo tayari tena kubeba lawama juu ya yale wanayoyatenda wenyewe na kuwabebesha mzigo huu wanafunzi na wazee jambo ambalo ni hatari kwa taifa letu. NECTA inaonekana haitaki kukiri kwamba baadhi ya watendaji wa baraza hilo sio waaminifu katika swala la kutunza mitihani, haitaki kukiri kwamba njia wanazotumia kuitunza nz kuisambaza mitihani inakasoro, wanachofanya sasa ni kuwachukulia hatua kali wanafunzi wanaohisi tu wamedanganya kwenye chumba cha mtihani huku kuvuja mitihani sio tena ajenda yao, pengine wanahisi wakijiingiza kwenye matamko ya uvujaji wa mitihani wengi wataziacha ofisi hizi za umma kutokana na matamko yatayofuata ya wanaharakati na vyombo vya habari, sasa wanasema "liache liende tu zikija karatai zao za majibu mkononi mwetu tutawaadhibu ili tulinde Unga wetu" hata wakipiga kelele hazitozidi za wabunge na wanaharakati. Hii ndio NECTA iliopewa jukumu la kusimamia maisha ya watoto wetu .
Tukumbuke baadhi ya wabunge waliwahi kulituhumu baraza hili kwamba haliwezi kuutunza mtihani, kwa hivyo baadhi ya watendji wake waondoshe hasa Dk Ndalichako , haya ndio matunda ya baraza hilo kwa watoto wetu ya kufutiwa matokeo huku uzembe ukianzia kwenye baraza. Hii ni hatari kwa taifa changa kama letu ambapo njia pekee ya kumkomboa mtoto ni elimu.mwanafunzi anaeshtumiwa tu amekopi adhabu yake miaka mitatu kutofanya mtihani, jee kijana huyu mdogo aliebeshwa zigo la NECTA afanye nini? Lakini kwa bahati mbaya sijawahi kumsikia afisa yoyote wa NECTA akipewa adhabu ya kutokana uvujai wa mitihani, wapo an wanaendelea kupeta huku watoto ndio muhanga wa uzembe wa NECTA. Sote tunajua mtihani ni swala nyeti, ndio maana vyumba vyote vya kuhifadhia mitihani kuanzia shule ya msingi hadi vyuo vikuu vinaulinzi mkali, komputa inayotumika kuchpiwa mtihani haitakiwi iguswa na asiehusika .
Shule nyingi za Zanzibar zimefutiwa matokeo, shule ya Kiislam Unguja kati ya 52, ni 1 tu alesalimika, Shule ya kiislam pemba wao wote wamesambaratika, Hamani, Sufa, High view, Lauret , Jangombe, regeza mwendo na nyengine nyingi zimekubwa na sakatata. Hili tujiuilize kwanini iwe 2011 na isiwe 2010, 2009 au hata 2007?
Hoja kubwa ya Dk Ndalichako kwamba walimu an wasimamizi wamehusika kwa kiasi kikubwa, swali la kujiuliz, hivi nani anateu wasimamizi hawa?
Hawa si ndio wasimamizi wanaoaminika na NECTA na kufanya vizuri kila mwaka? Iweje 2011 wabadilike an waungane na wanafunzi kuihujumu NECTA?lakini hata huo ushahidi wa NECTA kuwafutia wanafunzi wameupata wapi? Hawa si ndio waliokusanya na kuupeleka NECTA?au tuseme maofisa wa NECTA walifunga kambi Zanzibar?au tuamini NECTA waliafnya maamuzi haya wakiwa juu ya meza bila ya ushahidi makini?
Lakini pia hoja ya pili kwamba wanafunzi wakipeana vikratasi kwenye chumba mtihani. Hapa tunatakiwa tujiulize, chumba(bwawa) chenye wanafunzi 100 wakipena karatasi chumba hicho kitakuwa hali gani? Sio fujo, kelele za peleka hapa niletee hiyo? Jee usalama wa mitihani ulikuwa wapi tena hapo? Hawa waliosalimika walikaa vyumba vya pekee yao?polisi waliopewa ulinzi wa vyumba vya mtihani walikuwa likizo?
Pia hoja kwamba majibu ya wanafunzi yanalingana katika shule moja nayo ni hoja inayohatiji ufafanuzi zaidi, ni vigumu kama majibu haya hayakuandaliwa nje ya chumba tena siku moja kabla ya mtihani, haya sio majibu ya ndani ya chumba kwa masaa matatu.
Juhudi za pamoja zinatakiwa ili kuwakomboa watoto wetu kielimu, njia pekee ni kuangalia upya utendaji wa NECTA.
mwandishi amejitambulisha ni
Juma Said
Mob 0652 013301
KWA HILI DK NDALICHAKO ANAHUSIKA
Nimeisoma makala katika gazeti la annur la februari 24 yenye kichwa cha habari " mchawi wa Zanzibar sio Joyce Ndalichako". Mwandishi wa makala hayo ambae alijitambulisha kama mwandishi maalum amejaribu kuonyesha mambo mengi yanahusu kushuka kwa elimu Zanzibar na kubwa zaidi amedai kwamba wanafunzi wa Zanzibar hawapaswi kumlaumu katibu mtendaji wa baraza la mitihani (NECTA) kwa matokeo ya shule zao.
Binafsi nakubaliana na baadhi ya hoja ya hoja za mwandishi wa makala hayo hasa katika swala zima la kuporomoka kwa maadili ya vijana, watoto hata wazazi kwa ujumla, lakini pia la mfumo wa elimu wa visiwani unahitaji ufanyiwe utafiti (research), kwa mfano hapo miaka ya nyuma wanafunzi wanaofanya vizuri darasa la saba na kuchaguluwa kujiunga na shule maalum (michepuo) walikuwa wakifanya vizuri sana katika mtihani wa kidato cha nne cha sita,Lakini sasa licha ya kuwa hivyo lakini imepungua kwa kiasi kikubwa.
Kwa mtazamo wa harakaharaka, wanafunzi wengi sasa wanaofanya vizuri ni wanafunzi wanaotoka shule za mjini Unguja, hizi ni shule za serekali kama Lumumba, Benbella, Kiponda , shule ya Ufundi Mikunguni ambayo mwkaa huu imekubwa na fagio la NECTA na shule ya Biashara Mombasa. Kwa upande wa shule za watu binafsi (private)au mashirika ni ni shule kama SOS, sunny Medrasa ,shule ya wanawake Al ihsani , high view na Lauret ambazo mwaka huu nazo zimekumbana an fyagio la Chuma la NECTA.
Kwa upande wa kisiwa cha Pemba shule zinazoleta afueni ni shule ya Utaani ya Wete ,shule ya ya Ufundi Kengejana shule maarufu ya Fidel-Castro iliopo chake Chake .
Hii ni changamoto kubwa kwa wazazi , serekali na wanafunzi kwa ujumla, hapa unatakiwa ufanyike Utafiti wa kina kwanini hali hii inazidi kuongezeka siku hadi siku huku wazee wakitumia gharama kubwa ya kuwasomesha watoto wao kwa matumaini ya kujikomboa kielimu.
Lakini juu ya matokeo ya 2011 kwa upande wa Zanzibar, hapa ni wazi Dk Ndalichako anahusika, sijawahi kuona matokeo ya kushangaza ya mtihani wa taifa yakitolowa kama ilivyotokea haya ya 2011 hapa Tanzania ,nimetembelea nchi nyingi na pia kusikiliza vyombo vingi vya habari vya kimatifa lakini sijasikia popote pale baraza la mitihani lilitumia mkokoto wake kupata matokeo ya mtihani wa taifa kama ulivyotumika 2011.nimesoma darasa la kwanza hadi kumaliza shahada ya pili ya masmo yangu sijabahatika kuona Chuo au taasisi yoyote nchini imetoa matokeo ya mtihani kama ilivyofanya NECTA.
, Wanafunzi 52 wa chumba kimoja wanafutiwa matokeo na anabaki mmoja!, wanafunzi 150 wa shule moja wanafutiwa wanabaki 10 tena hao waaliobaki wanaambulia daraja la nne!,shule moja inafutiwa, shule ya jirani haiguswi hata kidogo !huku Katibu mtendaji wa NECTA anatamka kwamba NECTA ni chombo makini katika utendaji wake!Upi utendaji ulioutuka wa NECTA hapa, ni kuwafutia watoto huku baraza hilo likishtumiwa na kila mdau kwamba kimeshindwa kusimamia mitihani kwa umakini?
Ukiskiliza mijadala mingi kwenye mitandao utagundua wasiokuwa waislam wanasema waislam hawana uwezo wa kusoma ndio maana shule za Zanzibar na za waislam matokeo yao sio mazuri. Lakini tujiuliza?Lakni tujiulize jee waislam hawasomi katika mitihani ya NECTA tu?mbona mitihani ya NACTE (Baraza la vyuo vya ufundi) hufanya vizuri sana? Mbona wanabaohataika kuingia vyuo vikuu na daraja la Tatu la NECTA hufanya vizuri ? Jee Chuo kikuu cha waislam Morogoro kinaendeshwa na wasiokuwa waislam? mbona vyuo vikuu vya Zanzibar navyo vimejaa waislam na Wazanzibar huku wengine wakikosa nafasi? Mbona idadi kubwa ya wakufunzi wa vyuo hivyo vya Zanzibar ni waislam na vinaendeshwa kwa uwezo mkubwa pengine hata hivi vyuo vikuu vya madhehebu ya dini?
Nilipata kuongea na wanafunzi waliofanya mtihani 2011, waliofutiwa na waliobahatika kupenya kwenye tundu la NECTA. Wengi wamefikia hatua ya kuwataka walimu sasa watumie njia ya kuwafundisha wanafunzi wao jinsi ya kuujibu mtihani uliovuja ili majibu yasilengane kati ya mwanafunzi na mwanafunzi, wanaamini NECTA haiwezi tena kufanya mtihani uwe salama. Jee hali ikifikia hivi, nini tutegemee taifa letu kielimu?
.Uaminifu kuanzia baraza la mitihani hadi kumfikia mwanafunzi wanataka uchunguzwe kwa makini, Baraza la mitihani linatakiwa litupiwe jicho kali na wabunge , wanaharakati na hata vyombo vya habari, vyenginevyo tutegemee maafa makubwa ya elimu kwa vijana wetu, sio kwa upande wa Zanzibar hata Tanzania bara. Ni vigumu kupatikana mtihani Zanzibar usivuke bahari.
Inaonekana NECTA haipo tayari tena kubeba lawama juu ya yale wanayoyatenda wenyewe na kuwabebesha mzigo huu wanafunzi na wazee jambo ambalo ni hatari kwa taifa letu. NECTA inaonekana haitaki kukiri kwamba baadhi ya watendaji wa baraza hilo sio waaminifu katika swala la kutunza mitihani, haitaki kukiri kwamba njia wanazotumia kuitunza nz kuisambaza mitihani inakasoro, wanachofanya sasa ni kuwachukulia hatua kali wanafunzi wanaohisi tu wamedanganya kwenye chumba cha mtihani huku kuvuja mitihani sio tena ajenda yao, pengine wanahisi wakijiingiza kwenye matamko ya uvujaji wa mitihani wengi wataziacha ofisi hizi za umma kutokana na matamko yatayofuata ya wanaharakati na vyombo vya habari, sasa wanasema "liache liende tu zikija karatai zao za majibu mkononi mwetu tutawaadhibu ili tulinde Unga wetu" hata wakipiga kelele hazitozidi za wabunge na wanaharakati. Hii ndio NECTA iliopewa jukumu la kusimamia maisha ya watoto wetu .
Tukumbuke baadhi ya wabunge waliwahi kulituhumu baraza hili kwamba haliwezi kuutunza mtihani, kwa hivyo baadhi ya watendji wake waondoshe hasa Dk Ndalichako , haya ndio matunda ya baraza hilo kwa watoto wetu ya kufutiwa matokeo huku uzembe ukianzia kwenye baraza. Hii ni hatari kwa taifa changa kama letu ambapo njia pekee ya kumkomboa mtoto ni elimu.mwanafunzi anaeshtumiwa tu amekopi adhabu yake miaka mitatu kutofanya mtihani, jee kijana huyu mdogo aliebeshwa zigo la NECTA afanye nini? Lakini kwa bahati mbaya sijawahi kumsikia afisa yoyote wa NECTA akipewa adhabu ya kutokana uvujai wa mitihani, wapo an wanaendelea kupeta huku watoto ndio muhanga wa uzembe wa NECTA. Sote tunajua mtihani ni swala nyeti, ndio maana vyumba vyote vya kuhifadhia mitihani kuanzia shule ya msingi hadi vyuo vikuu vinaulinzi mkali, komputa inayotumika kuchpiwa mtihani haitakiwi iguswa na asiehusika .
Shule nyingi za Zanzibar zimefutiwa matokeo, shule ya Kiislam Unguja kati ya 52, ni 1 tu alesalimika, Shule ya kiislam pemba wao wote wamesambaratika, Hamani, Sufa, High view, Lauret , Jangombe, regeza mwendo na nyengine nyingi zimekubwa na sakatata. Hili tujiuilize kwanini iwe 2011 na isiwe 2010, 2009 au hata 2007?
Hoja kubwa ya Dk Ndalichako kwamba walimu an wasimamizi wamehusika kwa kiasi kikubwa, swali la kujiuliz, hivi nani anateu wasimamizi hawa?
Hawa si ndio wasimamizi wanaoaminika na NECTA na kufanya vizuri kila mwaka? Iweje 2011 wabadilike an waungane na wanafunzi kuihujumu NECTA?lakini hata huo ushahidi wa NECTA kuwafutia wanafunzi wameupata wapi? Hawa si ndio waliokusanya na kuupeleka NECTA?au tuseme maofisa wa NECTA walifunga kambi Zanzibar?au tuamini NECTA waliafnya maamuzi haya wakiwa juu ya meza bila ya ushahidi makini?
Lakini pia hoja ya pili kwamba wanafunzi wakipeana vikratasi kwenye chumba mtihani. Hapa tunatakiwa tujiulize, chumba(bwawa) chenye wanafunzi 100 wakipena karatasi chumba hicho kitakuwa hali gani? Sio fujo, kelele za peleka hapa niletee hiyo? Jee usalama wa mitihani ulikuwa wapi tena hapo? Hawa waliosalimika walikaa vyumba vya pekee yao?polisi waliopewa ulinzi wa vyumba vya mtihani walikuwa likizo?
Pia hoja kwamba majibu ya wanafunzi yanalingana katika shule moja nayo ni hoja inayohatiji ufafanuzi zaidi, ni vigumu kama majibu haya hayakuandaliwa nje ya chumba tena siku moja kabla ya mtihani, haya sio majibu ya ndani ya chumba kwa masaa matatu.
Juhudi za pamoja zinatakiwa ili kuwakomboa watoto wetu kielimu, njia pekee ni kuangalia upya utendaji wa NECTA.
mwandishi amejitambulisha ni
Juma Said
Mob 0652 013301